Hii ni kwa wana-CHADEMA tu

Nafurahi kuwa watu wengi wana uchungu na nchi. Mawazo mengi ya wanachadema yanaonyesha tatizo kubwa ni vijana kutopiga kura na ufahamu mdogo wa watu vijijini. Tukumbuke kuwa ule utaratibu wa kuchangia kwa neno CHADEMA umeuwawa na ccm baada ya kuyatisha makampuni ya simu. Sasa wazo langu ni kuwa kwanza tutambue kuwa matatizo yaliyotuangusha igunga yapo kila jimbo, hivyo ili tukabiliane nayo tufanye operation kitaifa. Chadema iendelee na operation Sangara maana ilionesha mafanikio makubwa. Pili chama kianzishe program za kufungua ofisi za matawi vijijini; hii ni kazi kubwa na inahitaji pesa kwahiyo hapa wanachama tujifunge mkanda. Zifunguliwe accounts katika kila benki lakini zisimamiwe na Chadema makao makuu, halafu uwekwe utaratibu wa chama kutoa riport kila baada ya miezi mitatu ambazo zitawekwa ktk mitandao ya kijamii, na media zingine. Utaratibu huu unaonekana mgumu lakini unawezekana maana ndivyo walivyofanya wafuasi wa Obama; watu walikuwa wanachangia hata dola 5 lakini riporti zilikuwa zinaonesha kila hela iliyochangwa na projected budget. Ikifanyika hivyo basi CCM inaweza hata kujitoa 2015 kwa kuogopa aibu.
 
Chadema sasa sio chama maskini. kama imeweza kushindana kigharama na CCM katika uchaguzi huu ina maana kuwa sasa chadema ina uwezo wa kuanzisha ofisi zake katika hatua za chini yaani huko vitongojini, vijijini na kuwaajiri wanachama wa kuzisimamia ofisi hizo ili zitoe huduma kwa wananchi, na pia kuandikisha na kuwafuatilia wanachama wake. Huku vijijini hatuna viongozi wa nyumba kumi wa Chadema. mashauri yetu yanasikilizwa na viongozi wa nyumba kumi wa CCM. Maisha ya kawaida tunazungukwa na CCM; CDM tunaiona huko kwenye gazi za taifa tu.

Wengi tunaiangalia chadema kutokana na matatizo ya kitaifa lakini haya ya huku vijijini kwetu tunajikuta hatuna namna bali kuwaangukia CCM watuhudumie maana chadema hatupo. Mfano uchaguzi wa serikali za mitaa. huku vijijini hatuna chadema, CCM wanapita bila kupingwa.

Chadema sasa tubadilike hizo hela za ruzuku tuzitumie kujenga chama ngazi za chini, tusisubiri upepo wa uchaguzi tu.

CCM inashinda tu kwa sababu ya mtaji wa wanachama waaminifu. na kiukweli wanao wengi sana, Sisi chadema hatuna wanachama bali tuna wapenzi; ambao kwa bahati mbaya sana wengi wao si wapiga kura.

CCM huwa wanafanya sensa ya wapiga kura wao kila ifikapo karibu na uchaguzi. kwa kutumia wale viongozi wao wa nyumba kumi hupita nyumba hadi nyumba. kwanza huuluza kama wanafamilia ni wana CCM then wanawauliza kazi zao za chama then, kadi zao za kupiga kura. Takwimu hizo zinawasaidia kujua kuza za uhakika hata kabla ya kampeni. Kipindi cha kampeni wanakitumia kijalizia tu hizo kura za wanachama wao

Sisi chadema hatuna takwimu kama hizo. tunategemea hotuba zetu za kampeni tu na ushawishi wa muda mfupi. Hii haitotusaidia kamwe.

