Hii sentensi ipo sahihi au huwa tunakosea??

Wali kuku ni lugha ya hotelini ama kwa utaalamu zaidi maneno haya huitwa sajili (Register) ni namna ya uzungumzaji kulingana na shughuli inayofanyika mf. Hotelini-wali kuku, hospitali-ASA, PCM 2 mara 3, nk. Yote kwa yote kuna utumizi wa lugha kwa minajili ya kupamba lugha kama hivyo, mf. Hotelini mhudumu anapouliza, Nani wali ng'ombe? Swali hili huburudisha
 
Wali kuku ni lugha ya hotelini ama kwa utaalamu zaidi maneno haya huitwa sajili (Register) ni namna ya uzungumzaji kulingana na shughuli inayofanyika mf. Hotelini-wali kuku, hospitali-ASA, PCM 2 mara 3, nk. Yote kwa yote kuna utumizi wa lugha kwa minajili ya kupamba lugha kama hivyo, mf. Hotelini mhudumu anapouliza, Nani wali ng'ombe? Swali hili huburudisha
Lengo kumbe ni kuburudisha...
 
Ngoja nikuchanganye zaidi lakini usipotee! Wewe ulikwenda kwa kuku akakulaki na kukupa wali ambawo ukala, ulitosheka au la! matumizi ya kiunganishi KWA. Si hivyo tu, kuku mlishirikiana kuumonda ule wali. Pale ulipotumiya kiunganganishi NA. Unataka usahihi wa kisarufi au katika maana! Unataka usahihi upi? :drum:
 
Ngoja nikuchanganye zaidi lakini usipotee! Wewe ulikwenda kwa kuku akakulaki na kukupa wali ambawo ukala, ulitosheka au la! matumizi ya kiunganishi KWA. Si hivyo tu, kuku mlishirikiana kuumonda ule wali. Pale ulipotumiya kiunganganishi NA. Unataka usahihi wa kisarufi au katika maana! Unataka usahihi upi? :drum:
kisarufi na maana pia!
 
Katika swala la chakula kuna lugha za hotelini kama nakumbuka vizuri wanaita (rejesta) nilisoma zamani.

Kusema wali kuku ni sawa lakn ukija home nitasema wali na nyama ya kuku.
 
yote ni sahihi wali kwa kuku au wali na kuku unamanisha kusema wali na kitoweleo chake ni kuku
 
Hongera, kwa kuiweka mada hadharahi. Unataka usahihi upi wa kimuundo au ule wa kimaana? Wataalamu husema tungo kama hizi husema ni mofu tata. Kimsingi huwategemea sana watumiaji wa lugha na muktadha wao. kama ilivyo katika matumizi ya lugha na matokeo yake, ni kuelewana ama kutofautiana. Hoja ni je, msikilizaji ameelewa nini katika masimulizi yanayohusu maakuli! :A S-coffee:
 
Back
Top Bottom