Hii italeta maafa makubwa migodini!!!!!!polisi acheni kuua raia

USTAADHI

JF-Expert Member
May 10, 2011
1,516
136
IMEKUWA desturi ya polisi wa TANZANIA kuua wananchi migodini kwa risasi ilimradi tu kulinda maslahi ya wakoloni waliobadilika na kuitwa wawekezaji! kitendo cha polisi kanda maalum hussani mkoani mara kuingia mpaka kwenye makazi ya wananchi na kuumiza mpaka akina mama na watoto sasa kinatia kichefu chefu mfano jana polisi wanasadikiwa kupiga watu wawili risasi katika eneo la TWO -SIX NYABIRAMA PITCH kisha kukamata watu na kuwapiga ovyo kisa waliwakuta vijana wakiokota mawe rejects!, yanayomwagwa pembezoni mwa mgodi,watu takribani 17 wameishapoteza maisha tangu 2005, kuna mtoto wa miaka7 alipigwa bomu na kuondokewa na jicho/ lakini zaidi kamanda chagonja aliwahi kufika katika eneo la MURWAMBE na kuahidi kutowaruhusu polisi kuingia kwenye makazi ya raia na kuwapiga kipindi wanapowakimbia,maana kukimbiwa pia ni ishara yakuogopwa iweje polisi muingie mpaka ndani kupiga hadi akina mama na watoto, hapa watu wanauwawa hata familia 1 inapoteza ndugu wananchi wanavumilia lakini hii sasa imekuwa kero iko siku kitaumana WANAJF TUSAIDIANE KUKEMEA HILI, na diwaniwa eneo hilo amekuwa akiishi kwa mashaka akihofia usalama wake kwa jinsi anavyotishiwa na polisi na mkuu wa wilaya ndugu Henjewele , ukijaribu kusemea tu unapewa kesi za ajabu mfano siku 1 mh Lissu aliwekwa ndani mh Esther matiko,kwa mambo hayahaya,mh Heche alishatishiwa kwa hoja hii akajibu polisi wakanywea .SIKU WATU WAKISEMA HAPANA tarime hapatakalika tena.
 
Migodi, migodi, migodi inauwa!!! this is toooo much! sasa tutafute solution kukaa na kulalamika tu inatosha guys wake up!
 
Guyz!
Mabeberu wanatengeneza matajiri wachache wa kitanzania ambao ni malimbukeni wasioona mbali wakti huo huo wanatengeneza maskini wengi. baada ya hapo watawagombanisha hao matajiri wachache. kwa kuwa maskini ni wengi kila mmoja atatengeneza kundi lake lenye hao maskini. Baada ya hopa tunaanza kichinjana ilhali hao mabeberu wanasafirisha utajiri wetu bila kulipa kodi wala mrahaba. baada ya kuona hatuna mbele wala nyuma kama walivyo somalia ndipo watajidai kuja kusaidia kwa kutoa kipande cha mkate. nasi tutawaona ni masia!!! CCM amkeni ndugu zanguni mnaingia kwenye jeneza bila kujua!!
 
Back
Top Bottom