Heligoland-Zanzibar Treaty:The basis For Malawi Claims

Hilo ziwa halina outlet! Linakuwa kila uchao, sehemu za makazi zimezama kwa miaka mm nakua kama 30km hivi
 
Sasa makazi ya zamani mengi yako ziwani ukienda sehemu za matema, inamaanisha malawi wanaexpand territory!
 
Sheria za kimataifa zinasemaje kwenye boarder source maji? Kwa upande wa mto songwe ulikuwa na matatizo hayohayo
 
Mto songwe, miaka ya nyuma watu kila mwaka wanakuwa raia wa nchi tofauti, mpaka miaka ya hivi karibuni wameucomfine!
 
mmmhh 43,44,45..........niko barabara kuu ya kwenda mby tokea iringa :.yanakwenda wapi haya!!au ndo kumekucha
 
Werema hawezi kufanya research thabiti kabla hajafikia conclusion. Mimi nikipewa hiyo kesi nitawabwaga Malawi bila hata kesi kusikilizwa, yaani kesi itakwisha kabla haijaaza. Nitatumia document hizi mbili tu; Heliogland-Zanzibar treaty, na hiyo The British Central Africa Order In Council ya August 1902. The fact kuwa Heligoland treaty ya mwaka 1890 ilikuwa ni temporary agreement, hivyo inakuwa superseded na hiyo Order in council ya mwaka 1902, na kuliacha ziwa halina mwenyewe. Hapo ndipo UNCLOS, RIPARIAN na LITTORAL RIGHTS (kama zilivyoanishwa na Ubungoubungo, na Azipa) zinatumika

Mkuu ningekuwa na kitufe cha like ninge kugongea bahati mbaya na galaxy bonge la point mkuu.
 
Serikali ya Tanzania inalijua hili kwa wazi na mapana yake kwamba hatuna haki hata ye tone moja la maji ya Ziwa Malawi.

Serikali haitakiwi kulifanya jambo hili la kisiasa maana kama ni siasa zako utacheza na wananchi wako lakini unaoweza kuwapiga mabomu ya machozi lakini si kwa watu kama Malawi ambao ni Soveregn state subject to international laws.

Kama kweli Tanzania inataka hata tone moja la Ziwa Nyasa, iachane na porojo za kisiasa na i-file lawsuit for the boundary ili mpaka uwe katikati ya maji kama wengine duniani.

Vinginevyo tutapigizana kelele kama wajinga na hakuna litakalotokea. Tutasubiri Rais wa Malawi tunayechekeana naye anayewapiga mabomu wapinzani wake nchini mwake, sisi tunatumia ziwa lile na kudhani kama ni letu.

Kesho wapinzani wa Malawi waliokuwa wanapigwa mabomu ya mchozi wanakamata nchi, na nyinyi mliokuwa ama mnakaa kimya bila kumkemea anaona mnatumia ziwa lake na si lenu. Kwa nini asilie na nyinyi.

Mimi huyu mama wa Malawi namkubali. Inawezekana anawapa fundisho wote waliomkera akiwa mpinzani wa serikali. Unadhani kwa nini alisema hamtaki Omar Bashir kuja mle.

Mwacheni mama yetu awafundishe adabu wote wanaodhani tutafumbia maonevu ya dunia na ndipo mjue muonewaji akikamata power mjue litakalotokea.

Najua kuna watakaonikejeli kuwa sina uzalendo. Hapa si suala la uzalendo. Baba na mama yangu wakifanya ujambazi wa kumdhulumu jirani yangu siwezi kukaa kimya na kuwatetea kwa kinachoitwa uzalendo. Huo ni wizi.

Nendeni Mahakama za Kimataifa kuwashinda wamalawi na msidhani wa kupelekwa mahakamani ni migomo ya madktari na walimu tu.

Kwa ushauri tu, hiyo hiyo Heligoland Treaty uliyoibandika hapo ungesoma Article VI ndio ungeelewa dai la Tanzania.
 
Read this Heligoland treaty document between German & Great Britain which is the one of the documents used by the Malawi government to argue their case.

hii nchi ni shamba la bibi kila mtu anavuna acha malawi wajichukulie ziwa nyasa, hata kongo wajichukulie tu ziwa tanganyika, kama vipi na nyinyi wakenya msizubae changamkieni mlima kilimanjaro fasta. tz haina mwenyewe ndugu zangu.
 
[/COLOR][/SIZE][/B]

Wewe ndo twambie sasa hiyo convention ya 1982 inasema nini !

inasema kuhusu territorial waters za kila nchi inayopakana na maji..ninachojua ni baharini ambapo ni km 14 nafikiri, hapa ukiingia bila vibali unazamishwa. kwenye maziwa makubwa karibuni kila nchi imegawana na wenzanke kwa sababu siyo practical kua na ziwa na wenzanko wa ufukweni upande wa pili hawatumii hata kukaa beach na kuogelea. Angalia Tanganyika kila nchi imepata share yake, angalia victoria kila nchi imepata share yake, great lakes kule marekani ya kaskazini kila mtu amepata sehemu yake, hata inland sea kama caspian sea/black sea majirani wote wamegawana maeneo..malawi katika hili itakua ndiyo nchi ya pekee kufanya hivi hata kama mikataba ya 19th c iko hivyo na ikawa adopted na OAU 1963, bado haitakua practical kwa tanzania kutotumia kabisa ziwa. lazima ipatikae practical solution na siyo makaratasi na ramani tu.
 
