Mama Mdogo
JF-Expert Member
- Nov 21, 2007
- 2,961
- 2,138
Mheshimiwa Nape Nnauye aliandamana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China Nd Liu wakitoa heshima zao kwenye mnara wa kumbukumbu za mafundi wa Kichina waliokufa wakati wa ujenzi wa reli ya Tazara. Mnara huu uko Majohe,Gongo la Mboto jijini Dar. Hapa katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC ya CCM, Nape Nnauye anaonekana kavaa vazi lisilooana na tukio. Nilitumaini kuwa kwa cheo chake angeziingatia protokali na kuvaa nguo nyeusi au ya deep bluu kama wenziwe. Cha kushangaza zaidi ni kuwa utoaji huu wa heshima kwa utamaduni wa mashariki ya mbali (kuinama au ku-bend) naona hana uzoefu nao. Haya basi, yetu macho na masikio.