Hii niyo tofuati yetu na wenzetu

oba

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
310
65
Hii ndiyo tofauti yetu nchi maskini- Tanzania na wenzetu walioendelea; UWAJIBIKAJI!!!! sisi ni wapuuzi, tena sana! tuna sheria nyingi lakini hazifanyi kazi maana zikivunjwa adhabu stahiki hazizolewi isipokuwa kwa wachache wanaoonewa na mfumo.......hivi inaingia akilini kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili haina kipimo cha CT scan kwa muda wa takribani miezi 11? hospitali ya taifa? wakati hospitali za watu binafsi zina kipimo hicho muhimu kwa matibabu sahii ya wagonjwa?kwamba watu binafsi wana hela nyingi sana kuliko serikali hata kufikia kiwango cha kuwa na CT machines ku;iko serikali? kama siyo upuuzi ni nini?hatuna fedha au hatuwajibiki kwa yeyote? hatuna sababu ya kuumia na kutafuta kila kinachowezekana kupata hiyo huduma kwa ajili ya afya za wagonjwa wetu?hatuwaonei huruma wagonjwa wetu wanaolazimika kulipa 282000 pale regency kwa ajili ya huduma hiyo ambayo ilikuwa inapatikana kwa 50000 muhimbili? hivi wenye dhamana ya kuhakikisha huduma hiyo inapatikana waendelee kusamehewa eti hawana cha kufanya kurejesha huduma za CT scan?......natamani nchi hii ikabidhiwe mikononi mwa dikteta mmoja kama mwl Nyerere au Kagame ili wawanyoshe viongozi wapuuzi wa nyakati hizi; nasikia hasira!!!!
 
Back
Top Bottom