Kwa vile sina mahali pengine pa kusemea na kuweza kumpongeza ndugu M. M. Mwanajijiji kwa makala yake aliyoandika kwenye gazeti la Manahalisi la tarehe 9 Desemba 2009 yenye kichwa cha habari "Kikwete amekwishafanya uamuzi mgumu", napenda kutumia fursa hii kumpongeza Mwkjiji kwa kazi ambayo ni muhimu kwa umma katika suala zima la kuwawezesha kifikira (attitude empowerment) kuhusiana na sifa za kiongozi bora. Mwkjj ameweza kuchambua kwa makini juu ya kiongozi bora ni nani, kwamba si yule afanyaye maamuzi magumu bari yule anayefanya maamuzi bora. Vyovyote vile mtu anavyoweza kuita hapa kama anamanisha maamuzi ambayo yako kwa manufaa ya umma ambao ulimuweka madarakani kiongozi husika, basi huo ndiyo uongozi bora aliomaanisa mwkjj.
Sina shaka pia na maana ya maamuzi magunu yaliyotajwa kwenye kongamano la Mwalimu Nyerere bali pia ulimaanisha maamuzi yale yenye maslahi kwa umma isipokuwa wao walitumia neno gumu badala ya bora kwa maana kwamba, kulingana na hulka na kushuka kwa maadili ya watanzania nchini, kufanya maamuzi bora mtu ataonekana kama vile anafanya maamuzi magumu kwao kuyatekeleza yapo ni maamuzi bora na yenye maslahi kwa umma.
Kwa kuwa makala ya Mwkjj inaujumbe kwa umma kuhusiana na sifa za kiongozi bora na wajibu wake kwa waliomchangua, napenda kuwaletea baadhi ya sehemu ya makala yake ili tuweze kujikubusha tuliosoma na tusiosoma tuweze kuupata ujumbea aghalabu kwa kifupi na hatimaye tuchagie ili kupanuana mawazo na uelewa wetu juu ya viongozi ambao watanzania wanatakiwa kuwachagua katika uchaguzi mkuu ujao akiwemo Rais wa nchi, nayo ni kama ifuatavyo:
"Uongozi ni uwezo. Uongozi siyo elimu, uzoefu au umri. Hivi vyote vinaweza kumsaidia kiongozi kuwa kiongozi mzuri. Lakini havimfanyi mtu kuwa kiongozi mzuri au hata kuwa kiongozi.
Hapa hatuna budi kusema wazi kuwa uongozi ni uwezo. Yaani, mtu ambaye anataka kutuongoza ni lazima awe ni yule mwenye uwezo wa kutufanya tuamini kuwa anaweza, ana maslahi yetu moyoni mwake na yuko tayari kusimamia maamuzi yake na kukubali matokeo ya maamuzi hayo.
Kiongozi mzuri siyo yule anayetuahidi nini atatufanyia bali yule ambaye yuko tayari kufanya yale ambayo sisi tunayataka kama wananchi.
Uwezo huu wa kiuongozi unamtofautisha mfuasi na kiongozi. Tangu utoto tumevutiwa na watu ambao wanatuonyesha uwezo wa kutushawishi kukubaliana nao. Kama ilikuwa twende tukacheze mpira au kucheza kombolela, kwenda kucheza ready au kwenda kuruka kamba; kutoroka darasani au kwenda kujisomea!
Wale waliotushawishi utotoni ni hawa tuliwafuata. Wale ambao walikuwa ni washawishi utaona hata baadaye ukubwani wamekuwa ni watu wa ushawishi vile vile na kuongoza wengine (katika mema au mabaya)!
Uwezo huonyeshwa katika maamuzi. Mojawapo ya maneno ambayo tumeyasikia karibuni ni kuwa tunahitaji viongozi wanaoweza kufanya maamuzi magumu.
Tumeyasikia haya kwa sauti zaidi katika kongamano siku chache zilizopita, ambapo baadhi ya watumishi wakongwe wa nchi yetu walipaza sauti zao wakitaka Rais Kikwete kufanya maamuzi magumu na hivyo kuonyesha uongozi. Naomba kutofautiana nao.
Rais Kikwete hahitaji kufanya maamuzi magumu! Ameshayafanya, yanatosha. Si yeye ndiye aliyemteua Andrew Chenge licha ya Chenge huyohuyo kuandamwa na tuhuma za ufisadi katika suala la rada?
Ni Kikwete aliyeruhusu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samwel Sitta, kusulubiwa katika vikao vya chama kiasi cha kutishia utawala wetu wa kikatiba. Ni yeye aliyeliacha Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) linunue dege lile bovu na kujiendesha kwa hasara huku akiendelea kulimwagia mabilioni ya fedha za walipa kodi.
