MKAZI wa kijiji cha Monuna kilichopo kata ya Nyambureti Wilayani Serengeti, James Juma [22] amekufa baada ya kumwagiwa mafuta ya taa na kuchomwa moto na wakazi wakijiji cha Maburi kwa lengo la kumwokoa baada ya kuvamiwa na kundi la nyuki.
Katika hali isiyotarajiwa watu waliofika kumsaidia walizidiwa na kundi hilo la nyuki na kutoa wazo la kummwagia mafuta ya taa, lakini nyuki walizidi kumshambulia, ndipo kukazuka wazo la kuwasha moto bila kujua kuwa tayari walikuwa wamemmwagia mafuta ya taa na moto ukashika nguo zake na kumuunguza vibaya sana.
Source: NIFAHAMISHE Tanzania news portal
Katika hali isiyotarajiwa watu waliofika kumsaidia walizidiwa na kundi hilo la nyuki na kutoa wazo la kummwagia mafuta ya taa, lakini nyuki walizidi kumshambulia, ndipo kukazuka wazo la kuwasha moto bila kujua kuwa tayari walikuwa wamemmwagia mafuta ya taa na moto ukashika nguo zake na kumuunguza vibaya sana.
Source: NIFAHAMISHE Tanzania news portal