VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mwishoni mwa juma nilikuwa nyumbani nilikozaliwa-Visiga,Kibaha.Nikiwa sina hili wala lile,nikapata ugeni nyumbani kwetu.Wakaja jamaa watatu wakidai kuwa na ujumbe wangu.Nikawakaribisha.Salamu zikafuata halafu mazungumzo.
Wakaniarifu kuwa,wao wameagizwa na wazee na vijana wa kata yangu waje kuniambia uamuzi wa wanakata juu ya nani anatakiwa kuwa Diwani wa Kata yetu hapo 2015.Wanataka kumandaa kabisa.Wanadai wamemchoka Diwani aliyepo kwakuwa hakufanya lolote kwa miaka yake 12 aliyokuwa madarakani.Pia,kwakuwa ni Darasa la saba.Wanamtaka msomi na mwenye uchungu na maendeleo ya Kata.Wameniona mimi nafaa.
Wageni wangu wakanieleza mchakato mzima uliwafikisha katika uamuzi wao huo.Mwishoni nikawauliza: kwa chama gani? Wakanijibu: CCM.Mwili wangu ukasisimka kama nimepigwa shoti ya umeme.Sikuwafokea.Nikawajibu kistaarabu tu: Ni heri nisiwe Diwani kuliko kuwa Gamba.Walionyesha kushtuka.Hawakuchelewa kuaga.
Eti WanaJF,nimekosea hapo?
Wakaniarifu kuwa,wao wameagizwa na wazee na vijana wa kata yangu waje kuniambia uamuzi wa wanakata juu ya nani anatakiwa kuwa Diwani wa Kata yetu hapo 2015.Wanataka kumandaa kabisa.Wanadai wamemchoka Diwani aliyepo kwakuwa hakufanya lolote kwa miaka yake 12 aliyokuwa madarakani.Pia,kwakuwa ni Darasa la saba.Wanamtaka msomi na mwenye uchungu na maendeleo ya Kata.Wameniona mimi nafaa.
Wageni wangu wakanieleza mchakato mzima uliwafikisha katika uamuzi wao huo.Mwishoni nikawauliza: kwa chama gani? Wakanijibu: CCM.Mwili wangu ukasisimka kama nimepigwa shoti ya umeme.Sikuwafokea.Nikawajibu kistaarabu tu: Ni heri nisiwe Diwani kuliko kuwa Gamba.Walionyesha kushtuka.Hawakuchelewa kuaga.
Eti WanaJF,nimekosea hapo?