Hili basi ni balaa jamani

Simba Mkali

JF-Expert Member
Jan 31, 2012
620
239
Kuna basi moja linafanya kazi ya kusafirisha abiria kati ya Dar es Salaam hadi Mwanza, linaitwa Muro kila siku linalaza abiria njiani, yaani bovu ile kinoma. Mbaya zaidi linapoharibika hakuna msaada wowote unaotolewa na wahusika, hapo ndipo inapokuwa mwisho wa mchezo, aidha abiria watafute usafiri mwingine au walale kwenye basi (kama ni usiku) hilo hadi kesho yake. Jamani haya si mateso jamani. Kwani linaruhusiwa kutembea au ni la mkubwa. Nani anayejua habari zake atuhabarishe?
 
Kwenye red kama ni kweli basi hatari sana.

Kuna basi moja linafanya kazi ya kusafirisha abiria kati ya Dar es Salaam hadi Mwanza, linaitwa Muro kila siku linalaza abiria njiani, yaani bovu ile kinoma. Mbaya zaidi linapoharibika hakuna msaada wowote unaotolewa na wahusika, hapo ndipo inapokuwa mwisho wa mchezo, aidha abiria watafute usafiri mwingine au walale kwenye basi (kama ni usiku) hilo hadi kesho yake. Jamani haya si mateso jamani. Kwani linaruhusiwa kutembea au ni la mkubwa. Nani anayejua habari zake atuhabarishe?
 
Kuna basi moja linafanya kazi ya kusafirisha abiria kati ya Dar es Salaam hadi Mwanza, linaitwa Muro kila siku linalaza abiria njiani, yaani bovu ile kinoma. Mbaya zaidi linapoharibika hakuna msaada wowote unaotolewa na wahusika, hapo ndipo inapokuwa mwisho wa mchezo, aidha abiria watafute usafiri mwingine au walale kwenye basi (kama ni usiku) hilo hadi kesho yake. Jamani haya si mateso jamani. Kwani linaruhusiwa kutembea au ni la mkubwa. Nani anayejua habari zake atuhabarishe?

Kwani Mwanza kuna bus hilo hilo moja? Badilisha usafiri mkuu
 
Kwani hamna mabsi mengine???? Unalalamika utadhani ndege ya kwenda Kigoma ambayo iko moja tu ATC
 
Kwani hamna mabsi mengine???? Unalalamika utadhani ndege ya kwenda Kigoma ambayo iko moja tu ATC
Mimi sipandi tena, ila tatizo ni ndugu zetu wengine wa Kitanzania bado wapanda likija kuleta madhara si tutalia wote kama tulivyolia kwenye MV Spice, kwanini tusichukue tahadhari mapema?
 
Duh umenikumbusha ndio ilikua mara yangu ya kwanza kwenda Kigoma, ndio nikaambiwa linaenda huko, balaa yaani kahama saa tano usiku ndio tunafika na kum,be linaishia hapo
 
Watu wengine mna majibu ya kukera sana, kutoa taarifa imeshakuwasoo..! Ametoa taarifa ili yeyote atakayesafiri kuelekea huko asilipande litamletea usumbufu. Kama yeye akibadili gari akawa anapanda aina nyingine ya bus bila kutoa taarifa sisi tutajuje? Si tutaingia mkenge kama yeye? . Mkuu big up 4 your information.
 
Jamani sio utani huyo jamaa kawatahadharisha tu,ilisha,ilishanitokea mimi nilikuwa nakwenda KAHAMA liliharibika si chini ya mara nne na tulilala Manyoni,Chalinze walikaza tairi,Kibaigwa ilifungukaka shafti,Bahi ikatoboka rejeta na tukawa tunaenda kama kobe na madumu ya maji ili isichemshe,wakalazimisha tupite usiku saa 9 manyoni watu wakakataa tukasubiri asubuhi wakalitengeneza,Tulifika KAHAMA saa 11 jioni.
Pale ubungo wanafanya uhuni wanakukatia Alliys ukifika muda wa kuondoka wanakwambia alliys mbovu ndo wanaleta mifupa yao, nilisafiri kwakuwa nililazimika kuondoka siku hiyo na mabasi mengine yalishatoka na kurudisha nauli ingelichukua muda sana.
KWELI MURO SIO BASI HATA KIDOGO.
 
mwanza magari ya uhakika ni haya 1. allys 2.green star 3. darlux 4. princess shabaha 5 akamba...... na ukitaka ufike dar mapema au mwanza mapema by saa2 panda Allys ila nauli 45000 ...yaliyobaki ndugu kama vile mohamed,mombasa, zuber,muro na mengineyo kama unataka kutekwa au kuliwa kiboga maeneo ya usagara wkt unatoka dar panda ila uandae kyjel kabisa kama ww mwanaume
 
Kuna basi moja linafanya kazi ya kusafirisha abiria kati ya Dar es Salaam hadi Mwanza, linaitwa Muro kila siku linalaza abiria njiani, yaani bovu ile kinoma. Mbaya zaidi linapoharibika hakuna msaada wowote unaotolewa na wahusika, hapo ndipo inapokuwa mwisho wa mchezo, aidha abiria watafute usafiri mwingine au walale kwenye basi (kama ni usiku) hilo hadi kesho yake. Jamani haya si mateso jamani. Kwani linaruhusiwa kutembea au ni la mkubwa. Nani anayejua habari zake atuhabarishe?

Aksante tutaliepuka... hata ukiliangalia kwa nje limekaa kishari shari vile...
 
best line, master line ni bora ulale stendi kuliko kupanda haya mabasi, kulala njiani ni nje nje halafu machafu mpaka kunguni ndani. mabasi mazuri mwanza-dar ni green star 2. lucky star, 3. allly's (yanakwenda kasi sana ni hatari) nikikosa haya huwa na ahirisha safari
 
Asante kwa taarifa mkuu,Nilienjoy kusafiri na Allys kwenda mwanza nakurudi na ilikua mara yangu ya kwanza kiukweli huwa sisahau ile safari!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom