hili moja ya mambo muhimu sana ambayo JK kalifanyia hili Taifa!!!

Papa D

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
753
182
Katoa uhuru mkubwa kwa vyama vya siasa na watanzania kwa ujumla. uhuru wa kutoa maoni umeongezeka katika mwaka wa 2011!!
kwa hili hata wanaomchukia jitahidini kumpongeza!!
 
Ni kweli vyombo vya habari kwa kiasi vimefaidi uhuru sijasikia zile kauli za kuponda waandishi wa nyumbani na kusifia wa ugenini. Lakini kazi yake moja ambayo itampa jina kuliko wote waliomtangulia ni kutuletea katiba mpya ambayo Watanzania tunaihitaji. Kwa sababu kila mwenye akili anajua kuwa katiba mbovu ndiyo kiini cha mikataba mibovu na maamuzi ya ovyo katika ngazi mbali mbali za kiutendaji serikalini. Kwa hiyo tumuombee kwa Mungu katika mwaka mpya ujao alione na kulisimamia hili kwa haki.
NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA WANA JF WOTE
 
Uhuru wa maoni bila kusikilizwa? sema kawa bubu kwenye midani za siasa na sio democrasia hana la maana alilofanya zaidi ya kuwa omba omba na kuwafaidisha washikaji zake
 
Uhuru wa maoni bila kusikilizwa? sema kawa bubu kwenye midani za siasa na sio democrasia hana la maana alilofanya zaidi ya kuwa omba omba na kuwafaidisha washikaji zake
ni vema ukasema ni Rais yupi wa Tanzania aliyemaliza awamu zake zote bila kutembeza bakuli?
Ububu hiyo si kweli maana mara kadhaa amekuwa akiwajibu walomsema na kumshutumu. mfano wakti anatoa msimamo wa kusaini mswada wa marekebisho ya katiba mpya. Pia tambua si kila jambo rais atalijibu kwenye vyombo vya habari!!
Angalizo amekuwa msikivu kwa raia wake mifano hii miwili inatosha kujiridhisha usikivu wake:-
1. wale wachimba madini walipouawa halafu polisi wakataka kizuba, aliingilia kati matokeo yake wahusika walifikishwa mahakamani
2. Wananchi walipompigia kelele Jairo amewasikiliza na kumuondoa
.

Kuna mifano mingi sana! hata ule wa kusukuma muafaka Zanzibar ili kuzuia maafa! hili jambo lilimshinda Mkapa na kusababisha maafa!
 
nani wa kumpongeza?huyu jk aliyeileta richmond aahhhh hapana.Yeye ashukuru tu NECna UWT walimpa urais.
 
Ni kweli vyombo vya habari kwa kiasi vimefaidi uhuru sijasikia zile kauli za kuponda waandishi wa nyumbani na kusifia wa ugenini. Lakini kazi yake moja ambayo itampa jina kuliko wote waliomtangulia ni kutuletea katiba mpya ambayo Watanzania tunaihitaji. Kwa sababu kila mwenye akili anajua kuwa katiba mbovu ndiyo kiini cha mikataba mibovu na maamuzi ya ovyo katika ngazi mbali mbali za kiutendaji serikalini. Kwa hiyo tumuombee kwa Mungu katika mwaka mpya ujao alione na kulisimamia hili kwa haki.
NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA WANA JF WOTE

Naogopa Ban kuchangia hii
 
Back
Top Bottom