Hii siyo Fair Dada zangu tutakuja kuuana.

Ukweli ni jambo muhimu ambalo litanusuru mambo mengi, kwa siku kadhaa nimekuwa nikimfuatilia dada fulani ambaye kanihakikishia kuwa yuko free, si hivyo tu pia kanihakikishia kuwa yuko tayari kuwa na mimi. Nimejipanga kadri ya uwezo wangu kupeleka barua ndo ananiambia kuwa samahani nimechumbiwa. Baada ya kuchunguza nimegundua ni kweli kachumbiwa na jamaa mmoja ambaye anaishi Dubai toka mwaka jana mwezi wa nne. Huu sio ustaarabu bora kuwa wawazi, ndani ya miezi minne niko na matumaini kumbe najivunia garasa. SI TABIA NZURI kuweni wazi, ona sasa wiki nzima sina raha nashindwa hata kufanya kazi zangu kwa ufanisi.

Mpindue huyo wa Dubai. Ukipenda unapigania unachokipenda. Like they say, You've got to fight the fight kid.
 
i see...

Kuna wanaume mnajua kujilipua i see.....
Miezi minne unapeleka barua?

Ndo maana ndoa siku hizi hazidumu....
 
Ukweli ni jambo muhimu ambalo litanusuru mambo mengi, kwa siku kadhaa nimekuwa nikimfuatilia dada fulani ambaye kanihakikishia kuwa yuko free, si hivyo tu pia kanihakikishia kuwa yuko tayari kuwa na mimi. Nimejipanga kadri ya uwezo wangu kupeleka barua ndo ananiambia kuwa samahani nimechumbiwa. Baada ya kuchunguza nimegundua ni kweli kachumbiwa na jamaa mmoja ambaye anaishi Dubai toka mwaka jana mwezi wa nne. Huu sio ustaarabu bora kuwa wawazi, ndani ya miezi minne niko na matumaini kumbe najivunia garasa. SI TABIA NZURI kuweni wazi, ona sasa wiki nzima sina raha nashindwa hata kufanya kazi zangu kwa ufanisi.


Hata nyie wanakaka mnafanya hivyo, si wadada tu. Tena bora huyu alikuwa na mchumba, nyie mmeshaoa kabisa na watoto mmezaa halafu mwajifanya mko single na kupeleka posa kabisa, halafu eti ukiliuliza uko peke yako kweli? linakujibu Am maximum single baby. Nyie pia hamfai loh!!!!!!!!
 
Iwe kweli au uongo HAIJALISHI. Kinachojalisha ni kua mazingira na matendo yamekuhukumu ndio maana hata mwenzio kajitenga na wewe.

She was wrong and she will come back to me and prove that
 
Ulishafanikiwa kumuingilia? Kama ni ndiyo basi huyo ni fuska na sio wife material!
BORA HICHO KIKOMBE KIMEKUEPUKA!
 
Preta, unamaanisha kuwa miezi minne ni michache. Kwa upeo wangu
kama umeshindwa kufanya Investigation ndani ya miezi 4 hata miaka
miwili huwezi pia.

Exactly, na short investigation is point only 2 your target and givs u intelligent decision

I enjoy always wid short tym inspection and I shot with confidense

-urafiki/uchumba wa mda mlefu ni kupeana nafasi kusomana udhaifu wa patna wako na vp utamuAttack mwenzako -kwikwikwi
 
Preta, unamaanisha kuwa miezi minne ni michache. Kwa upeo wangu
kama umeshindwa kufanya Investigation ndani ya miezi 4 hata miaka
miwili huwezi pia.

Kuchunguza sio tu kupeleleza au kuuliza watu kuhusu huyo mtu unayetaka kufunga ndoa naye. Kunahusisha kumchunguza yeye binafsi na kujua ni kiasi gani yuko tayari kwa pingu za maisha. Hii inahitaji muda mrefu zaidi kuliko muda unaohitajika kuwaulizia wengine.
 
Swala la muda gani wa kumchunguza mwenzio limekuwa gumu kueleweka, Preta naomba kama bado uko jukwaani uje na ufafanuzi wa muda gani unatosha kumchunguza mwenzio. Ninavyofahamu watu wanaokaa muda mrefu si kwamba wanachunguzana wameamua kuishi tu! Muda wa kumchunguza mtu ni mfupi tu! Wapo walioishi miaka mitano hadi kumi bila ndoa, lakini miaka miwili baada ya ndoa wakaachana Please PRETA nahitaji Clarification zaidi! Maana umekuwa mshabiki mkubwa wa kutaka muda wa kuchunguzana uwe mrefu.
 
Swala la muda gani wa kumchunguza mwenzio limekuwa gumu kueleweka, Preta naomba kama bado uko jukwaani uje na ufafanuzi wa muda gani unatosha kumchunguza mwenzio. Ninavyofahamu watu wanaokaa muda mrefu si kwamba wanachunguzana wameamua kuishi tu! Muda wa kumchunguza mtu ni mfupi tu! Wapo walioishi miaka mitano hadi kumi bila ndoa, lakini miaka miwili baada ya ndoa wakaachana Please PRETA nahitaji Clarification zaidi! Maana umekuwa mshabiki mkubwa wa kutaka muda wa kuchunguzana uwe mrefu.

kwa mfano mdogo tu, hakiki ya vipimo vya ukimwi huwa vinachukua muda gani vile?
 
ndio utie akili......
ndani ya miezi minne unatangaza ndoa......
nani alikwambia huwa tunataka kuolewa haraka haraka.....
au mnadhani huwa na sisi hatuhitaji kuwachunguza.....
next time usirudie......ni kosa kubwa sana kushobokea ndoa mapema.....
pole lakini.....itapita utazoea....ndio maisha......
umenena vema
 
hakuna kuchunguza wala nini chumbia mtu ambaye historia yake unaijua. cio kkrpuka kutaka oa mtu ambaye si ndugu wala rafiki zako wajuaye historia yake na tabia yake kwa ujumla
 
Ulikuwa Plan B..., in case Shit Happens.

Alafu miezi minne tu ushapanga kupeleka posa ?, kujuana ni muhimu pia.
 
Do not regret...maana destiny yako haiko attached to that lady who has gone. turn around-songa mbele. Hizo ni experiences za maisha tu braza. Usikatishwe tamaa eti mwanamke mpaka umchunguze mwaka 1,2,3,etc. Ni hulka tu za baadhi ya dada zetu. wanaishi kimtegomtego, ki-mbinumbinu hivi hata kwa watu walioko serious...
 
Pole kwanza. Hamna muda kamili wa kupeleka posa. Hata wiki moja inatosha tu kama roho wa bwana kakuonyesha. Mambo haya huwa tunachukulia kibinadamu ndio maana hatufiki mbali. Tumshikirishe Mungu kwenye haya. Unaweza ukakaa na mwanamke/mwanamme hata miaka kadhaa lakini ikawa bure tu
 
Unajua waswahili husema nyota njema huonekana Asubuhi. Na kwa maelezo uliyonipa hapo juu yanatosha kuniambia kabisa kuwa huyo demu hafai na hata kama ungemuoa bado ungeishia kulia tu. Mshukuru Mungu kwa kukuepusha naye na umuombe akutafutie mwenzi bora wa maisha.
 
Back
Top Bottom