Nimekuwa naangalia link ya airtel kwenye JF ambayo inasema 'NUSU SHILINGI YA UKWELI mchana kutwa, mwanzo hadi mwisho'. Nilipojaribu kuifuatilia link hiyo nikakuta ndani ya mtandao wa airtel wanasema airtel kwenda airtel ni Tsh.1 kwa sekunde na airtel kwenda mitandao mingine nchini ni Tsh.3 kwa sekunde. Binafsi nimeshindwa kuelewa kinachoendelea hapo. Ni namna ya kurubuni au kitu gani hasa? Tafadhali mwenye taarifa zaidi anifahamishe.