Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,707
Kuna propaganda za hovyo kuwa watu weusi wamelaaniwa na Mungu,sijui dhana hii imeanzia wapi,lakini iwe iwavyo mwanzilishi wake lazima atakua anawaogopa watu weusi,huwezi kukianzishia kitu au mtu dhana hasi kama hukiogopi.Weusi una thamani kubwa,shauri yenu mnaobadili nyele zenu,ngozi,majina n.k ili mfanane na weupe.Hivi unajua kama YESU alitoka familia yenye asili ya Africa?Unashangaa nini?YESU ngozi yake ilikua na rangi kama yako.Simoni Mkirene alilazimishwa kubeba msalaba wa YESU kwa sababu alikua na asili ya Afrika kama YESU,alikua anatokea mji uliokua unaitwa Krene(sasa Tripoli).Uafrika wa familia ya YESU unatokana na Musa kumuoa binti Yethro kuhani wa Midiani,huyu alikua mweusi kabisa,lakini Suleimani nae akampa ujauzito malkia wa sheba,hii ilikoleza rangi nyeusi kwenye ukoo wa YESU.Kwenye jamii ya wayahudi kukawa na Wayahudi wenye asili Afrika na wale wengine.Wakati Mtume Mathayo alipoenda Alexandria(Misri) wakristo wa huko walitengeneza sanam za YESU akiwa na pua kama za waafrika,kumbukumbu hizi wakoloni waliziharibu kuondoa ushahidi huu.Shauri yenu mnaoona weupe na nywele za weupe ni jambo la Kimungu!!Amkeni!!