ni vema ukasema ni Rais yupi wa Tanzania aliyemaliza awamu zake zote bila kutembeza bakuli?Uhuru wa maoni bila kusikilizwa? sema kawa bubu kwenye midani za siasa na sio democrasia hana la maana alilofanya zaidi ya kuwa omba omba na kuwafaidisha washikaji zake
Ni kweli vyombo vya habari kwa kiasi vimefaidi uhuru sijasikia zile kauli za kuponda waandishi wa nyumbani na kusifia wa ugenini. Lakini kazi yake moja ambayo itampa jina kuliko wote waliomtangulia ni kutuletea katiba mpya ambayo Watanzania tunaihitaji. Kwa sababu kila mwenye akili anajua kuwa katiba mbovu ndiyo kiini cha mikataba mibovu na maamuzi ya ovyo katika ngazi mbali mbali za kiutendaji serikalini. Kwa hiyo tumuombee kwa Mungu katika mwaka mpya ujao alione na kulisimamia hili kwa haki.
NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA WANA JF WOTE