Hii sensa kama maigizo

Sasa mbona mnawashangaa waislamu wanapoambizana hakuna kuhesabiwa wakati tatizo linajulikana.

jibu lipo clear tu kwamba watanzania kwa sasa wamechoshwa na porojo,,,,,unamwambia mtu anapaswa kuhesabiwa ili umsogezee huduma,,,ni kama kumdhihaki maana wanayoyasikia kuhusu ufujaji wa pesa za umma hiko kitu kinaumiza mioyo,,,,,pili mtu hawez kuacha kutafuta UGALI wake ukaja kumwambia amsubiri karani,,,,na mwamko huu ndio unaendelea hadi 2015,watanzania wengi zaid hawatapiga KURA sababu ya yale yanayoendelea bungeni,,,,,
 
[h=6]serikali yacheza mchezo mchafu: Yatumia magazeti ya uhuru na tanzania daima kudanganya umma wa kiislam kuwa baraza kuu la maulamaa wametangaza rasmi kushiriki sensa.

Huu ni uongo na hayati ulamaa kupitia katibu wao leo wamekanusha. Hivyo huo ni uongo na wamesema kama njia waliyotumia kuweka msimamo huo nasi kama ni kuutengua wangetumia njia hiyo hiyo.
Nawapenda waislam wote haswa wale wajitambuao na kufanya ibada.
[/h]


sensa ya mwaka huu imejaa griba na ubabaishaji mwingi. Leo hii yamebaki masaa machache ya kuanza zoezi lenyewe lakini cha ajabu vifaa bado havijakamilika, sehemu ya malipo ambayo makarani tulipaswa kulipwa ikiwa ni pamoja na pesa ya nauli, tulitakiwa kulipwa tarehe 22-8-2012 mpaka sasa hakuna. Vifaa vingine ni mabegi, vitambulisho, penseli maalumu, sare, fomu mbalimbali hadi leo hii bado hatuna na kuanzia kesho usiku tunatakiwa kuanza zoezi hivi kweli hii sensa kutakuwa na ufanisi?

Katika zoezi hili wameingiza kipengele cha rejesta kwa ajili ya vitambulisho vya taifa nje ya mkataba na baadhi ya sehemu hatujaambiwa tutalipwa shilingi ngapi sasa hapo tutegemee matokeo mazuri?

Kuna watu wanaenguliwa licha ya kujaza mikataba ili nafasi zao zichukuliwe na watoto wa wakubwa au jamaa zao pasipo utaratibu mzuri hivi tutegemee matokeo mazuri?

Tuliambiwa kuna mabegi maalumu ya kuhifadhia madodoso ili yasichafuke lakini ajabu tumepewa madodoso mikononi.

Tuliambiwa tutapewa pesa kwa ajili ya viogozi wa mitaa kututembeza maeneo yao na wameanza kututembeza jana lakini hadi jioni hii hakuna kinachoendelea. Utafikiri ni dharura kumbe ilipangwa miaka kadhaa nyuma. Ubabaishaji huu utaisha lini?
 
waislam karibu milioni 35 hawatajiandikisha zoezi hili kwa jinsi hamasa ya waislam inazidi kuongezeka siku hadi siku tusubiri tuone!

sasa km waislam karibia mil.35 hawatajiandksha,mnabishana nini sasa,TZ bara ina watu mil.40,visiwani mil.1,na ukisema 35 ml,hawahesabiwa ni wale wanaogopa,ukijumuisha wasiogoma unaweza kupata mil.39 bara na z'bar,we huon hapo mpo asilimia 99 ya watz wote? Sasa mnagoma nin wakati idadi mnaijua,au kaubabe tu?
 
Back
Top Bottom