Hii ndoa itadumu kweli?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,796
Ni ile ndoa ya ajabu kuwahi kutokea ulimwenguni! Ndoa ya mke mmoja waume wawili....
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulileta maana kipindi cha waasisi wake ambao kwasasa wote ni marehemu Mwalimu JK Nyerere na Mzee Karume , muunganiko wa Tanganyika na Zanzibar ni matokeo ya vita baridi wakati huo
Mahitaji ya wakati yaliufanya muungano huu uanze kupoteza maana kuanzia mwaka 1985 mzee Mwinyi alipoingia madarakani....Ni kuanzia kipindi hicho yalianza kutokea mabadiliko kadhaa kwa upande wa Zanzibar kuelekea nchi kamili huku kitu kinachoitwa 'kero za muungano' kikiongezeka kila wakati
Ili nchi itambulike kuwa nchi inahitaji haya
.mipaka kamili
.katiba
.Bendera
.Sarafu
.Majeshi
.Bunge
.Rais
.wimbo wa taifa
.uongozi wa kisiasa au kijeshi nk
Mabadiliko ya taratibu yaliyofanyika kwa vipindi tofauti ndani ya miaka 30, vimekuja kuirudisha Zanzibar kama nchi kamili na si sehemu ya Mungu ni (siwalaumu)
Kilichopo kwasasa ni muunganiko wa kisiasa tuu kwamba chama kimoja cha siasa kinahudumu katika nchi mbili tofauti (hilo laweza kuwa ajabu mojawapo la dunia sawa na mke mmoja kuolewa na waume wawili)
Kumekuwa na utamaduni ndani ya ccm rais kuwa mwenyekiti wa chama pia...hili limefanyika kwa kipindi chote cha utawala wa ccm
Jana ilikuwa pia kukamilisha utaratibu huo wa kumkabidhi Magufuli uongozi wa chama...tunajua mengi yalifutikwa chini ya zulia ili mchakato uende salama japo kuna nyuso zilionyesha waziwazi kuwa hazikuridhika kabisa (ushahidi wa hotuba yake ulidhihiri hilo)
Magufuli ni mtendaji si mwanasiasa, Magufuli hana uvumilivu na hili kakari mwenyewe, mtu ambaye hana uvumilivu hana tafakuri hana diplomasia...siasa zinataka hivyo vitu...Muungano umedumu kwasababu ya uvumilivu tafakuri diplomasia na unafiki kwa upande mwingine
Je chini ya Magufuli muungano huu utadumu? Muda utaamua
 
1469339450778.jpg
1469339456586.jpg
1469339475022.jpg
1469339486472.jpg
 
Mimi si mtaalamu wa utabiri ila kuna mama wa suluhu pembeni yake. Unaweza ukadumu kwa ngwe ya mwanzo
 
Ndoa itadumu kama kijijini hatatokea mwanaume mwingine(CUF) lakini akiingia katika kijiji kile ndoa itavunjika tu>
 
Mshana jana nimeota ndoto mbaayaa...

Ya tembo kuendelea kufa
Mmh tembo kuendelea kufa? Ndoto nyingi huja kinyume tafsiri yake..! Labda iwe ndoto maono ama ndoto taarifa
 
Ndugu Mshana, mengine yote uliyoweka hapa sina tatizo nayo....ila hiyo ramani. Hiyo mipaka mkuu, hiyo mipaka! Tanganyika haina mipaka inayopita ulivyoiweka hivyo.

Na ilitangazwa ni kosa kuweka/kutumia ramani yenye kupotosha.
 
Ndugu Mshana, mengine yote uliyoweka hapa sina tatizo nayo....ila hiyo ramani. Hiyo mipaka mkuu, hiyo mipaka! Tanganyika haina mipaka inayopita ulivyoiweka hivyo.
Asante kwa kuliona hilo ili ujue upotoshaji ulipo na watu wameukalia kimya...hiyo ramani iko kwenye makabrasha ya muungano
 
Oohooo! Mkuu, unasema kweli? Hivi hii nchi ina mikosi au ni nini?
Mikosi inaletwa na unafiki wa kujifanya tuna nchi mbili zilizoungana wakati kiuhalisia muungano huo ulishakufa siku nyingi...hivi ikitokea leo ccm wakaanguka kwenye uchaguzi upande mmoja wa huo muungano, tutasema kuna muungano tena hapo?
 
Mimi huwa nashangaa kwanini picha huwa inamuonesha Kambarage pekee akichanganya udongo.. Mwenzake yule sheikh alikuwa wapi..? Ni kama muoaji mmoja kumvika mwenzie pete na kujivika yeye mwenyewe..looks like upande wa masheikh haukuwa tayari.
 
Ukiambiwa uthibitishe Mkuu utafanya hivyo? Sisi humu hatuna shida , hao wenyewe wakihitaji uthibitishe hilo, na makbrasha ya muungano umeyapataje? Nyaraka za serikali
Kiongozi wala usipate shida ingia hapa mipaka ya Tanganyika na Zanzibar
 
Back
Top Bottom