Si yeye na serikali yake waliamua kuwaacha watoto wetu karibu 30 kwenye baridi la Ukraine na kuwalazimisha kuacha masomo ya chuo kikuu kwa kisingizio kuwa serikali haina pesa wakati leo hii wanatuma watu karibu sabini kwenda kwenye mkutano huko majuu wakati yeye na wenzake wakicheza kwenye bembea za Cuba? Wanataka Rais Kikwete afanye maamuzi gani magumu?
Ndugu zangu, uongozi siyo kufanya maamuzi magumu! Uongozi ni kufanya maamuzi bora! Tukitaka kiongozi yeyote ati afanye maamuzi magumu wakati mwingine tunampa ruhusa ya kufanya maamuzi magumu ya nani amridhishe.
Kama uamuzi ni kati ya kuwakamata wahusika wa Kagoda au kuifunua Meremeta na kuwawajibisha wote wahusika na kiongozi akaamua kutofanya lolote kati ya hayo akiamini kuwa huo ni uamuzi mgumu je tutamlaumu?
Uamuzi bora hutanguliwa na misimamo bora: Mojawapo ya mambo ambayo yanamtofautisha kiongozi bora na bora kiongozi ni misimamo aliyonayo. Vitu ambavyo vinanisumbua sana binafsi ninapoangalia watawala wetu ni kuwa misimamo wanayochukua ni ya kusikitisha. Bila ya mtu kujifunza kuchukua misimamo bora mtu huyo hawezi kuchukua maamuzi bora.
Kiongozi ni lazima awe na msimamo wa kuchukia rushwa ili aweze kuchukua maamuzi ya kupigana na rushwa; kiongozi ni lazima awe na msimamo wa kukataa uonevu ili achukue maamuzi ya kutokumuonea mtu.
Misimamo bora hutanguliwa na fikra bora. Hata hivyo, mtu hawezi vile vile kuchukua misimamo bora kama fikra zake na mtiririko wa fikra zake siyo bora. Mtu ambaye hajajifunza kufikiria na kujenga hoja na kuzipima kwa kina atajikuta anachukua misimamo mibovu.
Kama mtu anaamini kuwa wazungu wako mbali na kuwa wazungu siyo mafisadi mtu huyo anapoenda kujadiliana na wazungu hawezi kufikiria kuwa wanamuingiza mkenge!
Hivyo, ili mtu aweze kufikia misimamo bora ni lazima awe na fikra bora ili hatimaye aweze kuchukua maamuzi bora. Nje ya hapo utaona kuwa mtu mwenye fikra za uduni atakuwa na misimamo ya uduni (kama kwenye mikataba) na matokeo yake atachukua maamuzi ya mtu duni.
Ni kwa sababu hiyo, kama taifa na kama wananchi unapokuja uchaguzi huu mkuu ni lazima tuwapime viongozi wetu siyo kwa kile wanachosema bali kila wanachosimamia na hiki kinaonekana kwenye historia zao.
Kiongozi anayeibuka sasa hivi na misaada kwenye jimbo lake na ahadi kibao za nini atafanya ni kiongozi wa kuogopwa. Viongozi bora hawaanzi wakati wa uchaguzi. Ni wananchi wenzetu ambao tumekuwa nao wakituonyesha njia na kutushawishi katika mambo kadhaa hata bila ya wao kuwa na maslahi ya uchaguzi au kuchaguliwa. Hawa ndio viongozi ambao hutambulikana kwa fikra zao, misimamo yao na maamuzi yao bora.
Hawa ndio viongozi ambao ndani ya hizi kumi na mbili tunawahitaji ili kuweza kuanza kuushinda ufisadi na kuanza kujenga misingi ya taifa jipya la kisasa. Vinginevyo, tuwe tayari kupokea bora viongozi."
Heko Mwkjj!!!
Sina shaka pia na maana ya maamuzi magunu yaliyotajwa kwenye kongamano la Mwalimu Nyerere bali pia ulimaanisha maamuzi yale yenye maslahi kwa umma isipokuwa wao walitumia neno gumu badala ya bora kwa maana kwamba, kulingana na hulka na kushuka kwa maadili ya watanzania nchini, kufanya maamuzi bora mtu ataonekana kama vile anafanya maamuzi magumu kwao kuyatekeleza yapo ni maamuzi bora na yenye maslahi kwa umma.
