HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Miezi 2 iliyopita rafiki yangu mmoja alinipa taarifa juu ya mahusiano na mdada mmoja aliyempata kwa njia ya Mtandao mmojawapo wa kijamii, uitwao face book. Kwa maelezo yake, amekuwa akiwasiliana na huyu dada pasipo kuonana naye kwa takriban mwaka na nusu sasa. Uhusiano wao ulikuwa mzuri mno kiasi hata cha kufikia kupeana emails, majina yao halisi na picha ambazo kimsingi zilionyesha uhalisia wa mawasiliano yao!
Kilichokuwa kikimsibu huyu jamaa ni kuwa dada huyo alikuwa akikataa kata kata kuonana na huyo kaka, ingawa maelezo ya kuchat ya kila siku through emails and yahoo messenger na SMS (alitoa namba ambayo ilikuwa blocked kwenye voice call) yalionyesha dada kumpenda kaka kupita maelezo.
Kaka amekuwa akijitahidi kutuma vocha na vijisenti kupitia MPesa kwa ajili ya matumizi kwa takriban mwaka sasa akiamini kuwa ipo siku dada huyo angemkubali maana kuna kipindi rafiki yake mwingine aliwahi kuoa kupitia face book.
Juzi kapokea sms kutoka kwa huyo dada, kuwa yeye ni mwanaume na siyo dada na aliamua kumlia pesa kwa kipindi chote hicho na anamshauri atafute mke badala ya kuendekeza online dating!
Swali: Hivi kweli kuna midume inayojifanya midada kwenye mtandao ya kijamii? Na kwanini wanafikia kufanya haya mambo? Na ni kweli dada huyo ni mwanaume au kamchoka tu huyo kaka na kumtumia msg hiyo kwa lengo la kumkatisha tamaa?
Wenu,
HP
Kilichokuwa kikimsibu huyu jamaa ni kuwa dada huyo alikuwa akikataa kata kata kuonana na huyo kaka, ingawa maelezo ya kuchat ya kila siku through emails and yahoo messenger na SMS (alitoa namba ambayo ilikuwa blocked kwenye voice call) yalionyesha dada kumpenda kaka kupita maelezo.
Kaka amekuwa akijitahidi kutuma vocha na vijisenti kupitia MPesa kwa ajili ya matumizi kwa takriban mwaka sasa akiamini kuwa ipo siku dada huyo angemkubali maana kuna kipindi rafiki yake mwingine aliwahi kuoa kupitia face book.
Juzi kapokea sms kutoka kwa huyo dada, kuwa yeye ni mwanaume na siyo dada na aliamua kumlia pesa kwa kipindi chote hicho na anamshauri atafute mke badala ya kuendekeza online dating!
Swali: Hivi kweli kuna midume inayojifanya midada kwenye mtandao ya kijamii? Na kwanini wanafikia kufanya haya mambo? Na ni kweli dada huyo ni mwanaume au kamchoka tu huyo kaka na kumtumia msg hiyo kwa lengo la kumkatisha tamaa?
Wenu,
HP