Hello Great Thinkers...

Topic gani hufungwa au kufutwa kabisa JF?
Baadhi ya watu wamekuwa wakijaribu kuupindisha ukweli ndani ya JF na kuanza kuwafanya watumiaji wa JF kudhani kuwa aidha wanaonewa au kuna jambo nyuma ya pazia. Ni wakati muafaka wa kuwafahamisha watumiaji wa JF (wanachama na wasio wanachama) nini hufanywa na moderators na kwa misingi ipi.

Kwanza tuziangalie kanuni/sheria za JF ambazo ndizo hutumika kuwahukumu watumiaji wote (si nje ya hapo!). Mara nyingi tumekuwa tukiwasisitiza wanachama (members) kuwa ni vema wakazisoma sheria hizi kabla ya kuanza kuitumia JF ili hatua flani zinapochukuliwa zisionekane kuwa zimewakandamiza, ni wajibu wetu kama watumiaji wa JF kuanza kuangalia sheria hizi na kupendekeza wapi pafanyike marekebisho na kivipi.

=============
SHERIA NA KANUNI ZA JAMII FORUMS

Tafadhali jiepushe na mambo yafuatayo:


1. Kumvunjia heshima, kumkejeli, kumtukana, mjumbe yeyote.


Wadau wengi wamekuwa wakiivunja kanuni hii ambayo tulikubaliana tangu 2006; haturuhusu kwa namna yoyote iwayo kuvunjiana heshima kwa makusudi wala matusi kwa namna yoyote iwayo. Mfano: Kuandika neno fvck kwa nia ya kukwepa censorship ni kutukana kwa kudhamiria kabisa, tumelishtukia hili na mara inapobainika hoja husika huondolewa na mhusika kufahamishwa juu ya kosa lake, anapothibitika kuendelea kukaidi basi hufungiwa kwa muda au kufutiwa uanachama kabisa!

2. Kuleta katika JAMII FORUMS maelezo yenye maudhui mabaya, au kuweza kuleta maudhi yoyote kwa wajumbe ama kwa wingi wake, ukubwa wake, au mfumo wake.


Hili nalo pia husababisha hoja za watu kufungwa, kufutwa au mhusika kupewa onyo.


3. Kuleta makala au kuendeleza mijadala yenye kuleta ugomvi, uchochezi na yenye muelekeo wa kutengenishana badala ya kuungana miongoni mwa wajumbe wa JAMII FORUMS na Watanzania wote kwa ujumla.


Nadhani maelezo yaliyo juu yanajieleza wazi, natamani wengi wangeelewa maana ya maneno hayo juu! JF si sehemu ya kuanzisha uchochezi aidha wa kidini, kisiasa n.k.

Endapo itabainika umeanzisha hoja kwa nia ya kuibua uchochezi au ugomvi na mtu basi tunasikitika hoja hiyo itakufa HARAKA SANA.

4. Kuleta maongezi binafsi baina ya mwanachama na mwanachama (waliojisajili) waliyoongea kwa kuaminiana kutoka katika Private Messages (PM) au barua pepe (Emails) na kuyaanika hadharani kwa nia ya kuchafuana.


Kuna wadau walikuwa na kawaida ya kuwasiliana na wenzao kwa mapenzi yao wenyewe au hata bila wao kuhitaji, namna pekee ya kuwasilisha PM au email ambayo unaona inaleta tatizo kwako si kuibwaga katika hadhara bali kuituma kwetu na sisi tukaifanyia uchunguzi na kubaini ubovu wa PM wenyewe au Email husika ili mhusika achukuliwe hatua za kinidhamu. Tunalichukulia suala la PM na Emails kuwa private, kulileta hadharani ni kutafuta magomvi na kudhalilishana.


5. Kusambaza kwa makusudi au kwa uzembe barua zenye virusi vya kompyuta.



Kwa bahati hili halijatokea sana JF, threads ambazo zinakuwa zinaonekana kuwa na links ambazo si salama huwa zinaondolewa haraka, aidha waanzishaji wa hoja husika hufahamishwa lakini wakionekana kukaidi hatuna sababu za kuendelea kuwasiliana nao badala ya kuwafungia kwa muda (kutokana na kukaidi) na kisha kuanza kuwa-monitor kadiri siku zinavyokwenda.

6. Kutoa maelezo au shutuma dhidi ya mwanachama mwenzako, kiongozi wa au watu wenye hadhi kijamii bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwa lengo la kuchafua rekodi safi ya mhusika kijamii.


Wahusika mnaovunja sheria hii mnajua athari yake; tunaweza kuwa tunachukizwa na kitu flani kilichofanywa na kiongozi flani ndani ya serikali au kidini, kuanzisha shutma ambazo zinalenga kumchafua mtu bila kuwa na ushahidi ni kutaka kumchafulia jina mhusika. JF si sehemu ya kuchafuliana majina, hatua za kinidhamu huchukuliwa kwa wale wenye nia ya kuitumia JF kwa maslahi yao binafsi.

