Hi ndiyo ilikuwa tofauti kubwa aliyoigundua Nyerere kati ya Mkapa na Kikwete mwaka 1995

you are a GREAT THINKER OF OUR TIMES.kweli kabisa huyu bwana porojo namchukia kupita maelezo.ameigawa nchi vibaya mno and is not concerned at all.Watanzania tuko kwenye uhasama wa kidini ambao haujawahi kutokea.angalia MISA ya pasaka badala ya kusali usiku sasa watu watasali mchana kwa kuhofia usalama wao maana kuna tetesi kuwa kikundi cha waislamu wabaya wanampango wa kuwateketeza kwa mabomu ya kujitoa mhanga.yeye yupo tu ana chekacheka bila hata kukemea. INAWEZEKANA SIYO KWELI LAKINI ANAPO KAA KIMYA JAMII INACHUKULIA KUWA NI KWELI.Au ni upepo tu unapita?
 
Huu uchambuzi upo bias kidogo, nakubaliana na aliyofanya mkapa ingawa naye alikuwa na mapungufu yake kama ubabe wa kitoto. Kwa kikwete baaadhi ya mambo mazuri aliyofanya ni ujenzi wa chuo kikuu cha Nelson Mandela, kuna barabara nyingi amezijenga, kupandisha mishara kwa watumishi wa umma, nk.
 
Nilishawahi sema kitendo cha J.k. nyerere kuzungukia meza zote kuyaelimisha yale majamaa ya NEC (vichwa maji)-1995 ili yaweze kuona mbali kwa kubadilisha sura ya matokeo kwa kujua fika chaguo lao lilikuwa bomu.

cha ajabu nec hiyo haikujiongeza akili kuwa baba wa taifa alichokimaanisha kwao kuwa chaguo walilokusudia halikuwa chaguo bora na kwa nchi za wenzetu zilizoendelea na watu wenye hisa kubwa ya akili kamwe asilani ibadani lisingekuja jitokeza tena jina hilo kuja na kuomba wadhifa ule ule ambapo hapo awali aliwahi kukataliwa/kuonekana kutofaa kabisa.

Napenda kuhoji ni kwa namna gani NEC ya maccm inavyopatikana au ndo ile kesi ya ktk msafara wa mamba na kenge wamo.

Nasema hivyo kwa kuwa sijauona weredi wao ktk kufanya maamuzi ya kuteua vingozi wao.
Leo hii tunashudia siasa za mme,mke na watoto wakiingizwa kwenye vyombo vya juu vya maamuzi jambo ambalo muasisi wa chama hakuwahi au kuthubutu kulifanya.

leo hii kiongozi anasimama na kunadi kuwa maamuzi ya kugombea urais ni wake na familia yake hivyo yuko radhi kufanya anavyojisikia na si ktk misingi ya chama kama ilivyokuwa ada.

Nyerere alipaona ila majitu ndani ya maccm hayawezi kupima wala kuona mahali alipopaona.
ama kweli wapo watu vichwa maji,lkn hawa jamaa ni beyond comparison!!!!
 
Hongera uchambuzi mzuri, sema tatizo watanzania ni mazuzu! wakipewa sh10,000 na kuambiwa CCM oye basi mpaka gego la mwisho utaliona, na baada ya hapo huyo huyo mtanzania anaanza kulalamika eti serikali haitujali, eti mara ufisadi! Safari ni ndefu, Tanzania bado wajinga ni wengi!!!

Kweli watz ni mazuzu na wajinga ni wengi ikiwa ni pamoja na wewe mkuu.
 
mkapa alikua mtoto wa kiume jamani hata km kuna makosa yeye si mungu.lkn jk mmmmmm""nchi inaongozwa na mama.kwa mara ya kwanza 95% ya wanafunzi kufeli.rais anapenda kujirusha mno ndo maana anajenga viwanja vya ndege wkt tuna kandege kamoja tu kanabeba watu 10 kwenda mtwara hata hamshangai jmn.
 
muongezee JK mafanikio haya:
:Amewajenga TISS kutoka usalama wa Taifa hadi UHASAMA wa taifa.
:Amehalalisha WIZI kwa kuwaambia wezi wa EPA warudishe polepole.
:Ameruhusu vimada wake waishi kwa kodi za wananchi kwa kuwapa vyeo vya kubumba vimada wake wote.
:Ameunganisha UISLAMU dhidi ya UKRISTO na kuwahamasisha KUUTOKOMEZA UKRISTO kimya kimya ameanzisha sera kuu katika historia ya Tanzania na atakumbukwa kwayo nayo ni SERA YA UDINI>
 
