masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,171
Katika hali isiyo ya kawaida, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mbezi Jogoo(nyuma ya Cotex) Bw. Juma zmunanka amelazimishwa kujiuzulu leo mbele ya wananchi baada ya mlolonho wa vurumai za kutomtaka kwa kipindi kirefu sasa.
Munanka amekuwa na tuhuma nyingi za kuuza viwanja, nyingi ambazo zimeishia kwenye migogoro na wananchi.
Inasemekana Munanka anachunguzwa na TAKUKURU kwa kukusanya michango toka kwa viwanda vilivyopo sehemu yake kwa mradi hewa wa kituo cha watoto yatims.
Yote tisa, lakini kumi ni la uuzwaji wa kiwanja kilichopokaribu ya kiwanda cha Cotex , sambamba na kiwanda cha juisi ya kusindika cha MAZA.
Wananchi leo waliitishwa ili wapatanishwe na Munanka lakini wamekataa katakata.
Ndipo Juma Munanka akaomba kujiuzulu, lakini akasema aba machche ya kusema kabla ya kuondoka.
Akasema yote ya kuuza kiwanja yalisukwa toka Kwa Mkurugenzi wa Halmashauri Kinondoni, na kiwanja kimeuzwa na Mtu fulani anaitwa Namgongo( kimeuzwa kwa Mbunge-hakutajwa lakini anaishi jirani na hapo).
Munanka aliendelea kufunguka kuwa licha ya Mkurugenzi wa Kinondoni kufahamu na kusimamia mipango, Mbunge wa eneo hilo ( siyo mnunuzi)ana habari(Halima Mdee) ,na vilevile Diwani wa eneo hilo na hata Mkuu wa Kituo Polisi kawe na kwamba shughuli yote iligharimu kiasi cha tsh milioni 300.
Wananchi eneo hilo wameondoka huku wakiwa wamechanganyikiwa!
Munanka amekuwa na tuhuma nyingi za kuuza viwanja, nyingi ambazo zimeishia kwenye migogoro na wananchi.
Inasemekana Munanka anachunguzwa na TAKUKURU kwa kukusanya michango toka kwa viwanda vilivyopo sehemu yake kwa mradi hewa wa kituo cha watoto yatims.
Yote tisa, lakini kumi ni la uuzwaji wa kiwanja kilichopokaribu ya kiwanda cha Cotex , sambamba na kiwanda cha juisi ya kusindika cha MAZA.
Wananchi leo waliitishwa ili wapatanishwe na Munanka lakini wamekataa katakata.
Ndipo Juma Munanka akaomba kujiuzulu, lakini akasema aba machche ya kusema kabla ya kuondoka.
Akasema yote ya kuuza kiwanja yalisukwa toka Kwa Mkurugenzi wa Halmashauri Kinondoni, na kiwanja kimeuzwa na Mtu fulani anaitwa Namgongo( kimeuzwa kwa Mbunge-hakutajwa lakini anaishi jirani na hapo).
Munanka aliendelea kufunguka kuwa licha ya Mkurugenzi wa Kinondoni kufahamu na kusimamia mipango, Mbunge wa eneo hilo ( siyo mnunuzi)ana habari(Halima Mdee) ,na vilevile Diwani wa eneo hilo na hata Mkuu wa Kituo Polisi kawe na kwamba shughuli yote iligharimu kiasi cha tsh milioni 300.
Wananchi eneo hilo wameondoka huku wakiwa wamechanganyikiwa!