Elections 2010 Hili la viongozi wastaafu linakuaje?

Kazawadi

Member
Aug 27, 2010
11
0
Kwa maoni yangu nafikiri ni vyema viongozi wetu wakuu km raisi na waziri mkuu, wakistaafu wapewe stahili zao ambazo ni sawa kama watumishi wengine wa umma. Taifa lisienndelee kubeba mizigo ya kuwahudumia. Viongozi wetu wastaafu tunawapenda na tungependa waishi maisha marefu baada ya kustaafu uongozi wa kitaifa. Lakini si jambo jema kwa taifa kuendelea kubeba mzigo mkubwa wa kuwahudumia ilhali wameishastaafu kwenye ajira ambayo walilipwa mishahara mikubwa na marupurupu tele.

Akiongea na gazeti la mwananchi juzi, Professa Tigiti Sengo, amesema kwa sasa kuna wastaafu zaidi ya 12 na tz inapoteza mabilioni kila mwaka kuwahudumia hao. Ametoa mfano wa marekani na uingereza ambapo wastaafu hurejea ktk shughuli zao za kiuchumi kujiendeleza.

Hivi hapa tz haya hayawezekani? inakadiriwa tuna wastaafu wa jinsi hiyo zaidi ya 12, na kama nilivyosema hapo awali tunawatakia maisha marefu, je tukiwa nao 50 ama 100 taifa litawezaje mzigo huu?
 
Africa siasa ni ajira. Kwa wenzetu siasa ni wito au huduma kwa jamii. Usipowatunza watafanya shughuli gani? Chukulia JK na EL. Toka walipotoka shuleni wakaanza ukada wa CCM. Hawajawahi kufanya kazi yoyote productive nje ya CCM. Sasa wakistaafu usipowatunza watafanya nini? Labda ni kwa sababu ya hiyo background ndipo tunaweza kuelewa ufisadi wao.
 
Africa siasa ni ajira. Kwa wenzetu siasa ni wito au huduma kwa jamii. Usipowatunza watafanya shughuli gani? Chukulia JK na EL. Toka walipotoka shuleni wakaanza ukada wa CCM. Hawajawahi kufanya kazi yoyote productive nje ya CCM. Sasa wakistaafu usipowatunza watafanya nini? Labda ni kwa sababu ya hiyo background ndipo tunaweza kuelewa ufisadi wao.

Duh, hapo umegonga penyewe!

Hivi JK akipewa hata u-afisa uchumi wa wilaya ataweza kweli, mimi namuona kama mweupe vile ndiyo maana anafanya kila hila aendelee kukaa madarakani na kwa kufanya hivyo kuwalinda wenzake, wanaogopa yakitokea mabadiriko tunayoyataka haya marupurupu kwa wastaafu yasiyolingana na uwezo wa taifa yanaweza kufutwa, na ikitokea hilo wengine tunaweza kuanza kukutana nao mitaani wakiomba kwa sababu hiyo ndiyo hulka yao.
 
Back
Top Bottom