Shoo Gap
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 246
- 71
Kuna mambo mengi kwenye maisha ya kujivunia, ktk elimu leo ninapenda kumkumbuka Mwalimu wangu wa chekekea aliyenifundisha kusoma na kuandika. Hawa waalimu huwa wanafanya kazi kubwa sana sana ambayo inathaminiwa kidogo sana na jamii. Ebu fikiria ni mambo mangapi umefaidi kwa kujua tu kusoma na kuandika? Ilipotokea kijana kafika F1 bila kujua kuandika na kusoma tunabaki kujiuliza maswali mengi tu, Inakuwaje? Ila watu hawafikiri inakuwaje huyu Mwalimu wa chekekea anaweza kuwasaidia hawa watoto wa miaka 5 hadi 8 kuweza kuandika na kusoma na kuelewa maana ya kile wanachokisoma.
Mwalimu huyu zaidi ya kusoma na kuandika alinifundisha namna ya kupika chai, uji, kunawa uso, kuswaki, kufua, kupasi nguo n.k. Nakumbuka enzi hizo nukiwa na visoda vyangu shingoni ninawahi shule, darasani kulikuwa na vibao ambavyo tulijifunzia kuandika kwa kutumia chaki, wakati mwingine tuliandika chini wenye vumbi n.k. Tulijifunza michezo mingi mbalimbali, nyimbo zenye maudhui na mafundisho mbalimbali.
HUYU MWALIMU KAJENGA MSINGI MUHIMU SANA MAISHANI MWANGU.
Binafsi niko ktk mchakato wa kutafuta zawadi ya kumuenzi Mwalimu wangu huyu, niombe wasomi wenzangu kuwakumbuka watu kama hawa waliojenga msingi ktk maisha yetu ya elimu.
Haya nimeona baada ya kuona wanangu wanavyopiga hatua kiakili wakiwa na waalimu wao hawa.
Mwalimu huyu zaidi ya kusoma na kuandika alinifundisha namna ya kupika chai, uji, kunawa uso, kuswaki, kufua, kupasi nguo n.k. Nakumbuka enzi hizo nukiwa na visoda vyangu shingoni ninawahi shule, darasani kulikuwa na vibao ambavyo tulijifunzia kuandika kwa kutumia chaki, wakati mwingine tuliandika chini wenye vumbi n.k. Tulijifunza michezo mingi mbalimbali, nyimbo zenye maudhui na mafundisho mbalimbali.
HUYU MWALIMU KAJENGA MSINGI MUHIMU SANA MAISHANI MWANGU.
Binafsi niko ktk mchakato wa kutafuta zawadi ya kumuenzi Mwalimu wangu huyu, niombe wasomi wenzangu kuwakumbuka watu kama hawa waliojenga msingi ktk maisha yetu ya elimu.
Haya nimeona baada ya kuona wanangu wanavyopiga hatua kiakili wakiwa na waalimu wao hawa.