Son of Africa
JF-Expert Member
- Jan 16, 2011
- 233
- 31
Kweli raisi ni EL lakini kwetu Rais ni JK upo? Ipo tofauti kati ya Rais, raisi na Rahisi, nadhani EL wako ni raisi true
Karama yoyote awayo nayo binadamu yaweza kuwaletea furaha ama maombolezo wale wanaomzunguka,inategemea anaitumiaje.Agree with u, ana power ya uongozi.
<br /><span style="font-family: century gothic"><font size="3">Wana JF, kwa muda mrefu kumekuwa na maelezo yanayokinzana, hasa kuhusiana na uadilifu na uwezo wa uchapakazi wa Lowassa kwa kipindi cha utumishi wake kwa nchi hii, na hasa katika nafasi za uwaziri alizozishikilia. Kama namna nzuri ya kujaribu kutafakari utendaji wake, tujikumbushe kidogo alikopitia Lowassa.</font></span><br />
<span style="font-family: century gothic"><br />
<font size="3">1. Mwanzoni mwa miaka ya 90 Lowassa alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, akishughulikia majanga, na itakumbukwa kwamba huu ndiyo wakati ambao mikoa ya kusini na hasa Mtwara walikumbwa na mafuriko yaliyoteketeza maisha ya watu pamoja na mali zao na baadhi ya athari hizo bado hazijarekebishwa. Akiwa ndiye mhusika mkuu, Lowassa aliratibu upatikanaji na utoaji wa misaada na inasemekana alijinufaisha yeye binafsi kutokana na janga hilo kwani mingi ya misaada haikuwafikia walengwa.<br />
<br />
2. Baada ya kutoka hapo, Lowassa alipelekwa Wizara ya Ardhi na ni katika kipindi hiki ndipo tulishuhudia kilele cha migogoro ya ardhi (double allocations) maeneo ya Mbezi Beach, na hata kuporwa kwa maeneo ya wazi na kuyatolea hati, hasa maeneo ya Masaki, Msasani Peninsular na Oysterbay, katika mazingira ambayo yanaashiria kwamba kulikuwa na vichocheo vya rushwa. Ni katika kipindi hiki ndipo rushwa ilipokithiri wizarani na yeye mwenyewe kujilimbikizia viwanja, majumba na utajiri ambao ulikuja kuhojiwa na Mwalimu mwaka 1995 alipogombea nafasi ya kugombea urais. Ndicho kipindi cha kushamiri kwa wahindi kama Fida Hussein na Baghdad katika kupora viwanja na inasemekana Baghdad alikuwa na viwanja 100 Dar peke yake. Hadi leo serikali inahangaika kufanya revocation ya hati alizozitoa Lowassa katika mazingira ya utata.<br />
<br />
3. Wizara ya Maji na Mifugo. Shida ya maji jijini Dar es Salaam iliongezeka na mtandao wa maji nchini uliendelea kuwa duni na kushindwa kusogea kwenye malengo ya serikali ya maji safi kwa kila mtanzania kufikia 2015. Ndicho kipindi cha utapeli wa Dawasco na wawekezaji wa Bi-Water baada ya kuona karibu atashtukiwa aliwafurusha na kuzua kesi iliyoigharimu serikali mabilioni katika kuiendesha. Alizunguka nchi nzima na kuhimiza wananchi wajenge wabanda ya ng'ombe, akiahidi kukopesha ng'ombe ili wananchi walipe ng'ombe. Mabanda haya sas yamegeuka maghala baada ya miaka inayokaribia 10 ya kusubiri. Hali ya soko la wanyama wetu ilibaki kuwa isiyo na ufumbuzi, licha ya yeye kutoka katika jamii ya wafugaji.<br />
<br />
4. Ofisi ya Waziri Mkuu. Zaidi ya kututwisha mzigo wa Richmond, na kudandia hoja ya sekondari za kata iliyoasisiwa na utawala wa Mkapa, hakuna la kujivunia zaidi ya kukemea na kudhalilisha wafanyakazi wa chini yake. Aliendesha vikao vya kujadili bei za mazao na kuwaita wakuu wa mikoa na wilaya lakini hakuna ufumbuzi wa maana aliokuja nao kuhusu bei za mazao yetu kama pamba, korosho, kahawa, chai na pareto.<br />
<br />
Mimi nawasilisha maoni kwamba utumishi wa Lowassa umegubikwa na kukosa uadilifu na kushindwa kuleta tija inayohitajika kwa watanzania. Hoja za kwamba alikuwa mchapakazi ni porojo tu za kudhani zitaficha maovu ya ufisadi wake.</font></span>
Huyu jamaa inaonekana hajui kabisa hicho alichokiandika!hivi wewe ni mkimbizi eeh?itakuwa umetokea Libya ivi majuzi ndo maana hujui mazuri aliyotenda huyo jamaa!Lowasa ni nondo anajua siasa pia ni mchapa kazi kwa maisha yake yakawaida na serikali ndo sababu ana pesa nyingi,we ng'aa macho utakufa na umasikini wako,jamaa elimu yake inambeba ana akili nyingi!usimsingizie mambo yako ya kinafiki!
