Hii ni hospitali ya TAIFA - Muhimbili!

Mnafikiri ni sababu gani zitakazowafanya viongozi wetu waikumbuke Muhimbili wakati wao wanatibiwa India?
tupitishe sheria rais, makamu wa rais na waziri mkuu peke yake ndio watatibiwa njee kwa garama ya serikali iwapo watakuwa na tatizo kubwa wengine tubanane huko muhimbili ama sivyo ujigaramie mwenyewe kwenda apolo tuone kama muhimbili haitawezeshwa.
 
Mkubwa hapo sasa unataka Rais/Waziri/Katibu mkuu aje apange files!?N adhani hilo ni jukumu la hao watendaji ila kama na wao wanalalamika kama wewe lazima hali kama hii ijitokeze.Swala hapo ni watendaji hawataki kutimiza wajibu wao, siiamini kama wamekosa hela yakununua file.
TUIPENDE NCHI YETU NA TUWE WAZALENDO,TANZANIA ITAJENGWA NA KUBOMOLEWA NA WATZ WENYEWE.Wewe kamaumejitoa vile umebaki kulalamika tu kila cku MNH, nenda Botswana acha kutuboa
 
mkuu mswald kwani umelazimishwa kuchangia?..na nikweli sipo huko nipo katika Private practise ila bado ni Medical practise, ila hii si mada...issue ni utendaji na mfumo mzima katika hospitali zetu za serikali..sasa vifaa vya kulishia watu mahututi yaani Nasogastric tube,NGT na gloves vinapotumika isivyopaswa bado unaona ni sawa na kuleta mada ya kwenda Botswana?!!!
 
Mkuu hayo ya kawaida huku mikoani ndo usiseme, hakuna karatasi mgonjwa anaandikiwa kwenye karatasi la gloves na inawekwa kwenye file... Maisha yanaendelea!
Kumbe gloves zipo?
Bora yenu!
 
Kinachoifanya Tanzania iendelee kuwa na umasikini na kukosa ufanisi ni tabia ya kukosa maadili kwa watanzania. Kwa mfano kiongozi badala ya kufuata maadili ya kutumikia wananchi anachukua pesa kwa manufaa yake binafsi. Mfano mwingine wa kukosa maadili ni pale daktari au mtumishi wa afya anapopiga picha nyaraka binafsi za wagonjwa zenye majina yao na namba za mafaili yao na kuziweka kwenye vyombo vya habari. anakiuka patient confidentiality!

Tukitambua kuwa maadili yanaanza kwa kila mmoja wetu tutafika, iwapo tutaendelea kulilia wengine wawe na maadili ilhali sisi hatuna maadili tutakuwa tunajidanganya tu.
 
Kinachoifanya Tanzania iendelee kuwa na umasikini na kukosa ufanisi ni tabia ya kukosa maadili kwa watanzania. Kwa mfano kiongozi badala ya kufuata maadili ya kutumikia wananchi anachukua pesa kwa manufaa yake binafsi. Mfano mwingine wa kukosa maadili ni pale daktari au mtumishi wa afya anapopiga picha nyaraka binafsi za wagonjwa zenye majina yao na namba za mafaili yao na kuziweka kwenye vyombo vya habari. anakiuka patient confidentiality!

Tukitambua kuwa maadili yanaanza kwa kila mmoja wetu tutafika, iwapo tutaendelea kulilia wengine wawe na maadili ilhali sisi hatuna maadili tutakuwa tunajidanganya tu.

mkuu doctor-patient confidentiality ni kuhusu ugonjwa ila suala la nani kalazwa hospitali sivyo, kutaja usiri ya UGONJWA ni kukiuka maadili kweli lakini not just names.
 
mkuu doctor-patient confidentiality ni kuhusu ugonjwa ila suala la nani kalazwa hospitali sivyo, kutaja usiri ya UGONJWA ni kukiuka maadili kweli lakini not just names.

