Quinty
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 462
- 74
Hii hali ya Ubungo Bus Terminal inasikitisha sana kuona kuko giza kila umeme unapokatika. Nimeshuka hapo mara kadhaa usiku ni giza nene. Sipendi kuamini kuwa uongozi wa hapo umeshindwa kugharamia generator wakati wa usiku. Hayo makusanyo ya sh. 200/- kila kichwa, 500/- gari ndogo na gharama za kulaza mabasi zinafanyia kazi gani? Wageni wanataabika hawaoni mwelekeo, hawaoni wenyeji wao, wenyeji pia hivyo hivyo hawajui hata mabasi yanayoingia. Wabeba mizigo Na vibaka hawaonekani maana giza. Huduma ya matangazo nayo hamna. Wanaokusanya pesa wanatumia mishumaa..! Watanzania lini tutaachana Na hii dhuluma ya viongozi wetu Na kunyanyasika Na kodi zetu kuliwa bila kupata huduma stahili...?