CHADEMA needs big revolution on its management and organization system.
Mkuu nakuunga mkono lakini nadhani ndo ngoma imeaanza. Chama kimekua ghafla na mahitaji yake ni makubwa kila sehemu wanahitaji kuwa na tawi la chadema. Gharama huenda zikawa kikwazo pia lakini viongozi wanapashwa kujitokeza na kusema ili watu wajue wasaidie vipi chama.
 
ucjali mkuu...tactic za ccm muda unavyozidi kwnda ndivyo wanavyozidi kuproof failure...ndio maana maujanja(hila) ni mengi...mi nadhani trend ya cdm ni nzuri tu ukilinganisha na watawala(sipendi kuwaita viongozi) wetu

naamin viongozi wachadema ni makini. Chamuhimu ni kufanya utafiti na nakujua sababu za kimsingi zakutopiga kura. Hili nijambo la msingi sana kwa chaguzi zijazo. Mbinu za magamba ni za hila zaidi cha msingi nikuuza sera kama tulivyofanya igunga.
 
Nadhani elimu hii ikianza sasa, 2015 nadhani tutaeleweka, tutakuja na mikakati ya kazi, tuombe uzima, kwa mfano kutoa nchanganu kuwa hela wanayosema ccm wanatumia kujenga barabar si ya wanachama wa ccm, ni hela ya watanzania wote, wakulima, wafanyabiashara, madini n.k, yawezekana wakulima wanadhani hele ya kuendesha serikari inatolewa na ccm ndio maana wanaogopa kuiondoa

Elimu ya uraia ni muhimu sana sio kwa Igunga au Tabora tu bali kwa Tanzania nzima, hasa maeneo ya vijijini kwa ile mikoa ya pembezoni na iliyo nyuma kimaendeleo na kielimu.
 
ndugu zangu wana cdm( nasisitiza ni chadema tu) matokeo ya igunga yamenifanya nije na wazo.Huu si wakati wa sie kutulia na kuacha hili jambo linapita bila kulifanyia kazi.Kifupi ushauri wangu harakati za chama ziendelee chini ya viongozi hapo wilayani kwa kuimarish chama kama walivyoshauri watu wengi mikutano mijini na vijijini watu wapewe elimu ya uraia .kukubalika kwa cdm kumenistua sana na hili jambo lisiachwe hivi hivi.mwalimu aendelee na mikutano ya kushukuru wananchi na kuendelea kuwapa taarifa wale 22000 na zaidi ambao hawaitaki ccm.wana cdm tuwe tayari kusapport juhudi kama hizi. Maeneo mengine wameweza kwa kutumia michango toka kwa wanachama na changizo mbalimbali. Hili linawezekana wana cdm tujitoe hata kwa mali ili ukombozi upatikane naomba kuwasilisha

Pamoja na kuunga mkono hoja nadhani viongozi waandae maandamano kwenye yale maeneo ambayo bado yale maandamano yetu hayajafanyika. Maeneo kama Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Mtwara, Lindi Pwani na kisha hitimisho liwe Dar. Unajua kama kuna kitu kilichoiinua CDM ni yale maandamano. Hiyo ni njia nzuri sana ya kuonyesha hisia, na jinsi watanzania walivyochoka hiyo ndiyo njia ya kuimarisha imani ya wananchi kwa chama. Hili haliondoi umuhimu wa kuingia zaidi vijijini na kuwakomboa wananchi kifikra. Hawa watu wa vijijini ndio wametuangusha Igunga, laiti kama CDM ingeingia huko mapema nina imani hali ingekuwa tofauti. Hata hivyo makamanda mnastahili pongezi kuingia Igunga vijijini ndani ya miezi miwili hivi na kutoa upinzani mpaka wana magamba wakachanganyikiwa.

Pamoja tutashinda, hakuna kukata tamaa, japo ichelewe haki daima itashinda. Ni suala la wakati tu.
 
niwazo ambalo nillilokuwa naliwaza sana,je sisi wa jf mchango wetu nini katika chama zaid ya kusifia tu? naunga mkono hoja na mkakati mahususi ufanywe haraka iwekanavyo
 
naunga mkono hoja 100%. what is next step?

