Hili la URANIUN SONGEA limekaaje??

Confirmed: Hawa jamaa ni MATAPELI. Nimeongea na watu wa mgodini jana tu, hamna kitu kama hiyo>.
 
Kulikuwa na Bandiko hapa la kazi mgodini Songea,sasa kwa baadhi ya watu walioomba wameambiwa shortlist inaandaliwa na vigezo vya kuingia kwenye shortlist inahitajika utume Tsh Laki 6 (600,000), lakini kwa kuanzia inabidi uwatumie laki 2(200,000) halafu ukishaenda kwa inteview then inabidi uwalipe inayobaki ie laki 4(400,000).

JE kama kuna mwenye details zaidi atujuze hii kitu ipo sawa au wanaweza kuingia mkenge hawa watakaoanza kutuma hizo laki 2? Na hizi nafasi ( nyingi za Operators) zilitoka kwenye gazeti au ni kwenye internet pekee?? Manake mambo ya mtandao hapa usije ukaingia UPOPO.
Nawakilisha.
Mkuu wakati mwingine unaweza kuamua kujilipua tu katika inshu kama hizo,kuwa risk taker ili ujifunze kutokana na makosa yako,kumbuka woga wako ndio umaskini wako pia.....toa hela upate fedha,hiyo kitu mbona ipo sana hao wanaokuambia eti kitu kama hicho hakuna katika sokola ajira ni kwamba wamekalili na hayajawakuta.....but play with steps and be carefully.
 
Duuh uwizi mtupu! Nimesoma hii nyuzi ya mleta mada mpaka nahisi kichwa kinauma.
Jukwaa la kazi na tenda limevamiwa vijana tuwe macho!.
 
Sasa humu imeshakuwa habari zinatumwa zinakuwa ni za uongo, wewe unayeombwa laki sita unataka kutapeliwa,ulishaona wapi ajira za hivyo?mimi huwa naona mtu anaetaka wafanyakazi huwa anagharamikia kila kitu,je iweje leo anaetafuta kazi aombwe pesa?vile vile hilo Tangazo lilikuwa ni la uongo mtupu hakuna ajira Songea,tusidanganyane,Tuwe makini sana wana jamii forum wakati wa ku post matangazo mbali mbali humu ndani.
 
Back
Top Bottom