Hii ni Ajabu Kwangu

Chapa Nalo Jr

JF-Expert Member
Dec 8, 2010
7,514
6,488
Kuna jamaa mmoja kanisimulia kitu ambacho kwangu mimi ni ajabu, ana wanawake kadhaa nje ya ndoa, mke wake amekuwa akifuatilia sana simu yake. Sasa jamaa kaamua kubuni mbinu kwa kuajili katibu muhtasi wa ku-coordinate mademu wake. Hivyo hao mademu wake hawatakiwi kumpigia simu yeye badala yake wanampigia kijana wa kiume(ana saloon ya kiume) ambaye ndiye hufikisha ujumbe kwa jamaa. Ili kufanikisha vizuri mpango wake ameachana na mademu wake wa zamani kwa kuwatengenezea visa tu ili hawa wapya wasiwe na simu yake isipokuwa ya coordinator. Amempa huyo coordinator mikakati murua jinsi ya kupanga mambo. Maswali mengi yameniibukia kwa ufafanuzi ila sikupata muda wa kumuuliza.

Kweli shetani haishiwi mbinu.
 
Katumia mbinu ya kizamani sana aisee. Mwambie ajiunge JF akasome zile sheria mama za infidelity...
 
sawa dada(naamini ni she) nimekupata, hebu tupe na ushamba wenu mnafanyaje kuwazunguka waume/mabwana zenu?
mimi sina ndoa niko single sina mbinu yoyote ya kucheat subiri wadau.ila sidhani kama kuna mtu anafanya mambo hayo ya kishamba hapa jf
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom