Hii ndiyo picha halisi inayoonyesha uwajibikaji wa CCM ilala....Lukuvi....mh!!!

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
Mimi sielewi hivi mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, mbunge na madiwani wanafanya nini au ni nini kimeshindikana hadi watoto wakae chini wakati sijaona Landcruiser za wakubwa hawa zimekosa mafuta??

mtihani%20wa%20mock.jpg


source: Majira
 
wakati jana nilisimuliwa kisa cha mgogoro wa mpaka uliosogezwa na aga khan schools kuingia upande wa zanaki secondary, yule mama mwl mkuu alitokwa na machozi kwamba watoto au wajukuu wetu watakosa pa kusomea huko baadae , manispaa, wilaya inajua lakini hamna kitu naomba wahusika wafuatilie ile shule yetu ina historia yake.
 
Kitu nachojiuliza kila mara ni kwa nini pesa za kuendesha vikao, semina, mafuta ya magari, vipuri, chai ya maofisini n.k. inapatikana lakini viti vya kukalia watoto wetu madarasani hakuna.

Hawa hawa makuwadi wa ufisadi (CCM) wanatembea kifua mbele eti wanaboresha maisha ya wadanganyika??

Uone CCM wasivyofikiri, kampuni kama coca cola hawalipi ushuru kibao, kwa nini viti wanavyovitoa kwenye baa na kumbi za starehe visitolewe mashuleni?? kama kweli CCM na serikali yao wanawakumbatia wawekezaji, ni kwa nini basi badala ya kutoa viti kwenye baa wasivitoe mashuleni!!!!
 
hizi ndo ajabu ukienda baa,hotel hukosi kiti lakini watoto wanasoma eti wnakaa chini, ndo watawala wetu hao halafu wapo kifua mbele,dah inatisha
 
kwanza hata mfumo wa watoto wetu kukalia madawati umepitwa na wakati kwa nini tusitumie viti vya plastic tu?? Najua watasema oh...mara siyo imara lakini hivyo imara kama tunashindwa kwa nini tusitumie ambavyo tunakalia baa??

Prof. Maghembe mwenyewe anajua tuliwahi kukaa naye pale kwenye baa ya kambarage morogoro na tulikalia viti vya plastic, je anashindwa nini kuvitumia kusaidia watoto wetu mashuleni??

Zipo hata meza za plastic ambazo bei yake ni nafuu, hili pia najua wabongo watasema ah.... mbona zinavunjika haraka lakini swali ni je, hizo imara tunaziweza?? na kama tunaziweza kwa nini CCM na serikali yao wanazishindwa??

Prof. Maghembe, tunataka mabadiliko????
 
Mimi sielewi hivi mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, mbunge na madiwani wanafanya nini au ni nini kimeshindikana hadi watoto wakae chini wakati sijaona Landcruiser za wakubwa hawa zimekosa mafuta??

mtihani%20wa%20mock.jpg


source: Majira

Hakika hii picha ukiiangalia mara 2 unaweza kutoa machozi, ni kweli taifa linaloweza kununua gari moja kwa TZS 110,000,000 linalomtoa waziri, katibu au Mkurugenzi masaki kwenda posta na kurudi linashindwa kutoa TZS 500,000,000 kununua madawati ya nchi nzima
 
Hakika hii picha ukiiangalia mara 2 unaweza kutoa machozi, ni kweli taifa linaloweza kununua gari moja kwa TZS 110,000,000 linalomtoa waziri, katibu au Mkurugenzi masaki kwenda posta na kurudi linashindwa kutoa TZS 500,000,000 kununua madawati ya nchi nzima

Halafu sijui CCM na serikali yake kama kweli wanashindwa kufikiri au wanafanya makusudi. Hivi viongozi wote walio mijini wakipewa colora limited hawata fika mjini?? au ni wazito kuliko uwezo wa gari ndogo???
 
hizi ndo ajabu ukienda baa,hotel hukosi kiti lakini watoto wanasoma eti wnakaa chini, ndo watawala wetu hao halafu wapo kifua mbele,dah inatisha

Hapo ndio na sisi watu wazima wakubwa tuliulize tunawaidiaje hawa watu wazima wadogo... nakumbuka nilisoma kwenye matofali hadi darasa la nne lakini alikuja mzee mmoja pale kijiji chetu alihamasisha mpaka wazazi wakachangia madawati

Cha maana ni kujenga pamoja... Ilala kuna watu wako poa wangeweza kuchangia halafu na serikali nayo ijitutumue, tuidai [hasa kwa vitu kama hivi]

Tukikaa kugemea wenye vyeti feki, tutangoja mpaka yesu arudi tena
 
CCM hawana fikra mlizo nazo ninyi. wao wanafikiria kutawala na kuendelea kuwatawala ndo maana watafanya kila hila mpumbae muwapigie kura pamoja na vizazi vyenu
 
siku hizi nadhani kuanzia diwani watoto wao hawasomi hizi kayumba kwa hiyo hakuna mwenye uchungu hata mmoja na madawati wala majengo ya hizi shule
 
