Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,994
- 144,329
Watanzania sasa tunavuna kile tulichopanda baada ya kupeleka wawakilishi wengi wa chama kimoja ambao wao kwao kitu muhimu ni chama kwanza na mwananchi baadae.Inasikitisha kuona namna ambavyo wanatumia wingi wao bungeni kupitisha mambo ambayo hayana tija na mwisho wa siku anaeumia ni mwananchi wa kawaida.
Katika mambo ambayo nilitarajia wangesimama kidete ni kuhakikisha mishahara ya watumishi inapunguziwa kodi kwani mishahara ni midogo sana na bado inatozwa kodi kubwa.Wao wenyewe wanaona posho ya sh 150,000 kwa siku haitoshi sasa mbona hawajiuliza huyu mtumishi ataishi vipi kwa mshahara wa sh 170,000 kwa mwezi.
Jambo lingine miongoni mwa mengi ya kuudhi ni kuona wameruhusu kampuni ya Kiwira itengewe sh bilioni 40 licha ya hasara kubwa iliyosababishwa na mwekezaji wa mgodi huu.Kwanini hawakupinga jambo hili la kifisadi!Hivi hizo pesa zingeelekezwa kwa madaktari si zingeepusha mgomo.Hata kama si kwa madaktari zingeweza kusaidia ktk maeneo mengine.
Hiyo ni mifano michache tu ya mapungufu ambayo ni ya wazi kabisa lakini watu hawa wameziba masikio na kutia pamba masikionoi wakiwaacha watanzania wanaangamia ktk dimbwi la umasikini.Na kinachouma ni kuona namna ambavyo wanashangilia na kupiga meza kanakwamba wamepata uungwaji mkono kutoka kwa wanaowawakilisha.Sijui labda huwa wanapigiwa simu za pongezi baada ya kupitisha.
Mh.Tundu Lisu aliposema this is another silly season hakukosea kabisa na mimi naunga mkono kauli yake kwa asilimia mia moja kama wao wanavyounga mkono kwa asilimia mia moja hizo bajeti tata.
Acheni siasa kwa mambo muhimu ya kitaifa na siasa mkafanyie majukwaani na sio humo bungeni.
Binafsi huwa nashangaa kusikia spika anaanza kwa maombi( maarufu kama dua ya kuliombea bunge) alafu kinachofuata ni dhambi kwa watanzania, tena kwa kila kikao bila kujirekebisha.
Katika mambo ambayo nilitarajia wangesimama kidete ni kuhakikisha mishahara ya watumishi inapunguziwa kodi kwani mishahara ni midogo sana na bado inatozwa kodi kubwa.Wao wenyewe wanaona posho ya sh 150,000 kwa siku haitoshi sasa mbona hawajiuliza huyu mtumishi ataishi vipi kwa mshahara wa sh 170,000 kwa mwezi.
Jambo lingine miongoni mwa mengi ya kuudhi ni kuona wameruhusu kampuni ya Kiwira itengewe sh bilioni 40 licha ya hasara kubwa iliyosababishwa na mwekezaji wa mgodi huu.Kwanini hawakupinga jambo hili la kifisadi!Hivi hizo pesa zingeelekezwa kwa madaktari si zingeepusha mgomo.Hata kama si kwa madaktari zingeweza kusaidia ktk maeneo mengine.
Hiyo ni mifano michache tu ya mapungufu ambayo ni ya wazi kabisa lakini watu hawa wameziba masikio na kutia pamba masikionoi wakiwaacha watanzania wanaangamia ktk dimbwi la umasikini.Na kinachouma ni kuona namna ambavyo wanashangilia na kupiga meza kanakwamba wamepata uungwaji mkono kutoka kwa wanaowawakilisha.Sijui labda huwa wanapigiwa simu za pongezi baada ya kupitisha.
Mh.Tundu Lisu aliposema this is another silly season hakukosea kabisa na mimi naunga mkono kauli yake kwa asilimia mia moja kama wao wanavyounga mkono kwa asilimia mia moja hizo bajeti tata.
Acheni siasa kwa mambo muhimu ya kitaifa na siasa mkafanyie majukwaani na sio humo bungeni.
Binafsi huwa nashangaa kusikia spika anaanza kwa maombi( maarufu kama dua ya kuliombea bunge) alafu kinachofuata ni dhambi kwa watanzania, tena kwa kila kikao bila kujirekebisha.