kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Wanafunzi wamvaa DC kupinga mwenzao kupigwa na mwalimu
Wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari ya Siha, Wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro, wameandamana hadi kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, kupinga mwenzao kupigwa na mwalimu makofi, mateke na ngumi hadi kupoteza fahamu.
Pia waligoma kuingia madarasani, badala yake walimbeba mwenzao kwa machela hadi Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Annarose Nyamubi, ili kumuonyeshea hali halisi kabla ya kumpeleka hospitali.
Mwanafunzi aliyepigwa na mwalimu huyo, ni Baraka Munuo, anayesoma kidato cha sita.
Inadaiwa kuwa kipigo dhidi ya mwanafunzi huyo, kilitokana na kutovaa sare za shule na kukaidi amri ya mwalimu iliyomtaka kwenda kuvaa sare halisi za shule.
Hata hivyo, maandamano ya wanafunzi hao, yalizimwa na polisi walipokaribia kufika katika ofisi hizo na kushauriwa kumpeleka mwenzao hospitalini wakati suala hilo likiendelea kushughulikiwa.
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa majina wakati wa maandamano hayo, baadhi ya wanafunzi, walisema mwenzao alipigwa na mwalimu huyo (jina tunalo) Januari 31, mwaka huu asubuhi wakati wakiwa katika ukaguzi.
Mkuu wa Wilaya, Nyamubi, ambaye alikwenda katika shule hiyo, aliwataka wanafunzi kuwa watulivu wakati serikali ikiwa inalifanyia kazi suala hilo na kuwataka kurejea madarasani.
Wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari ya Siha, Wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro, wameandamana hadi kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, kupinga mwenzao kupigwa na mwalimu makofi, mateke na ngumi hadi kupoteza fahamu.
Pia waligoma kuingia madarasani, badala yake walimbeba mwenzao kwa machela hadi Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Annarose Nyamubi, ili kumuonyeshea hali halisi kabla ya kumpeleka hospitali.
Mwanafunzi aliyepigwa na mwalimu huyo, ni Baraka Munuo, anayesoma kidato cha sita.
Inadaiwa kuwa kipigo dhidi ya mwanafunzi huyo, kilitokana na kutovaa sare za shule na kukaidi amri ya mwalimu iliyomtaka kwenda kuvaa sare halisi za shule.
Hata hivyo, maandamano ya wanafunzi hao, yalizimwa na polisi walipokaribia kufika katika ofisi hizo na kushauriwa kumpeleka mwenzao hospitalini wakati suala hilo likiendelea kushughulikiwa.
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa majina wakati wa maandamano hayo, baadhi ya wanafunzi, walisema mwenzao alipigwa na mwalimu huyo (jina tunalo) Januari 31, mwaka huu asubuhi wakati wakiwa katika ukaguzi.
Mkuu wa Wilaya, Nyamubi, ambaye alikwenda katika shule hiyo, aliwataka wanafunzi kuwa watulivu wakati serikali ikiwa inalifanyia kazi suala hilo na kuwataka kurejea madarasani.