Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Na. M. M. Mwanakijiji
Mwl. Julius K. Nyerere alikoswakoswa kwenda jela mwaka 1958 baada ya kushtakiwa na serikali ya mkoloni kuwa alitoa kauli za kashfa kwa watendaji mbalimbali wa serikali. Alikutwa na hatia na alitakiwa kufungwa jela au kulipa faini. Kwa vile walikuwa wanaelekea kwenye uchaguzi wa kwanza ambapo TANU ilikuwa inaelekea kushinda mjadala mkubwa ulikuwa ni je alipe faini au akubali kwenda jela? Yeye mwenyewe alikuwa anataka kwenda jela kama walivyokuwa wanaenda viongozi wengine wa Afrika. Lakini waasisi wenzake walimtaka akubali kulipa faini ili TANU isipoteze nafasi yake kwenye uchaguzi ule. Nyerere mwenyewe alisema kwenda jela kungekuwa ni kama kuhitimu katika siasa za harakati za uhuru.
Mhe Godbless Lema (MB) - Arusha Mjini
Jana huko Arusha Mbunge wa Arusha Mjini Bw. Godbless Lema alikubali kufanya kinyume chake. Alikuwa na uchaguzi wa kupewa dhamana katika kesi inayomhusu na kwenda zake nje na kufurahia uhuru au kwenda jela. Katika kitu ambacho alikipanga mapema Lema aliamua kwenda jela na kukataa kuwekewa dhamana. Uamuzi huu kwa baadhi ya watu unaweza kuonekana ni wa kujitafutia sifa na umaarufu wa kisiasa. Hilo siwezi kulipinga kwani Lema ni mwanasiasa na wanasiasa huhitaji umaarufu mara zote na si kosa.
Lakini zaidi kilichonigusa mimi ni sababu alizotoa na kwanini alifikia uamuzi huo. Ninaziangalia sababu hizi kwa mwanga mpya wa kisiasa ambapo Lema amejaribu kutuma ujumbe usio na utata kuwa wanasiasa wa Tanzania hawapaswi tena kuishi kwa hofu ya kufikishwa mahakamani au kupewa vifungo kwa sababu ya harakati zao. Alichokifanya ni kutaka kutuma ujumbe kuwa watawala wetu hawawezi kutumia mahakama na polisi kama rungu la kuwatisha wanasiasa.
Lema alisema katika taarifa iliyotangulia uamuzi wake huo kuwa Kila mara nilipotishiwa nikagundua wanaonitishia, wananitishia kwa jela na mauti. Na mimi nikagundua na nikatambua ni afadhali kuishi miaka hamsini jela huku sababu ikiwa ni kupinga uonevu na ukandamizaji kuliko maisha ya woga na anasa yasiyo na kusudi katika kutetea utu na heshima ya mwanadamu mwenzangu. Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari
Aliendelea na kusema kuwa nitaenda jela kwa hiari yangu binafsi wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu. Kosa kubwa ambalo lilifanywa na watu wa mahakamani labda ni kukubali kutomwachilia kwa utambulisho wake mwenyewe (self-recognizance) na hivyo kumpa nafasi. Hivi kweli Mbunge wa Jamhuri ya Muungano anaweza kufungwa kwa kosa dhamana?
MALIZIA MAKALA HII YA KUFIKIRISHA
KUTOKA MAKANGE BLOG
Mwl. Julius K. Nyerere alikoswakoswa kwenda jela mwaka 1958 baada ya kushtakiwa na serikali ya mkoloni kuwa alitoa kauli za kashfa kwa watendaji mbalimbali wa serikali. Alikutwa na hatia na alitakiwa kufungwa jela au kulipa faini. Kwa vile walikuwa wanaelekea kwenye uchaguzi wa kwanza ambapo TANU ilikuwa inaelekea kushinda mjadala mkubwa ulikuwa ni je alipe faini au akubali kwenda jela? Yeye mwenyewe alikuwa anataka kwenda jela kama walivyokuwa wanaenda viongozi wengine wa Afrika. Lakini waasisi wenzake walimtaka akubali kulipa faini ili TANU isipoteze nafasi yake kwenye uchaguzi ule. Nyerere mwenyewe alisema kwenda jela kungekuwa ni kama kuhitimu katika siasa za harakati za uhuru.
Mhe Godbless Lema (MB) - Arusha Mjini
Jana huko Arusha Mbunge wa Arusha Mjini Bw. Godbless Lema alikubali kufanya kinyume chake. Alikuwa na uchaguzi wa kupewa dhamana katika kesi inayomhusu na kwenda zake nje na kufurahia uhuru au kwenda jela. Katika kitu ambacho alikipanga mapema Lema aliamua kwenda jela na kukataa kuwekewa dhamana. Uamuzi huu kwa baadhi ya watu unaweza kuonekana ni wa kujitafutia sifa na umaarufu wa kisiasa. Hilo siwezi kulipinga kwani Lema ni mwanasiasa na wanasiasa huhitaji umaarufu mara zote na si kosa.
Lakini zaidi kilichonigusa mimi ni sababu alizotoa na kwanini alifikia uamuzi huo. Ninaziangalia sababu hizi kwa mwanga mpya wa kisiasa ambapo Lema amejaribu kutuma ujumbe usio na utata kuwa wanasiasa wa Tanzania hawapaswi tena kuishi kwa hofu ya kufikishwa mahakamani au kupewa vifungo kwa sababu ya harakati zao. Alichokifanya ni kutaka kutuma ujumbe kuwa watawala wetu hawawezi kutumia mahakama na polisi kama rungu la kuwatisha wanasiasa.
Lema alisema katika taarifa iliyotangulia uamuzi wake huo kuwa Kila mara nilipotishiwa nikagundua wanaonitishia, wananitishia kwa jela na mauti. Na mimi nikagundua na nikatambua ni afadhali kuishi miaka hamsini jela huku sababu ikiwa ni kupinga uonevu na ukandamizaji kuliko maisha ya woga na anasa yasiyo na kusudi katika kutetea utu na heshima ya mwanadamu mwenzangu. Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari
Aliendelea na kusema kuwa nitaenda jela kwa hiari yangu binafsi wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu. Kosa kubwa ambalo lilifanywa na watu wa mahakamani labda ni kukubali kutomwachilia kwa utambulisho wake mwenyewe (self-recognizance) na hivyo kumpa nafasi. Hivi kweli Mbunge wa Jamhuri ya Muungano anaweza kufungwa kwa kosa dhamana?
MALIZIA MAKALA HII YA KUFIKIRISHA
KUTOKA MAKANGE BLOG