Utaratibu wakuchangia unaongeza intimanse kwa chama na nidhamu hiyo itatufanya kutotamani kitu au vitu kutoka cdm zaidi ya uongozi bora utakao ondoa na kero za wananchi na hatimaye tukaacha kutwa nchi maskini.
 
Ndugu watu walikata tamaa kuona kuwa wanajiandikisha na kupiga kura then wanashindwa so kwa kufanya hayo hapo juu cdm itafika mbali.lifunguliwe tawi hapa jf then litaratibu kila kitu.
 
Naunga mkono hoja mia kwa mia. Nafarijika sana tena sana kila nikiona harakati za ukombozi wa kweli. Niko tayari hata kwa kuchangia.
 
Naunga mikono na miguu yote, kwanza hoja yako nimeipa kipaumbele kuliko zote zilizotangulia, pili nimekugongea like, na tatu mimi naanza kwa mfano kwa kuwaelimisha watakao elewa na wale wasio waelewa nitaweka utaratibu wa kununua shahada zao siku chache kabla ya uchaguzi wowote na kuzichoma moto, namshauri Dr aungurumishe chopa tena igunga awaite wananchi wote kwenye mkutano mkubwa zaidi ya ambayo imeshawahi kufanyika ili kuwashukuru wanaigunga na pia kuwatia moyo pamoja na mgombea wao ili wajue kuwa cdm haikuwa kwao kwa ajili ya madaraka au ubunge bali kwa mapenzi ya cdm kwao...kama bajeti ya chopa hamna wana cdm tuko wengi huku jf tunaweza kujichanga na kufanikisha hilo ni mtazamo wangu tuu....nawasilisha
 
Hivi hatuwezi kumwajiri Mwalimu Kashindye kufanya hii kazi kwa mkoa mzima wa Tabora? Nadhani si ngumu kumlipa japo allowance sawa na ule mshahara na malupulupu aliyokuwa anapata wakati akiwa afisa elimu.

Tujiulizeni jamani mchango wetu ni upi katika ukombozi wa nchi hii? Wenzetu wanatumia matajiri kufadhiri chama lakini cdm haina matajiri hivyo ni sisi walalahoi tutawafadhiri cdm mpaka kieleweke.

Tunaomba viongozi wa cdm watupatie ile namba ya kutuma neno 'CHADEMA' kwenda kwenye short code ya wasp ili tuchangie kwa airtime. Ni pesa ndogo sana lakini kama kila mtu atafanya hivyo mara kwa mara anapo recharge simu yake itasaidia sana kupata kiasi fulani kikatumika kwa ajili ya Elimu ya uraia vijijini.

Mkuu umetoa wazo zuri sana,
huu ndio mda wa kukijenga chama na wazo hilo inabidi lianze sasa na
liwe endelevu,....naimani hadi kufikia 2015 kitakua kimepatikana kiasi cha kutosha na
michango hiyo itakua imesaidia kujenga chama kwa kiasi kikubwa
 
Nafurahi kuwa watu wengi wana uchungu na nchi. Mawazo mengi ya wanachadema yanaonyesha tatizo kubwa ni vijana kutopiga kura na ufahamu mdogo wa watu vijijini. Tukumbuke kuwa ule utaratibu wa kuchangia kwa neno CHADEMA umeuwawa na ccm baada ya kuyatisha makampuni ya simu. Sasa wazo langu ni kuwa kwanza tutambue kuwa matatizo yaliyotuangusha igunga yapo kila jimbo, hivyo ili tukabiliane nayo tufanye operation kitaifa. Chadema iendelee na operation Sangara maana ilionesha mafanikio makubwa. Pili chama kianzishe program za kufungua ofisi za matawi vijijini; hii ni kazi kubwa na inahitaji pesa kwahiyo hapa wanachama tujifunge mkanda. Zifunguliwe accounts katika kila benki lakini zisimamiwe na Chadema makao makuu, halafu uwekwe utaratibu wa chama kutoa riport kila baada ya miezi mitatu ambazo zitawekwa ktk mitandao ya kijamii, na media zingine. Utaratibu huu unaonekana mgumu lakini unawezekana maana ndivyo walivyofanya wafuasi wa Obama; watu walikuwa wanachangia hata dola 5 lakini riporti zilikuwa zinaonesha kila hela iliyochangwa na projected budget. Ikifanyika hivyo basi CCM inaweza hata kujitoa 2015 kwa kuogopa aibu.

