siamini kama uko serious,nimecheka sana!aisee mimi wa kwangu akigeuka namzaba kibao!
Hapo wala hujakosea BJ kuangalia uumbaji sio kosa kabisa lakini kwa wenzetu nyinyi akina mama sijui ni wivu au kutojiamini.Mimi siku moja nilimpeleka wife kwenye soko la samaki,kufika yeye akaingia ndani mi nikabaki nje namsubiri basi akapita mrembo wa haja aliyeumbwa akaumbika,nami mtoto wa kiume bila hiyana nikawa namsindikiza kwa macho nilikuja kushtuka mtu ananibip na kofi mgongoni ,kugeuka namkuta wife kachachamaa unaangalia nini kwani mimi sikutoshi?Lakini ningekuwa mimi wala tusingefika huko.Kwa hiyo basi mi naona kutazama ni kama kuufurahia utukufu wa mungu katika uumbaji.
Hiyo poa tu mbona. hata mimi wa kwangu kama hajaona huwa namshtua, ila lazima atoe comments; ndo starehe yangu.
mwanzoni alikuwa anaibia kuangalia, alidhani ananikwaza kwa kuangalia wazi wazi, siku moja aliibia halafu alipnigeukia alinikuta namwangalia huku nacheka nikamwambia Uwe na amani tu, hakuna ubaya ku-appreciate uumbaji
Tatizo ni pale mwanaume akiona kila mwanamke anapita shingo lilee hata kama unamwongelesha haelewi kitu..yani mtu hata mkirudi kwenye maongezi akili yake haipo kabisa,ya uumbaji kama utampataje?mawasiliano yake nk.. inawezekana nyie mnawaza zaidi
Mie simkatalii aangalie wanawake wengine mana pia urembo kuna kuzidiana, kwahiyo fahari ya macho ashindwe yeye tu!!
he he he! hapo atanishangaza!!!!Tatizo ni pale mwanaume akiona kila mwanamke anapita shingo lilee hata kama unamwongelesha haelewi kitu..yani mtu hata mkirudi kwenye maongezi akili yake haipo kabisa, inawezekana nyie mnawaza zaidi ya uumbaji kama utampataje?mawasiliano yake nk..
Mie simkatalii aangalie wanawake wengine mana pia urembo kuna kuzidiana, kwahiyo fahari ya macho ashindwe yeye tu!!
swali ni hili kwa nini wanawake wengi wanakereka wakiona mwanaume wake
anatazama vifaa vingine,wakati macho hayana pazia,na kutazama sio kula???????????