7. Ni sharti kwa kila mwanachama kutoa maelezo au mchango wake kwa uwazi na ukweli na kutomuogopa yeyote wala kumpendelea yeyote bali kuweka mbele maslahi ya taifa.


Tunaheshimu SANA hoja za kila mmoja, kuna wadau walikuwa wanadhani huenda wao si mali kitu hapa JF, tunatambua kuwa Mwenyezi Mungu katujalia karama tofauti, lakini wakati huohuo tunaamini kila mmoja anaweza kubadilika kadiri siku zinavyokwenda. Hakuna mwanachama wetu ambaye tunamwona "mbabe" dhidi ya wenzake, wote ni sawa mbele zetu na tunawapa heshima sawa.

Hatua za kinidhamu zinaweza kuchukuliwa dhidi ya yeyote yule atakayeshindwa kuzingatia maelezo hayo hapo juu.



Hii si sheria bali ni angalizo tu.
==========================

Other Rules to be noted:


1 - Flaming, Bashing, and Trolling:
Hate posts and personal attacks will not be tolerated on the boards. Treat others on these message boards as you would expect them to treat you. Posting topics specifically designed to provoke a negative response from someone (aka trolling) is also asked to be avoided.




Nadhani nimeigusia hii hapo juu, lakini ni msisitizo zaidi.


2 - Profanity:
Profanity is not tolerated in the board, some words will be censored, also there is to be no name calling, doing so will give you a warning, and then a ban if you continue.




Maelezo ya hapo juu hasa yenye rangi nyekundu hupelekea posts nyingi kuondoshwa na pengine wahusika KUFUNGIWA kwa muda!


3 - Spam:
Purposely spamming a message board with senseless, vacuous, or empty messages to gain a higher post count, or just to annoy others is HIGHLY frowned upon! Commercial spamming and advertising are just as unwelcome unless it is done in the special designed area. Promoting your site is only allowed with permission of the site owners. Bumping old threads is allowed in the request forums, but needless bumps in other forums will be classed as spam.



Niliyoiwekea rangi nyekundu mkuu MS aliianza, mdau mwingine (Shy) naye amekuwa akiweka links kibao kwenye post zake, sharing is caring... Lakini sharing inapofanyika hapa JF ni vema kuweka content husika kisha utoe CREDIT kwa chanzo cha habari, haipendezi kubwaga habari JF bila kuweka chanzo (credit) cha habari. Japo kuna vyombo huchukua habari zetu hapa bila kutu-credit lakini sisi bado tunasisitiza wanachama wetu kuona umuhimu wa kuthamini vyanzo vya habari zetu.

4 - Email & Private Message Spam:
If the members are using the private message facility to spam the others with pointless, unsolicited mail they will be banned. If anyone receives one of these messages, please contact an admin immediately.


Hili tulilisisitiza kuwa endapo litawatokea wanachama basi wawasiliane nasi haraka. Wanaoonekana kutuma malalamiko ni wachache na hatua huchukuliwa.


5 - Piracy, and Warez:
We do not mind discussions about piracy or warez, as long as they are just that...discussions. Linking or giving information about any site that distributes illegal software, or warez, seeking help to circumvent any copyright laws, or encouraging software or media piracy grounds for an immediate ban.



Inajieleza


6 - Impersonating Other Users / Accessing Another User Account:
You may not impersonate another board member or create an account specifically for the purpose of provoking other users. Also, accessing or using someone else's account or attempting to access another poster's account is strictly prohibited. You will be banned.



Mpaka sasa hatujapokea malalamiko ya kuvunjwa kwa sheria hii lakini ipo


7 - Off-Topic Posts:
There is no major punishment for off-topic posters. But lets be honest, it drives us all mad!! If you have something to say but it really has nothing to do with the current thread you are in, please open a new thread for it. Otherwise it will just be deleted and won't solve anything at all.



Wengi wamekuwa wakiivunja hii makusudi kabisa; wanaanzisha salaam ndani ya topic na mods huchukua hatua za kuondoa kila post yenye kuwa nje ya hoja au wanapoona topic imejaa majibizano yasiyo na tija kwa jamii basi topic nzima hufungwa au kuondolewa kabisa. Aidha, kuanzisha mjadala wa kidini sehemu ya siasa wakati kuna jukwaa la dini ni kukosea, mods huhamisha mjadala husika kwenda jukwaa husika wakiwa wameacha redirection na ukibonyeza title ya topic husika utajikuta unaendelea kuisoma katika location mpya.

Ieleweke kuwa kila post ambayo inaondolewa kwenye public domain ipo; zinabaki kwa ushahidi siku za usoni maana wengine hukana kuwa walifanya makosa wanayoambiwa walifanya; hatufuti MOJA KWA MOJA, zinawekwa sehemu kwa ajili ya reference za makosa ya wanachama wetu.


