Tatizo cdm mnatetea hata visivyotetewa kisa ni mtu wa cdm, inawezekana kabisa hata huyo Lema ni jambazi mi naamini na kama sio basi aende mahakamani kudai fidia hata ya shilingi moja kwa kuchafuliwa na Zombe! khaa! na kama ni majambazi wao sio cdm! kwani CCM wote ni mafisadi? mi sipendi kutetea ujinga kisa eti ni mtu wa cdm! inamaana kama ni majambazi na wanaendeleza wizi basi waachwe tu kisa cdm? inaudhi sana!
Hapo nakuunga mkono nami nashangaa sana wana CDM kutetea mtu msiyemjua jifunzeni wa CCM maana wao wamekubali kuwa wana mafisadi na lazima wajivue gamba lakini nyinyi mnatetea mtuhumiwa wa Ujambazi je ikija kuthibitishwa kama ni jambazi mtawaambia nini wananchi.
Tuache kutetea uovu kila mtu abebe zigo lake mwenyewe kama kweli Lema ni jambazi au katibu wake jambazi tuwaache wabebe mizigo yao wenyewe maana ni ya kwao sio ya CDM
Na CCM vile vile isiwatete mafisadi tuwaache wabebe mizigo yao. Siasa inayotakiwa ni chama gani chenye muongozo wa kuwaokoa wananchi na shida walizo nazo na kuwaletea maendeleo mimi nadhani hii ndio siasa safi
Vyama vya siasa ndivyo vinavyoipeleka Tanzania shimoni leo CCM wanaitwa mafisadi kesho CDM wataitwa majambazi hili halitoisaidia nchi jamani