makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Baada ya mgombea Ubunge jimbo la Maswa Magharibi Mhe. Shibuda kuachiwa na polisi kuwa hahusiki na mauaji,Kamati ya maadili ya Uchaguzi ya Wilaya hiyo imemjia juu Shibuda kwa kutaka aenguliwe na NEC baada ya kuandika barua kwenda NEC.
Kitu kinachoshangaza ni hii Kamati ya Maadili inaposhondwa kutumia busara. Kuwa Shibuda hahusiki na mauaji hayo na Polisi wamethibitisha hivo na ndiyo maana wakamwachia huru aendelee na Kampeni.
Ni dhahiri kwamba Kamati hii iko kwa ajili ya maslahi ya CCM. Hilo liko wazi kabisa. Haiwezekani wafuasi au mashabiki wa vyama husika vya siasa wafanye vurugu na kuuana halafu useme mgombea wa chama mojawapo anahusika na aenguliwe. Hivi je,kama tukio hili lingekuwa kinyume chake Kamati hii ingelikuwa tayari kusema Wagombea wote wa CCM waenguliwe???
Naamini NEC si wapuuzi kiasi hicho cha kukubaliana na maoni ya Kamati hii ya Maswa ambayo inataka kuibeba CCM kwa mbeleko kuipeleka Bungeni. Haikubaliki asilani.
CCM wanaonyesha kuwa na hasira na uchungu na Shibuda kwa kuihama CCM bbada ya kumfanyia mizengwe kwenye kura za maoni ilhali bado anakubalika na wananchi.
Hata kuwekwa ndani kwa Shibuda ililkuwa ni shinikizo la Vigogo wa CCM akiwemo Makamba,Kinana na JK. Hapa CCM wanaonekana na kuwa na siasa za chuki.
Mimi nawakumbusha CCM tu kuwa wasifikiri tumesahau kile kilichotokea Zanzibar uchaguzi wa 2000 walipoua wananchi zaidi ya 25 kwa upuuzi wa maelekezo ya CCM. Mbona CCM hawakuenguliwa baada ya Polisi kuua idadi hiyo ya watu kwa maelekezo ya vigogo wa CCM? Chondechonde CCM na NEC msitake kurejesha mambo ya mwaka 2000 huko Unguja.
Kitu kinachoshangaza ni hii Kamati ya Maadili inaposhondwa kutumia busara. Kuwa Shibuda hahusiki na mauaji hayo na Polisi wamethibitisha hivo na ndiyo maana wakamwachia huru aendelee na Kampeni.
Ni dhahiri kwamba Kamati hii iko kwa ajili ya maslahi ya CCM. Hilo liko wazi kabisa. Haiwezekani wafuasi au mashabiki wa vyama husika vya siasa wafanye vurugu na kuuana halafu useme mgombea wa chama mojawapo anahusika na aenguliwe. Hivi je,kama tukio hili lingekuwa kinyume chake Kamati hii ingelikuwa tayari kusema Wagombea wote wa CCM waenguliwe???
Naamini NEC si wapuuzi kiasi hicho cha kukubaliana na maoni ya Kamati hii ya Maswa ambayo inataka kuibeba CCM kwa mbeleko kuipeleka Bungeni. Haikubaliki asilani.
CCM wanaonyesha kuwa na hasira na uchungu na Shibuda kwa kuihama CCM bbada ya kumfanyia mizengwe kwenye kura za maoni ilhali bado anakubalika na wananchi.
Hata kuwekwa ndani kwa Shibuda ililkuwa ni shinikizo la Vigogo wa CCM akiwemo Makamba,Kinana na JK. Hapa CCM wanaonekana na kuwa na siasa za chuki.
Mimi nawakumbusha CCM tu kuwa wasifikiri tumesahau kile kilichotokea Zanzibar uchaguzi wa 2000 walipoua wananchi zaidi ya 25 kwa upuuzi wa maelekezo ya CCM. Mbona CCM hawakuenguliwa baada ya Polisi kuua idadi hiyo ya watu kwa maelekezo ya vigogo wa CCM? Chondechonde CCM na NEC msitake kurejesha mambo ya mwaka 2000 huko Unguja.