Siku kadhaa zilizopita, waziri wa Utamaduni, Habari na Michezo alikuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha miaka 50 ya uhuru ambazo wizara yake iliamua kuziandaa kijijini Butiama. Katika sherehe hizo jambao moja lilikuwa dhahiri. Kwamba si mjane wa Hayati Baba wa Taifa, wala familia yake na hata ukoo wa Mwalimu waliokuwepo kwenye sherehe hizo.
Ukizingatia kwamba madhumuni ya sherehe hizo kufanyikia Butiama ni kuenzi na kutambua mchango wa Malimu katika ukombozi wa nchi hii na yale yote mazuri tunayojivunia leo, suala la kukosekana kwa watu hao, ambao siyo kwamba ndiyo wenyeji wake, bali pia ni walengwa muhimu, kunaleta maswali mengi sana ambayo pengine yanaia dosari kubwa katika utendaji wa wizara hiyo na hasa Nchimbi binafsi.
Taarifa tulizonazo ni kwamba Mama Maria alikuwa safarini Uingereza, wakati wanafamilia wengine walikuwa Dar na Musoma lakini kwa vile hawakuhusishwa walikaa kando. Kinachoshangaza ni kwamba Nchimbi huyo huyo analalamika kwamba familia hiyo ilimsusia sherehe hiyo na kusema kwamba kitendo cha wao kutokuwepo kwenye hafla hiyo na kuhudhuria kwa wingi kwenye sherehe ya wizara ya mambo ya nje siku chache baadae kinatafsiriwa katika jicho la kisiasa na uchaguzi wa 2015.
Mimi naona kwamba Nchimbi aitake radhi familia hii na watanzania kwa kuwadhalilisha!
Ukizingatia kwamba madhumuni ya sherehe hizo kufanyikia Butiama ni kuenzi na kutambua mchango wa Malimu katika ukombozi wa nchi hii na yale yote mazuri tunayojivunia leo, suala la kukosekana kwa watu hao, ambao siyo kwamba ndiyo wenyeji wake, bali pia ni walengwa muhimu, kunaleta maswali mengi sana ambayo pengine yanaia dosari kubwa katika utendaji wa wizara hiyo na hasa Nchimbi binafsi.
Taarifa tulizonazo ni kwamba Mama Maria alikuwa safarini Uingereza, wakati wanafamilia wengine walikuwa Dar na Musoma lakini kwa vile hawakuhusishwa walikaa kando. Kinachoshangaza ni kwamba Nchimbi huyo huyo analalamika kwamba familia hiyo ilimsusia sherehe hiyo na kusema kwamba kitendo cha wao kutokuwepo kwenye hafla hiyo na kuhudhuria kwa wingi kwenye sherehe ya wizara ya mambo ya nje siku chache baadae kinatafsiriwa katika jicho la kisiasa na uchaguzi wa 2015.
Mimi naona kwamba Nchimbi aitake radhi familia hii na watanzania kwa kuwadhalilisha!