KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
Jamani naomba tufahamishane labda mimi huwa nafanya makosa. Hivi kati ya mwanamke na mwanaume walioko ndani ya ndoa ni nani anayepaswa kumwambia mwenzake kuwa nahitaji kufanya tendo la ndoa? Maana siku zote mimi huwa ndiye ninayemwambia mke wangu kuwa nina hamu na tendo la ndoa.Sasa huwa nabaki nikijiuliza au huwa namkwaza mwenzangu,au huwa anaogopa kuniambia?,au huwa hana hamu na mimi? Au huwa hataki tuu. Tafadhali naomba tufahamishane.