[hizi ndo ajabu ukienda baa,hotel hukosi kiti lakini watoto wanasoma eti wnakaa chini, ndo watawala wetu hao halafu wapo kifua mbele,dah inatisha[/QUOTE]

Na wanene miongoni mwao huko baa wanakalia viwili viwili (au hata vitatu)
 
Hakika hii picha ukiiangalia mara 2 unaweza kutoa machozi, ni kweli taifa linaloweza kununua gari moja kwa TZS 110,000,000 linalomtoa waziri, katibu au Mkurugenzi masaki kwenda posta na kurudi linashindwa kutoa TZS 500,000,000 kununua madawati ya nchi nzima
Pole sana Bill lkn hii ndiyo Tanzania na Chama Chao cha kupindu aka CCM nambali one...maisha bora kwa kila mdanganyika....kuna watu wana hasira na CCM lakini watapozwa na Kanga, T-shirt, Kofia, Pilau (msosi) then watasahau shida zao zote na maisha yanaendelea... sijui tuwaelimishaje wadanganyika maana mpaka kero, maana ukiangalia maswala ya EPA, magari wanao tembelea viongozi wetu,richmond,melemeta,majengo pacha ya BOT, mgao wa umeme nk halafu uangalie halisi ya wadanganyika kweli machozi yatakutoka... kama kweli watanzania tunakereka basi tuwaonyeshe Tarehe 25/10/2009..
 
Serikali ikitaifisha mali zote za wizi toka kwa mafisadi basi shule zote zitaweza kupata madawati. Pesa ipo ila mikononi mwa wajanja. Angalia sasa, hii si hujuma watoto kukaa chini wakati kuna watu wanaishi kama wapo peponi??
 
kwanza hata mfumo wa watoto wetu kukalia madawati umepitwa na wakati kwa nini tusitumie viti vya plastic tu?? Najua watasema oh...mara siyo imara lakini hivyo imara kama tunashindwa kwa nini tusitumie ambavyo tunakalia baa??

Prof. Maghembe mwenyewe anajua tuliwahi kukaa naye pale kwenye baa ya kambarage morogoro na tulikalia viti vya plastic, je anashindwa nini kuvitumia kusaidia watoto wetu mashuleni??

Zipo hata meza za plastic ambazo bei yake ni nafuu, hili pia najua wabongo watasema ah.... mbona zinavunjika haraka lakini swali ni je, hizo imara tunaziweza?? na kama tunaziweza kwa nini CCM na serikali yao wanazishindwa??

Prof. Maghembe, tunataka mabadiliko????

Binafsi sioni sababu ya kutumia meza na viti vya plastic, iwe bar, shuleni au nyumbani. Mtu huishi kutokana na mazingira yaliyomzunguka. Tumezungukwa na ardhi kubwa na misitu ya kupandwa ya mbao laini (soft wood) kama Cyprus, bines, mikaratusi nk.

Wenzetu kule Uarabuni, Asia na hata Ulaya hawana soft wood za kutosha ndo maana wanatumia plastic. Hawa jamaa wangekuwa wanaishi Africa hata viti vya mabasi vingekuwa vya mbao.

Tatizo letu tunapenda kutumia vitu wanavyotumia wenzetumpaka tumefanywa soko la kila kitu. We don't need plastic chairs/tables. Lets be innovative.
 
Binafsi sioni sababu ya kutumia meza na viti vya plastic, iwe bar, shuleni au nyumbani. Mtu huishi kutokana na mazingira yaliyomzunguka. Tumezungukwa na ardhi kubwa na misitu ya kupandwa ya mbao laini (soft wood) kama Cyprus, bines, mikaratusi nk.

Wenzetu kule Uarabuni, Asia na hata Ulaya hawana soft wood za kutosha ndo maana wanatumia plastic. Hawa jamaa wangekuwa wanaishi Africa hata viti vya mabasi vingekuwa vya mbao.

Tatizo letu tunapenda kutumia vitu wanavyotumia wenzetumpaka tumefanywa soko la kila kitu. We don't need plastic chairs/tables. Lets be innovative.

Kama umenielewa ndo maana ktk masuala yote uliyo highlight imesema "kama CCM na serikali yake wameshinwa basi watumie hata plastic". Lakini najua kwamba plastics siyo a better option lakini kama CCM siyo innovative what do we do???
 
Ukweli ni kwamba, hakuna mtu Tanzania ya leo anaewania madaraka ili alete maendeleo kwa sababu ana uchungu na nchi. Wanaloliwaza ni wao watafanikiwa vipi kujiendeleza wao binafsi na familia zao. Si CCM tu, hata hao wapinzani wanalolitafuta ni hilo. Inatia uchungu sana!!!!
 
Back
Top Bottom