Nakubaliana na wewe kuwa Mkapa alikuwa Mtendaji si mwanasiasa. ndiyo sababu alisimamia alichoamini kuwa sahihi hata kama baadaye kikaonekana si sahihi. a leader has to make a decision not follow a decision!!. Tukio moja ambalo mpaka hii leo nampa heshma mzee mkapa ni pale alipokataa kupandisha mishahara ya watumishi wa umma kwa hoja za msingi ambazo wafanayakazi waliridhika nazo alisema hivi:-
Ninatakapopandisha mishahara mfumuko wa bei utaongezeka na hiyo mishahara itaonekana haina msaada. Jamba ninalofanya ni kudhibiti mfumuko wa bei hili hiyo mishahara kidogo ninayotoa iweze kukidhi mahitaji yenu. Hapo alisema alichoamini ni sahihi na baada ya miaka kadhaa kilidhihirika kuwa ni cha msingi. thats what a leader s made of!! JK alipoambiwa aongeze mishahara kwanza akadanya idadi ya watumishi wa umma, pili akadanganya mapato yanayohitajika kuwalipa watumishi. mambo haya yote si ya kiongozi mtendaji!!

A brilliant analysis! Well done...
 
hapo ndo aliamua kusema kwa ,maneno yake kuwa "KAMA NEC MKIAMUA KUMPITISHA JK KAMA MGOMBEA URAIS BASI NIKO TAYARI KUWASHAWISHI WATANZANIA KUWAPIGIA KURA WAPINZANI NA SI KUWAPA KIONGOZI WA AINA HII"
Nyerere hakuwahi kusema hivyo. Uongo mkubwa.
 
sioni tofauti ya nyani na sokwe labda ukubwa wao tusipotoke lets go 2015 chadema tuongoze watanzania huu uzi kimantiki sio makini katiba mpya ikiweka kipengele aliyewahi kutawala agombee unambeba mkapa! Take care!
 
hakika ulichoandika ni chuki tu zisizo na msingi, lakini pia wacha kunukuu nukuu mambo usiyoyajua, ni kheri ukae kimya kuficha chuki zako...ukiona mtu emekupongeza hakika hana tofauti na wewe, usipende kujipa uhakimu wakati huwezi kuhukumu kwa haki" ni dhambi kubwa.
 
Ukweli ni kwamba kila mtu (Mkapa na JK) wana mabaya na mazuri yao, though huzidiana, na sasa ya ------ yamezidi mno na hasa mabaya (Udini ndo pabaya zaidi:nono:) sijui ndo LAIZZER AFFAIR rulling style........
 
Wakati wa mahojiano na Tido Mhando(2010) katika ule Mdahalo feki JK alisema kwa "legacy" yake. Yaani yeye anataka akumbukwe na Watanzania kwamba aliitoa Tanzania hapa akaifikisha pale. Kwa maneno yake mwenyewe.I felt very embarrassed. Hapa nikajuwa kwa uhakika hatuna mtu!
 
Hatujawahi kuwa na Rais mzuri kuanzia Tanganyika hadi Tanzania. Kuanzia awamu ya kwanza ya Nyerere hadi awamu hii ya pili ya Kikwete. Wote ZERO. Nyerere alichukua madaraka ya Tanganyika ikiwa nchi yenye neema. Akawa kama mtoto aliyerithi mali za baba yake na badala ya kuziendeleza akazitafuna zote nchi ikabaki masikini wa kutupwa wakati "anang'atuka.

Vitega uchumi vyote alivyovikuta akavitaifisha akawapa makada wa chama chake kuviendesha ambao hawakuwahi huko nyuma kumiliki hata baiskeli!! Ufisadi ukaanzia hapo na nchi ikafilisika mpaka tukafikia hali ya kushindwa hata kujilisha tukawa ombaomba wa kutupwa. Akaja Mwinyi ambaye ni sehemu ya pili ya awamu ya kwanza kwa maana kwamba aliyemuweka pale ni Nyerere. Naye akatoka patupu. Nchi ikabaki bado taifa maskini wa kutupwa. Akaja Mkapa ambaye anawakilisha sehemu ya tatu ya utawala wa Awamu ya kwanza kwani naye aliwekwa na Nyerere kwa mabavu. Akamaliza mda wake nchi bado masikini wa kutupwa. Akaingia Kikwete ambaye ni awamu ya pili kwani aliingia madarakani bila kete ya Nyerere. Naye mda wake unaishia na taifa bado maskini wa kutupwa.

