USTAADHI
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 1,516
- 136
IMEKUWA desturi ya polisi wa TANZANIA kuua wananchi migodini kwa risasi ilimradi tu kulinda maslahi ya wakoloni waliobadilika na kuitwa wawekezaji! kitendo cha polisi kanda maalum hussani mkoani mara kuingia mpaka kwenye makazi ya wananchi na kuumiza mpaka akina mama na watoto sasa kinatia kichefu chefu mfano jana polisi wanasadikiwa kupiga watu wawili risasi katika eneo la TWO -SIX NYABIRAMA PITCH kisha kukamata watu na kuwapiga ovyo kisa waliwakuta vijana wakiokota mawe rejects!, yanayomwagwa pembezoni mwa mgodi,watu takribani 17 wameishapoteza maisha tangu 2005, kuna mtoto wa miaka7 alipigwa bomu na kuondokewa na jicho/ lakini zaidi kamanda chagonja aliwahi kufika katika eneo la MURWAMBE na kuahidi kutowaruhusu polisi kuingia kwenye makazi ya raia na kuwapiga kipindi wanapowakimbia,maana kukimbiwa pia ni ishara yakuogopwa iweje polisi muingie mpaka ndani kupiga hadi akina mama na watoto, hapa watu wanauwawa hata familia 1 inapoteza ndugu wananchi wanavumilia lakini hii sasa imekuwa kero iko siku kitaumana WANAJF TUSAIDIANE KUKEMEA HILI, na diwaniwa eneo hilo amekuwa akiishi kwa mashaka akihofia usalama wake kwa jinsi anavyotishiwa na polisi na mkuu wa wilaya ndugu Henjewele , ukijaribu kusemea tu unapewa kesi za ajabu mfano siku 1 mh Lissu aliwekwa ndani mh Esther matiko,kwa mambo hayahaya,mh Heche alishatishiwa kwa hoja hii akajibu polisi wakanywea .SIKU WATU WAKISEMA HAPANA tarime hapatakalika tena.