8 - Circumventing a Ban:
If you log onto the forums and receive a message that you have been banned, please submit an unban request and wait for a staff member to get in touch with you. You may NOT re register under a new name if the software lets you. But, if you try to sign up again and we caught you, then it will become a permanent IP Ban. We do NOT send out notices that you have been banned.



Inajieleza wazi tu. "Member flani" kuna kipindi alikosea kulingana na mojawapo ya sheria lakini alipogundua aka-submit unban request nasi tukawasiliana na yule ambaye walikuwa wamekoseana na wakakubaliana kuwa yameisha na akafunguliwa. Tunatambua kuwa wote huwa tunajikuta tumepandwa na jazba na wakati mwingine kutoa kauli ambazo si za kiungwana, uungwana ni vitendo, ukigundua umekosea ukaomba radhi basi utasamehewa!

9 - Nudity / Porn:
Please remember that this board is a PUBLIC forum. There are 12 year olds here just as there are 50 year olds. Nudity and porn is prohibited for obvious reasons.



Inajieleza


10 - Signatures & Avatars:
We do not have any specific set of rules regarding signatures. However, we do ask you that it will not be offensive to others and the length should be within reason. If you desire to have a custom avatar, it must be 100x100 pixels or less. No adult, drug related or racist content please.



Signatures za watu wengine huwa ndefu SANA, au zina maneno yasiyo na heshima kabisa. Huwa tunaziondoa na kumfahamisha mhusika, akionekana kuwa mbishi basi ananyimwa access ya kuwa na signature. Hii pia hujitokeza kwa avatars.

11. Do not post any copyrighted material unless the copyright is owned by you, except for brief credited excerpts to illustrate a point;


Inarejea kulekule, kuwa ni vema unapochukua content kokote haijalishi ni copyrighted au sio copyrighted, basi toa credit ya chanzo cha habari usiibwage as if ni wewe umeandaa hoja husika.

12. You will not post what is commonly called spam, which includes but is not limited to such things as advertisements, chain letters, pyramid schemes, solicitations, or promoting a particular cause or organization. Exceptions may be granted for worthy (in our sole opinion) causes if you obtain prior permission from us;

13. We reserve the right to ban any user temporarily or permanently, refuse posting from screen names we find offensive, edit or delete any post, limit postings on any topic, and shut down any topic altogether, for any reason, or no reason, without explanation or warning.

14. You are solely responsible for the content of your messages. We cannot verify content and thus accept no responsibility for it, nor do we vouch for the accuracy, completeness, or utility, of any message or the qualifications of any user.

15. Do not post private messages at JamiiForums or elsewhere without the express permission of the sender of the Private Message.

16. Do not engage in internet stalking. This includes, but is not limited to, following a JamiiForums member from site to site, or from thread to thread within this site; taking posts from JamiiForums in order to attack a poster at another site; and attempting to defame or discredit JamiiForums members on other sites for views they may have expressed at JamiiForums.


Hizo juu zinajieleza; ingawa nyingine ni kama zinajirudia


17 - Questionable Content:
Since we can't have a rule to cover everything, this is the rule to, well, cover everything. These are public boards, so act like you would if you were in a public place. These issues are left to the discretion of the individual moderators, but may include any material that is knowingly false and or defamatory, misleading, inaccurate, abusive, vulgar, hateful, harassing, obscene, profane, sexually oriented, threatening, invasive of a person's privacy, that otherwise violates any law, or that encourages conduct constituting a criminal offense.


Na hii ndo huwapa mods kazi ngumu, wanajaribu kuzipitia threads kuangalia kama zinastahili kubakia katika public domain au zinavunja yale niliyoonyesha kwa rangi nyekundu hapo juu.... Inakuwa ni mtihani lakini kwa ushirikiano wa members wanaojali basi huzifanyia kazi accordingly.

IELEWEKE KUWA:

JF kamwe haitamsimamia au kumpendelea mtu kwa sababu ya DINI yake au ITIKADI YA KISIASA aliyokuwa nayo.

Tutaendelea kutoa uhuru, hatuwezi kumfungia mtu kwakuwa hupendi anavyopingana na mtizamo wako wa kisiasa au kidini; kama huwezi kujizibizana naye kaa mbali naye.

Hatutamwonea huruma yeyote anayeonekana kutaka kuvunja sheria kwa kisingizio chochote kile; endapo unaona kuna mtu kaenda kombo na sheria hizi usisite kuwasiliana nasi, unaweza kubonyeza CONTACT US ambayo ipo kwenye 'bar' ya bluu hapo juu au hata kutumia barua pepe kwenda support@jamiiforums.com ili hatua za haraka zichukuliwe.

Naamini nimeyajibu maswali ya baadhi ya watu. Topic hii haihusiani na siasa wala uchaguzi lakini kuelekea uchaguzi tunajua wengi watakuwa wanavunja sheria makusudi katika jukwaa hili hivyo tukaonelea vema tuweke bayana haya ili maamuzi yanapochukuliwa wajue ni misingi gani imefuatwa.​
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom