Hii kauli ya EWURA ni sahihi au ni longolongo zao tu

kaburunye

JF-Expert Member
May 12, 2010
672
74
Wadau; naomba ni-quote kutoka gazeti la majira la leo:

"MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) imesema pamoja na juhudi zinazofanyika kupunguza uchanganyaji wa mafuta ya taa kwenye dizeli na petroli, tatizo hilo halitakoma kama kodi na ushuru wa mafuta hayo utaendelea kutofautiana". Mwisho wa kunukuu

Je ni kweli kuwa tatizo ni kodi ya mafuta na eti kodi ikiwekwa vizuri hapatakuwa na kachumbari kwenye mafuta? au hawa jamaa wanatafuta visingizio tu? Mi nahisi wameshindwa kazi na wanatafuta "escape route". Vituo vinavyochanganya mafuta vinajulikana na hawawezi kukwepa kuwajibika. Ni sawa na kusema ili ufisadi maofisini basi wafanyakazi wapewe mishahara minono. Hata kama kodi ikirekebishwa tatizo litaendelea kuwepo maana wafanyabiashara wanajua hata wakichanganya mafuta hakuna hatua itakayochukuliwa - maana wao wanajali faida kubwa tu haijarishi imepatikanaje.
 
mi naona mchezo umezidi! iwekwe adhabu ya kifungo kwa muuzaji na mmiliki nafikiri wataacha, magari yetu yanaharibika ati
 
Finally, EWURA wamezinduka na kutangaza vita kali dhidi ya vituo vinavyofanya uhuni wa kuchanganya mafuta......

It is too bad kwamba kuzinduka kwao ni mpaka magari ya STATE yaathirike....isingekuwa hivyo, it would have been business as usual..... tatizo la mafuta feki ni la muda mrefu..kutokana na tamaa ya wafanyabiashara wa mafuta wasio waamnifu kutaka faida chapchap

The whole point ya kuwa independent executive agency ni kuwawezesha kufanya kazi kwa ufanisi.....they are well renumerated na pia wana full-autonomy....

Rai yetu kwa all other agencies...iwe SUMATRA (usafiri), TDFA (madawa na chakula),TCRA (communication)....wawe proactive....wasisubiri mpaka litokee janga au limuathiri kiongozi ndio wazinduke.....


Na Richard Makore
18th June 2010

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imepandisha zaidi ya mara mbili viwango cha adhabu kwa wafanyabiashara watakaokutwa na kosa la kuchanganya mafuta ya taa na dizeli.

Hatua hiyo ya Ewura inalenga kukomesha vitendo vya kuchakachukua mafuta vinavyofanywa na wafanyabiashara kwa lengo la kujipatia faida kubwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu, alisema mtu akifanya kosa kwa mara ya kwanza adhabu yake imepanda kutoka Sh. milioni tatu hadi Sh. milioni saba, akirudia mara ya pili atatozwa Sh. milioni 25 badala ya Sh. milioni tano za awali.
Aidha, atakayebainika kufanya kosa hilo kwa mara ya tatu, atanyang'anywa leseni na kufunga kituo chake.

Wakati huo huo, Masebu alisema uchunguzi umeonyesha kuwa mafuta yaliyojazwa kwenye magari ya Ikulu hayakuwa na ubora unaotakiwa. Alisema tayari mfanyabishara wa kituo hicho cha mafuta mkoani Kilimanjaro amepigwa faini pamoja na kumfungia biashara yake. Magari ya Ikulu yalikumbwa na tatizo hilo June 8 mwaka huu ambapo baada ya kuwekewa yalizimika na ksuhindwa kuwaka.
 
Mimi naona adhabu hiyo ni kiduchu. Lazima kuwepo kitisho cha kuswekwa lupango ili watu waone kuwa hili ni suala zito.
 
Back
Top Bottom