oba
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 310
- 65
Kwa uhakika, sakata la mgogoro kati ya madaktari na watumishi wa afya linaendelea kuchukua sura mpya baada ya bunge kujipitishia nyongeza ya posho zao hadi 200,000 huku serikali ikidai haina pesa ya kutekeleza matakwa ya madaktari katikati ya bajeti.
Najaribu kufikiria kuwa hiyo nyongeza ya posho za wabunge kuwa imefanywa katikati ya bajeti au ilikuwa ni agenda ya siri ambayo haikuwekwa wazi wakati wa bajet.
Nionalo mimi ni kuwa SERIKALI IKO TAYARI KUUA WANANCHI WAKE KULIKO KUSIKILIZA HOJA ZA MADOKTA na ktk hili sitawasamehe viongozi!
Ningekuwa mimi ningefanya hivi kwa hoja za madokta;
1. Ningeamuru ma intern doktaz wote waliohamishwa warejeshwe muh2 walipokuwa awali
2. Ningewachukulia hatua viongozi wa wizara waliokuwa chanzo cha mgogoro na kuchangia mauaji haya ya wananchi na kwanza ningeanza na katibu mkuu kwa kumtimua kazi
3. Ningemsimamisha kazi mkurugenzi wa Hosp ya muh2 kwa kushirikiana na katibu mkuu kuua watu
4. Ningetangaza nyongeza ya poso za madokta hadi 40,000- half per diem
5 Ningeamuru wafanyakazi wote wa afya wapewe green kadi za bima ya afya
6 Ningeagiza mchakato wa mishahara na allowances za madokta na wana taaluma ya afya ziwe reviewed within a month na kurekabishwa
7. Ningeagiza haraka kurekebishwa kwa huduma za afya na nyongeza za vitendea kazi kwa wagonjwa ikiwemo kuongeza vitanda vya wagonjwa na vifaa vingine
8. Ningeagiza utaratibu uanze wa kununua mabasi ya wafanya kazi wa afya kwa kila hospitali ambayo yangewachukua na kuwarudisha makwao kila siku
9. Ningeanza utaratibu wa kuwakopesha madokta magari ili kuwapunguzia adha ya kugombania na kubanana na wagonjwa wao kwenye daladala
10. Ningewaomba madokta samahani kwa usumbufu niliofanya kama serikali na kisha ningewasihi warejee kazini huku mchakato wa kuyatimiza yote hayo ukiendelea
Nawasilisha
Najaribu kufikiria kuwa hiyo nyongeza ya posho za wabunge kuwa imefanywa katikati ya bajeti au ilikuwa ni agenda ya siri ambayo haikuwekwa wazi wakati wa bajet.
Nionalo mimi ni kuwa SERIKALI IKO TAYARI KUUA WANANCHI WAKE KULIKO KUSIKILIZA HOJA ZA MADOKTA na ktk hili sitawasamehe viongozi!
Ningekuwa mimi ningefanya hivi kwa hoja za madokta;
1. Ningeamuru ma intern doktaz wote waliohamishwa warejeshwe muh2 walipokuwa awali
2. Ningewachukulia hatua viongozi wa wizara waliokuwa chanzo cha mgogoro na kuchangia mauaji haya ya wananchi na kwanza ningeanza na katibu mkuu kwa kumtimua kazi
3. Ningemsimamisha kazi mkurugenzi wa Hosp ya muh2 kwa kushirikiana na katibu mkuu kuua watu
4. Ningetangaza nyongeza ya poso za madokta hadi 40,000- half per diem
5 Ningeamuru wafanyakazi wote wa afya wapewe green kadi za bima ya afya
6 Ningeagiza mchakato wa mishahara na allowances za madokta na wana taaluma ya afya ziwe reviewed within a month na kurekabishwa
7. Ningeagiza haraka kurekebishwa kwa huduma za afya na nyongeza za vitendea kazi kwa wagonjwa ikiwemo kuongeza vitanda vya wagonjwa na vifaa vingine
8. Ningeagiza utaratibu uanze wa kununua mabasi ya wafanya kazi wa afya kwa kila hospitali ambayo yangewachukua na kuwarudisha makwao kila siku
9. Ningeanza utaratibu wa kuwakopesha madokta magari ili kuwapunguzia adha ya kugombania na kubanana na wagonjwa wao kwenye daladala
10. Ningewaomba madokta samahani kwa usumbufu niliofanya kama serikali na kisha ningewasihi warejee kazini huku mchakato wa kuyatimiza yote hayo ukiendelea
Nawasilisha