Kweli,na hichi kitu kinanikera kweli.Ila mara nyingi unajikuta umeanza kama slang halafu unajikuta imekuwa tabia!nimesikitika sana kuona hata kwenye bang! magazine,na michuzi akiwa ndio chief editor. Mwishowe tutaharibu lugha yetu iwe kama kiswahili cha kenya!
Una bahati mkuu wengine kwetu haikuwa hivyo,..Nina bonge la kithembe yaani omba mungu usinikute,.Sidhani kama ni 'slang' hii ni kutofundishwa matumizi sahihi ya lugha.
Nakumbuka hata wakati nikisoma shule ya msingi mama yangu
alikuwa akinisahihisha matamshi. Tulikuwa tuna lazimishwa kusoma kile
kitabu kinachoitwa "soma kwa hatua" Ni bahati niliweza kusisitiziwa
msingi mzuri nyumbani. Lakini kuna ambao aidha hawakupata mwalimu
mzuri au msimamizi aliye fuatilia elimu yao nyumbani.