What if these names would have been that of your close relatives or yourself ( when you went for consultation to Dr X ) on the news paper, JF etc?! Would it be the same to you? You are misusing your position (authority by vartue of your profession) to give out patients records without their consent. STOP leveraging your wants on your patients' vulnerabilities. You need to go back to your medical ethics classes!!
 
Si sahihi kusema tarehe ya mtu ya kuzaliwa, kusema kuwa siku fulani afya yake ilikuwa na mgogoro, kusema kuwa Dr. Fulani alimtibia. Taarifa hizo ni mali ya mgonjwa na kuziweka kwenye vyombo vya habari ni ukiukwaji wa maadili. Hawa mnaoweka majina yao hapa ni watu wa Kama kuna chuo kinafundisha kuwa kukiuka maadili ni kutaja ugonjwa tu basi wanafundisha uongo.
Chukua mfano mtu ana ugonjwa wake ambao ameamua kuufanya siri na tarehe husika aliaga nyumbani anaenda kumtembelea rafiki ili aende hospitali, halafu the following week file lake linawekwa kwenye media, huoni kuwa kitendo hicho kitamkwaza mgonjwa na kusababisha kuogopa kuhudhuria hospitali next time? Tabia hii inawafanya wagonjwa wakose uhuru wa kueleza matatizo yao hospitalini.
 
Si sahihi kusema tarehe ya mtu ya kuzaliwa, kusema kuwa siku fulani afya yake ilikuwa na mgogoro, kusema kuwa Dr. Fulani alimtibia. Taarifa hizo ni mali ya mgonjwa na kuziweka kwenye vyombo vya habari ni ukiukwaji wa maadili. Hawa mnaoweka majina yao hapa ni watu wa Kama kuna chuo kinafundisha kuwa kukiuka maadili ni kutaja ugonjwa tu basi wanafundisha uongo.
Chukua mfano mtu ana ugonjwa wake ambao ameamua kuufanya siri na tarehe husika aliaga nyumbani anaenda kumtembelea rafiki ili aende hospitali, halafu the following week file lake linawekwa kwenye media, huoni kuwa kitendo hicho kitamkwaza mgonjwa na kusababisha kuogopa kuhudhuria hospitali next time? Tabia hii inawafanya wagonjwa wakose uhuru wa kueleza matatizo yao hospitalini.
Absolutely, nakubaliana na hoja yako. Ulimbukeni wa kujua kupost vitu kwenye mtandao utawaponza wabongo.
 
Mkuu Measkron, yaani hata continuation sheets hazipo, imagine NGT(Nasogastric tube) na gloves(clean gloves and not sterile) ndio zinatumika kufungia karatasi za wagonjwa??? zikipotea nani alaumiwe? vifaa navyo vikipotea-kama feeding tubes(NGT) zinatumika??Sijui tunaelekea wapi, kama hii ndio Hospitali ya TAIFA!!!!

Basi haraka sana utasikia kule bungeni, mbunge mmoja wa CCM atasema "... matatizo hayo yote yamesababishwa na Chadema..."
 
Aiseeee baba yangu mi nikiumwa nabakigi huku huku rombo kutibiwa kuna hosp yetu ya mkuu aina tofauti na apolo mungu wangu
 
Jamani serikali haina hela kwa sasa... Subirini mpaka tukiuza twiga na wanyama wengine then tutapata hela za kununua baadhi ya vitu sawa.. Au kama vp nendeni private hosp maana baadhi ya hizo hospital viongozi wenu wana shares huko so inabidi mzitumie kidogo maana hizo hospital za serikali zikiboreshwa nani ataenda private hosp?
 
Ulitegemea nn mkuu? Pesa zote serikali inapeleka makanisani kupitia MoU. Badala ya kujenga na kuboresha hospitali zake serikali yetu imekazana kumimina mabilioni kwenye hospitali za kanisa ambazo pamoja na kupata mabilioni hayo bado gharama za matibabu ziko juu. Ni mpaka pale serikali itakapoacha kupoteza pesa za kodi zetu kugharamia makanisa ndiyo itaweza kusimamia mambo yake. Serikali isiyo na dini na kufadhili kanisa wapi na wapi!!!?
 
Back
Top Bottom