Sidhani kama njia ya kutuma neno CHADEMA imeuawa. Hii huhitaji kwenda kwa watu wamtandao bali unaelewana na watu wanaitwa WASP ambao wao tayari wanaendesha hii biashara na watu wa mtandao ambao mtakuwa mnagawana mapato.

Hii ni njia rahisi sana kwa watu wengi wenye simu. Na kunaoption ya ku register na unakuwa unakatwa hele kila baada ya muda fulani.

Kwa mfano tunaweza kuamua kutumia njia ya kujiregister kwa WASP na kuchagua uwe unakatwa mara ngapi labda kwa mwezi na kiasi gani. Say naweza kusubscriber monthly deduction ya Tsh. 5000. hivyo wasp anakuwa anapeleka request kwa operator ya mimi kukatwa hiyo hela kila mwezi kutoka kwenye credit ya Simu yangu. Cha msingi ni lazima ni hakikishe na recharge simu yangu angalau hiyo subscription yangu kila mwezi na ziada kwa ajili ya kutumia simu.


Hii ni Kitu halali na mtu ana subscribe au kujiondoa kwa hiari yake hamna wizi wala nini.

Chadema waongee na wasp juu ya concept hii kama inaungwa mkono na watu wengi hapa.
 
ni kweli nimesoma habari moja ya kustua kwamba gari moja la matangazo la ccm lilikuwa likipita kwenye baadhi ya vijiji siku ya uchaguzi wakitangaza kwamba mgombea wa cdm amejitoa laiti wale wananchi wangekuwa na elimu ya uraia leo tugekuwa tunasema haya na ushahidi kamili.sijajua mstakabali wa mwalimu kuhusu ajira yake hivyo wana chadema lazima tufikirie haya sio kutulia kuja kuibukia 2015.

Hilo pia ni la msingi
 
dah!! wazo zuri, mm ningechangia trilion 3 lakini naogopa Mbowe asizifyeke kwenye miradi yake ya mafuso mabovu!!!!!!!!!
 
Kimsingi wazo ni zuri na naimani 2nachokiandika kinatoka chini na uvunguni wa mioyo ye2 na kwa kua viongozi we2 ni wackivu naimani watalifanyia kazi na pengine zoezi la uchangiaji linaweza kuwatayari hata kabla ya siku 7 kuanzia leo sambamba na zoezi la kuwashukuru wapiga kura wa igunga kwa kujitahidi bila kujali vitisho kuikaribisha kesho yao yenye furaha na lakini wakaporwa haki yao ya kuchagua lakini 2nawaambia wacfe moyo na wacrudi nyuma saa ya ukombozi ni sasa.
 
CDM ifanye utaratibu wa namna ya sisi wananchi tuweze kuwachangia fedha ili zitumike katika harakati za "OPERATION ELIMU VIJIJINI" Hata kwa kutuma sms inatosha, hakuna kitu ambacho kitaniuma kama CDM isipochukua NCHI 2015, harakati ni sasa kamanda MBOWE, DKT WA UKWELI, KABWE ZITO, KAMANDA LEMA, SCHOOL OF LAW {TUNDU LISU}, KAMANDA HALIMA, MNYIKA, KAMANDA HECHE, N.K.
Vijana na Umma wa watanzania tupo nyuma yenu.
Mungu bariki TANZANIA, Mungu bariki CHADEMA.
AMENI.
 
Back
Top Bottom