TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 4,963
- 15,239
Jamaa ametoka home anaenda zake mjini. Sasa kawaida amezoea kuweka simu yake mfukoni upade wa kulia. Mara akiwa kwenye daladala, akapanda abiria mmoja yuko rafu rafu kama kibaka vile na kwenda kukaa siti moja na jamaa. Jamaa kuona vile akahamua aihamishie simu yake mfuko wa kushoto, safari ikaendelea. Kufika mjini, yule kijana rafu akashuka, akavuka barabara, akasimamisha daladala nyingine akapanda. Huku nyuma yule jamaa aliebaki kwenye siti akapapasa mfukoni kutaka kutoa simu, hola! Simu haipo. Akapayuka 'Mungu wangu, nimeshaibiwa'! Naye akashuka, akavuka barabara, akingia kwene daladala lile lile liloingia yule kijana. Sasa akawa anafikiria alianzisheje? Apige kelele za mwizi au amkwide tu yule kijana aanze kumpa kichapo? Wakati anaendelea kujiuliza maswali, huku daladala likiendelea na safari, hasira tele, mara simu yake ikaanza kuita. Jamaa nusu azimie. Mfuko wa kushoto!