Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Msiniite mbea na sipigi chuku wala sifanyi fitna………………….
Week end hii, nilimtembelea mzee mmoja ambaye nilitambulishwa na rafiki yangu anayeishi mkoani. Nakumbuka nilipokuwa huko mkoani nilibahatika kufahamiana na jamaa mmoja na katika mazungumzo yetu alinijuza kwamba anaye mjomba wake huku Dar na akanipa mzigo fulani niufikishe kwa huyo mjomba wake.
Baada ya kuwa bize kwa majuma kadhaa, week end hii nikawasiliana na huyo mjomba wa jamaa yangu na baada ya kunielekeza kwake nikafunga safari hadi pale kwake. Nilikaribishwa vizuri sana na kwa kuwa ilikuwa ni weekend siku ya mapumziko, nilibahatika kuikuta familia yake, wote wakiwa hapo nyumbani. Baada ya kunitambulisha kwa mkewe, aliwaita wanae ili anitambulishe kwao.
Walikuja wavulana wanne na wasichana wawili mdogo kabisa wa kike alionekana kuwa na umri wa 14 hivi na mkubwa kabisa wa kiume nadhani alifikia miaka 30 hivi. Alinijulisha kuwa wale wote ni wanae na huyo mkubwa ameshaoa na anajitegemea na wavulana wengine wawili hawajaoa lakini wanajitegemea pia. Pale nyumbani walikuwa wamebaki wale wasichana wawili na mvulana mmoja.
Huyu mvulana ndiye ninayetaka kumzungumzia. Kati ya wale watoto wa yule mzee huyu alikuwa tofauti kabisa na wenzake........yeye alikuwa ni mweupe na nywele zake kama za shombe kama za kiarabu ingawa wazazi wake wote yaani mjomba na mkewe ni weusi tii kama mimi Mtambuzi.......Awali nilidhani ni mtoto wa ndugu yake lakini alimtaja kama mtoto wake wa nne kuzaliwa kati ya watoto wake 6 aliowazaa na mkewe.
Anyway sikutaka kufanya udadisi. Lakini jana wakati nazungumza na huyu jamaa yangu wa mkoani kwenye simu kumjuza kwamba nimefikisha ule mzigo alionipa kwa mjomba wake.......kama vile alisoma mawazo yangu, aliniuliza kama nilimuona yule mtoto wa mjomba wake mwenye asili ya kiarabu.......nikamjibu ndio, na ndipo akaniambia kuwa yule mtoto alileta ugomvi mkubwa katika ndoa ya mjomba wake na almanusura ndoa yao ivunjike, ni busara za wazee tu waliinusuru ndoa ile kwa kigezo kwamba kitanda hakizai haramu..............
Mungu aniepushe na balaa hilo kwa Mama Ngina............
Week end hii, nilimtembelea mzee mmoja ambaye nilitambulishwa na rafiki yangu anayeishi mkoani. Nakumbuka nilipokuwa huko mkoani nilibahatika kufahamiana na jamaa mmoja na katika mazungumzo yetu alinijuza kwamba anaye mjomba wake huku Dar na akanipa mzigo fulani niufikishe kwa huyo mjomba wake.
Baada ya kuwa bize kwa majuma kadhaa, week end hii nikawasiliana na huyo mjomba wa jamaa yangu na baada ya kunielekeza kwake nikafunga safari hadi pale kwake. Nilikaribishwa vizuri sana na kwa kuwa ilikuwa ni weekend siku ya mapumziko, nilibahatika kuikuta familia yake, wote wakiwa hapo nyumbani. Baada ya kunitambulisha kwa mkewe, aliwaita wanae ili anitambulishe kwao.
Walikuja wavulana wanne na wasichana wawili mdogo kabisa wa kike alionekana kuwa na umri wa 14 hivi na mkubwa kabisa wa kiume nadhani alifikia miaka 30 hivi. Alinijulisha kuwa wale wote ni wanae na huyo mkubwa ameshaoa na anajitegemea na wavulana wengine wawili hawajaoa lakini wanajitegemea pia. Pale nyumbani walikuwa wamebaki wale wasichana wawili na mvulana mmoja.
Huyu mvulana ndiye ninayetaka kumzungumzia. Kati ya wale watoto wa yule mzee huyu alikuwa tofauti kabisa na wenzake........yeye alikuwa ni mweupe na nywele zake kama za shombe kama za kiarabu ingawa wazazi wake wote yaani mjomba na mkewe ni weusi tii kama mimi Mtambuzi.......Awali nilidhani ni mtoto wa ndugu yake lakini alimtaja kama mtoto wake wa nne kuzaliwa kati ya watoto wake 6 aliowazaa na mkewe.
Anyway sikutaka kufanya udadisi. Lakini jana wakati nazungumza na huyu jamaa yangu wa mkoani kwenye simu kumjuza kwamba nimefikisha ule mzigo alionipa kwa mjomba wake.......kama vile alisoma mawazo yangu, aliniuliza kama nilimuona yule mtoto wa mjomba wake mwenye asili ya kiarabu.......nikamjibu ndio, na ndipo akaniambia kuwa yule mtoto alileta ugomvi mkubwa katika ndoa ya mjomba wake na almanusura ndoa yao ivunjike, ni busara za wazee tu waliinusuru ndoa ile kwa kigezo kwamba kitanda hakizai haramu..............
Mungu aniepushe na balaa hilo kwa Mama Ngina............