Read this Heligoland treaty document between German & Great Britain which is the one of the documents used by the Malawi government to argue their case.

nchi hii ni shamba la bibi kila mtu anavuna, malawi chukueni ziwa lenu. kisha wakongo nanyi mjiandae kujitwalia ziwa tanganyika. kenya nanyi msizubae kilimanjaro mountain jichukulieni. nchi hii haina mwenyewe ndugu zanguni.
 
Nyerere na Kawawa walijikita kwenye Heligoland treaty ndo maana hawakuwa na msimamo. Mimi ningeomba Tanzania isimamie hizo Riparian rights. Kitendo cha hilo ziwa kupita mpakani kwetu peke yake kinatupa umiliki wa kiasi fulani cha hilo ziwa na huo ndo msimamo wetu tangu enzi za Chief Mhaiki

Nimesoma hiyo British Central Africa kwenye London gazette.pdf. Haijaweka bayana ni wapi mpaka upite zaidi ya kusema West of lake Nyasa @ Kichuguu

Ukisoma Heligoland treaty inaonekana wakoloni hawakuweka umuhimu wa nani mmiliki wa waterbodies ambazo zipo mipakani kwasababu majirani mfano British Central Africa na German East Africa walikuwa wana uwezo wa kutumia hayo maziwa bila kujali mipaka
 
Nikupateje wewe utakuwa mmalawi uliyejibanza hapa kwetu.
Kama ni mtanzania basi utakuwa jinga kabisa. Miaka yote wamalawi walikuwa hawajui kwamba ziwa lote ni la kwao?
Nachojua ni kwamba malawi watake wasitake, wapende wasipende tunagawana pasu kwa pasu ziwa nyasa.
Mwita Maranya kwasababu kosa limekuwa likitendeka kwa muda mrefu hiyo haibadilisha kitendo hicho kutoka kuwa kosa hadi usahihi mpaka hapo taratibu nyinginezo zitakapofanyika...
Hii inabatoa changamoto kwa wanataaluma na viongozi etu kuwa mambo yanapokuwa shwari au yanapokuwa yametulia haimaanishi kuwa ni wakati wa kulala, as long bado wapo katika nafasi na majukumu wanatakiwa kuangalia mbele zaidi ili kuhakikisha mapito yetu yanaendelea kuwa salama, sasa hapa ukiisoma hii treaty ilivyo inawafanya Malawi wawe wazito katika Mizani baina ya Tanzania na wao.
Hawapendi kupitia historia, hawapendi kujisomea, hawapendi changamoto wala hawapendi kufikiri, je unatarajia nini katika hali kama hiyo?
 
Last edited by a moderator:
Kwa ushauri tu, hiyo hiyo Heligoland Treaty uliyoibandika hapo ungesoma Article VI ndio ungeelewa dai la Tanzania.

Na vipi ikitokea upande mmoja ukakataa kufanya majadiliano baada ya kuamini wana haki zote?
 
Mkuu you are referring "Law of the Sea" while here we are discussing "Lake Malawi/Niassa/Nyasa"! Mwisho utakuja kudai EEZ ndani ya Lake Nyassa!! Hiyo UNCLOS Convention is not applicable here! Pia kujenga ports n.k. si kumiliki Lake! Na Wamalawi hata siku moja hawajawazuia kutumia Lake Nyasa for transportation, fishing n.k. Na hata meli yao MV Ilala ilikuwa inatia nanga Itungi port Kyela.
Wao walichofanya ni kutafiti upatikanaji wa gesi ziwani ndio sisi tunakurupuka kuwa Ziwa pia ni letu!!!

Siyo sisi tunaokurupuka kusema kuwa ziwa ni letu. labda wewe ndie ulie kurupuka kusema kuwa ziwa ni letu.kinachoelezwa hapa ni kwamba mpaka uko katikati ya ziwa upande mmoja uko tz na upande mwingine uko malawi.labda km kuna masilahi unayo yapata ndio maana unasema hivyo.km unaona malawi kufanya utafiti wa mafuta na gesi siyo tatizo kwa vile watz hatujakatazwa kutumia ziwa hilo utambuwe kuwa kinachofuata baadae ni kupigwa marufuku kabisa kutumia ziwahilo km hatutalivalia njuga jambo hili.
 
hakuna seriikali ya kutengua maka kwa maneno na mikataba kama kweli wanata nyasa wajaribu kwa nguvu
 
umakini,pia utaalamu ni muhim pia katika suala hili,nashauri pia serikali iwahusishe wasomi wa sheria zq majini katika mada hii
 
Na vipi ikitokea upande mmoja ukakataa kufanya majadiliano baada ya kuamini wana haki zote?

Labda mimi sikuelewa, majadiliano pale siyo ya Tanzania na Malawi! Ni majadiliano ya powers za kikoloni I.e Uingereza na Ujerumani
 
bdo unaweza kuingia Google ukatafuta malawi Map au atlas of Malawi wikimedia au bofya hapo
nashukuru km tunaanza kuelewa pa kuanzia ni wapi na kwanini waMalawi wamepata king katika draft hili
Atlas of Malawi - Wikimedia Commons

Ukwaju, kuna wengine wameishaitwa si WaTZ na si Wazalendo kwa issue hii ya mpaka wa Malawi na TZ, ki ukweli kabisa Malawi wana advantage kuliko sisi (Tz), yaani kinachotakiwa ni kukaa meza moja na watuhurumie tu, ila deal ni lao
 
Kwa ushauri tu, hiyo hiyo Heligoland Treaty uliyoibandika hapo ungesoma Article VI ndio ungeelewa dai la Tanzania.

Na vipi ikitokea upande mmoja ukakataa kufanya majadiliano baada ya kuamini wana haki zote?
 
Back
Top Bottom