<br />
<br />
Ndugu yetu Mudavadi, hata kama na wewe ni lile kundi uliotumwa kumtukana Lowassa, basi angalau uje na hoja ili tuweze kuchangia. Hakuna kiongozi nchi hii kwa miaka ya karibuni aliyekuwa scrutinised kama Lowassa, na naomba uelewe maana ya hilo neno scrutinised. Sidhani kama kuna jambo baya ambalo hatujaambiwa, either kupitia kwenye forum hii au magazeti yale yaliyopo kazini chini ya Mropokaji Nape. Lakini kila siku najiuliza, mbona hatujadili mazuri na mabaya ya viongozi wengine tunaodhani wana uwezo kwa 2015? Unajikuta kwamba tunaompenda na wanaojifanya hawampendi, wanaona ndiyo solution pekee kwa nchi yetu lakini wasiompenda wanaogopa ile aibu yao kama ikitokea Mungu akamjalia kuwa Rais wa nchi hii. Lowassa amefanya mengi makubwa nchi hii na wote tunajua, hata wewe Mudavadi unajua, Tanznia inajua na Dunia inajua. Tusipotoshane na tuendelee kujadiliana kwa hoja, I love LOWASSA, nitampigia kura ya urais saa yoyote, sehemu yoyote, come rain or sun or thunderstorm. Ramadhan kareem wadau
yaani pamoja na mambo yote mh. lowasa aliyofanya "RICHMOND" na mengineyo na kuliingiza taifa kwenye hasara! bado kuna watu wanamsifia...! sikatai ni mchapakazi... lakini .. mhhh! hafai kuwa kiongozi , yeye mwenyewe aligundua hilo pale alipojiuzulu uwaziri mkuu
Alikuwa mzuri pale alipokuwa the director wa Arusha conference centre baaasi. Wewe Ona waziri gani ajishushe mwenyewe kwenda ofisini kwa Mohame Enterprise-Mohamedi Dewji? Anaingia ndani na kukaaa masaamanne huku sisi tukisubiri interview! Matajiri wote wa kihindi kafanya nao deal za ajabu ajabu. Ramesh Patwa aliwahi hata kumkodia ndege, kwa hisani gani? Kweli huyu atweza kututoa katika reseccion? my grave will vote for him and not my living body!!!!!!!
We mjinga, wewe unafaidika na wiziz wake. Watanzania ni wengi, wapo wa kuongoza nchi hii, siyo huyo mwizi firauni, hafai!Haya unayoandika ni upumbavu tu na wivu...we unashinda internet kumtukana Lowassa wakati yeye na wanaye wanafanya kazi za kuzalisha na kuimarisha kipato cha familia yao,hamwezi kulingana...WANA AKILI KULIKO WEWE!
sasa naomba kujua kati ya hawa nani anafaa kuwa Rais wa TZ 2015 toka toka chama chetu CCM
- PINDA
- MEMBE
- SAMWEL SITTA
- NAHODHA
- NCHIMBI
- MWANDOSYA
- SALM A SALM
- MALECELA (nadhani hajacha kampeni ya Urais)
- LOWASSA
- ASHA ROSE MIGIRO
sasa naomba kujua kati ya hawa nani anafaa kuwa Rais wa TZ 2015 toka toka chama chetu CCM
- PINDA
- MEMBE
- SAMWEL SITTA
- NAHODHA
- NCHIMBI
- MWANDOSYA
- SALM A SALM
- MALECELA (nadhani hajacha kampeni ya Urais)
- LOWASSA
- ASHA ROSE MIGIRO
<br />Mbona wewe unashinda kwenye keyboard kujipendekeza kwa familia ya Lowassa, unajuaje kama hao kina lowassa wana akili kuliko reformer, kwangu mimi mtu anayejipatia kipato kwa njia za kifisadi hana maana.