Kutokana na historia hii. Tusitegemee Rais yeyote kupitia CCM atakayeweza kuinyofoa nchi yetu kutoka kwenye lindi la umaskini tulionao. Mizizi ya CCM ni utapeli, ubabaishaji na ufisadi tangu TANU hadi leo hii CCM.

Rais atakayeweza kuikoa nchi yetu kwenye aibu hii ya umasikini wa kutupwa lazima atokee chama cha upinzani.
 
Hatujawahi kuwa na Rais mzuri kuanzia Tanganyika hadi Tanzania. Kuanzia awamu ya kwanza ya Nyerere hadi awamu hii ya pili ya Kikwete. Wote ZERO. Nyerere alichukua madaraka ya Tanganyika ikiwa nchi yenye neema. Akawa kama mtoto aliyerithi mali za baba yake na badala ya kuziendeleza akazitafuna zote nchi ikabaki masikini wa kutupwa wakati "anang'atuka.

Vitega uchumi vyote alivyovikuta akavitaifisha akawapa makada wa chama chake kuviendesha ambao hawakuwahi huko nyuma kumiliki hata baiskeli!! Ufisadi ukaanzia hapo na nchi ikafilisika mpaka tukafikia hali ya kushindwa hata kujilisha tukawa ombaomba wa kutupwa. Akaja Mwinyi ambaye ni sehemu ya pili ya awamu ya kwanza kwa maana kwamba aliyemuweka pale ni Nyerere. Naye akatoka patupu. Nchi ikabaki bado taifa maskini wa kutupwa. Akaja Mkapa ambaye anawakilisha sehemu ya tatu ya utawala wa Awamu ya kwanza kwani naye aliwekwa na Nyerere kwa mabavu. Akamaliza mda wake nchi bado masikini wa kutupwa. Akaingia Kikwete ambaye ni awamu ya pili kwani aliingia madarakani bila kete ya Nyerere. Naye mda wake unaishia na taifa bado maskini wa kutupwa.

Kutokana na historia hii. Tusitegemee Rais yeyote kupitia CCM atakayeweza kuinyofoa nchi yetu kutoka kwenye lindi la umaskini tulionao. Mizizi ya CCM ni utapeli, ubabaishaji na ufisadi tangu TANU hadi leo hii CCM.

Rais atakayeweza kuikoa nchi yetu kwenye aibu hii ya umasikini wa kutupwa lazima atokee chama cha upinzani.

Ni watu wachache sana wanao ona kama wewe watu tulikula yanga na hakuna kiongozi yeyote wa ccm ambaye ataweza ku-unmask evil things walizofanya wenzao na wao wakiwa ni sehemu ya huo uozo.

Mwingi nae alifanya madudu mengi tu kwanza alishindwa kuuko-control uchumi na inflation ilikuwa kuwa, kuuza mbuga ya lolionda kwa yule mfalme wa arabuni, kugeuza ikulu kuwa bakwata na yeye kuwa mufti mkuu kwasababu yeye ndo alikuwa anatanga mwandamo wa mwezi na sikukuu zake, what a waste president.

Mkapa naye alikuja na madudu yake hasa kwenye ubinafsishaji, kuna makampuni yalikuwa yanafanya vizuri kabla ya kubinafsisha na yalipo binafsishwa ndo yaka chimbiwa kaburi kabisa kuforce kununua president jet wakati hiyo hela wange-inject kwenye shirika la ndege la mwanzo angalu sasa hivi tungekuwa mbali.

Kikwete huyo jamaa hata sijui ana matatizo gani, kwa maana Mkapa anatoka madarakani nafasi ya ukurugenzi wa halmashauri watu walikuwa wanaomba ila alipo ingia yeye tu akaanza teua watu wake wakaja kutufanyia madudu mengi tuu.

Rai yangu kama mtanzania na kwa watanzania wenzangu ni kuwa sisi ndiyo tuna andaa na kuchagua raisi once tunapo mess up hapo itatugharimu kwa kipindi ya miaka 20 inayokuja. Ningependa tujiulize je tunaweza kutoka hapa? Tufuate njia gani kufika pale tunapotaka kufika.
 
tunataka nchi itulie tulii kuliko maji ya mtungini,ukitaka kula kubali kuliwa na wewe ata kidogo
 
Chuo kikuu cha Dodoma bado nasema ni maamuzi ya zima moto na kuhitaji umaarufu usio na maana. Serekali imechukua pesa kwenye social security funds ambazo kuzilipa ni ngum,lakini pia chuo kile kimeshusha sana standard ya elimu Tanzania.Kuna wanafunzi pale wanasoma miaka minne hawafundishwi hata na mwalimu mmoja mwenye PhD
 
Back
Top Bottom