Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Wiki hii nimekutana matukio mawili ambayo pamoja na umri wangu huu yamenitoa machozi. Tukio mojawapo ni hili la bibi kizee mwenye umri wa miaka zaidi 100 kubakwa kwa zaidi ya saa 8 (hadi usiku wa manane) na kutelekezwa bila matibabu.
Tukio hili limetokea hivi karibuni huko Nzega, Tabora; katika kijiji cha Mwantoba, kata ya Bukene na kuripotiwa na Pendo Omary katika gazeti la Dira ya Mtanzania la 21-23 Novemba 2011. Bibi huyo amepata maumivu makali ya kifua, sehemu za siri na pia alichomwa na mti kwenye mguu. Mbaya zaidi ndugu na jamaa zake wamekosa shilingi 25000 (elfu ishirini na tano tu) kwa ajili ya kumpatia matibabu. Pia polisi wamekataa kumchukulia hatua mbakaji na pia uongozi wa kijiji nao hauna mpango wa kumsaidia huyu bibi ingawa mhusika yuko pale pale kijijini anatanua!!
Hili tukio si tu limenigusa bali limenisababishia kero ya aina yake kwa kuona jinsi ambavyo watu waliopewa dhamana ya kusimamia uhai na maslahi yetu wanavyofurahia mateso ya bibi, mama, dada na ndugu zetu wengine.
Kwa wale ambao watapenda kumsaidia huyu bibi walau apate matibabu au msaada wa kisheria, wawasiliane na Mhariri wa gazeti (Dira ya Mtanzania, 0655 063 839 au diramtanzania@yahoo.com) au mwandishi mwenyewe (Pendo Omary, 0716 3728 07 au Ommygarl@yahoo.com).
Tukio hili limetokea hivi karibuni huko Nzega, Tabora; katika kijiji cha Mwantoba, kata ya Bukene na kuripotiwa na Pendo Omary katika gazeti la Dira ya Mtanzania la 21-23 Novemba 2011. Bibi huyo amepata maumivu makali ya kifua, sehemu za siri na pia alichomwa na mti kwenye mguu. Mbaya zaidi ndugu na jamaa zake wamekosa shilingi 25000 (elfu ishirini na tano tu) kwa ajili ya kumpatia matibabu. Pia polisi wamekataa kumchukulia hatua mbakaji na pia uongozi wa kijiji nao hauna mpango wa kumsaidia huyu bibi ingawa mhusika yuko pale pale kijijini anatanua!!
Hili tukio si tu limenigusa bali limenisababishia kero ya aina yake kwa kuona jinsi ambavyo watu waliopewa dhamana ya kusimamia uhai na maslahi yetu wanavyofurahia mateso ya bibi, mama, dada na ndugu zetu wengine.
Kwa wale ambao watapenda kumsaidia huyu bibi walau apate matibabu au msaada wa kisheria, wawasiliane na Mhariri wa gazeti (Dira ya Mtanzania, 0655 063 839 au diramtanzania@yahoo.com) au mwandishi mwenyewe (Pendo Omary, 0716 3728 07 au Ommygarl@yahoo.com).