Kwa kuwa makala ya Mwkjj inaujumbe kwa umma kuhusiana na sifa za kiongozi bora na wajibu wake kwa waliomchangua, napenda kuwaletea baadhi ya sehemu ya makala yake ili tuweze kujikubusha tuliosoma na tusiosoma tuweze kuupata ujumbea aghalabu kwa kifupi na hatimaye tuchagie ili kupanuana mawazo na uelewa wetu juu ya viongozi ambao watanzania wanatakiwa kuwachagua katika uchaguzi mkuu ujao akiwemo Rais wa nchi, nayo ni kama ifuatavyo:
"Uongozi ni uwezo. Uongozi siyo elimu, uzoefu au umri. Hivi vyote vinaweza kumsaidia kiongozi kuwa kiongozi mzuri. Lakini havimfanyi mtu kuwa kiongozi mzuri au hata kuwa kiongozi.
Hapa hatuna budi kusema wazi kuwa uongozi ni uwezo. Yaani, mtu ambaye anataka kutuongoza ni lazima awe ni yule mwenye uwezo wa kutufanya tuamini kuwa anaweza, ana maslahi yetu moyoni mwake na yuko tayari kusimamia maamuzi yake na kukubali matokeo ya maamuzi hayo.
Kiongozi mzuri siyo yule anayetuahidi nini atatufanyia bali yule ambaye yuko tayari kufanya yale ambayo sisi tunayataka kama wananchi.
Uwezo huu wa kiuongozi unamtofautisha mfuasi na kiongozi. Tangu utoto tumevutiwa na watu ambao wanatuonyesha uwezo wa kutushawishi kukubaliana nao. Kama ilikuwa twende tukacheze mpira au kucheza kombolela, kwenda kucheza ready au kwenda kuruka kamba; kutoroka darasani au kwenda kujisomea!
Wale waliotushawishi utotoni ni hawa tuliwafuata. Wale ambao walikuwa ni washawishi utaona hata baadaye ukubwani wamekuwa ni watu wa ushawishi vile vile na kuongoza wengine (katika mema au mabaya)!
Uwezo huonyeshwa katika maamuzi. Mojawapo ya maneno ambayo tumeyasikia karibuni ni kuwa tunahitaji viongozi wanaoweza kufanya maamuzi magumu.
Tumeyasikia haya kwa sauti zaidi katika kongamano siku chache zilizopita, ambapo baadhi ya watumishi wakongwe wa nchi yetu walipaza sauti zao wakitaka Rais Kikwete kufanya maamuzi magumu na hivyo kuonyesha uongozi. Naomba kutofautiana nao.
Rais Kikwete hahitaji kufanya maamuzi magumu! Ameshayafanya, yanatosha. Si yeye ndiye aliyemteua Andrew Chenge licha ya Chenge huyohuyo kuandamwa na tuhuma za ufisadi katika suala la rada?
Ni Kikwete aliyeruhusu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samwel Sitta, kusulubiwa katika vikao vya chama kiasi cha kutishia utawala wetu wa kikatiba. Ni yeye aliyeliacha Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) linunue dege lile bovu na kujiendesha kwa hasara huku akiendelea kulimwagia mabilioni ya fedha za walipa kodi.
Si yeye na serikali yake waliamua kuwaacha watoto wetu karibu 30 kwenye baridi la Ukraine na kuwalazimisha kuacha masomo ya chuo kikuu kwa kisingizio kuwa serikali haina pesa wakati leo hii wanatuma watu karibu sabini kwenda kwenye mkutano huko majuu wakati yeye na wenzake wakicheza kwenye bembea za Cuba? Wanataka Rais Kikwete afanye maamuzi gani magumu?
Ndugu zangu, uongozi siyo kufanya maamuzi magumu! Uongozi ni kufanya maamuzi bora! Tukitaka kiongozi yeyote ati afanye maamuzi magumu wakati mwingine tunampa ruhusa ya kufanya maamuzi magumu ya nani amridhishe.
Kama uamuzi ni kati ya kuwakamata wahusika wa Kagoda au kuifunua Meremeta na kuwawajibisha wote wahusika na kiongozi akaamua kutofanya lolote kati ya hayo akiamini kuwa huo ni uamuzi mgumu je tutamlaumu?
Uamuzi bora hutanguliwa na misimamo bora: Mojawapo ya mambo ambayo yanamtofautisha kiongozi bora na bora kiongozi ni misimamo aliyonayo. Vitu ambavyo vinanisumbua sana binafsi ninapoangalia watawala wetu ni kuwa misimamo wanayochukua ni ya kusikitisha. Bila ya mtu kujifunza kuchukua misimamo bora mtu huyo hawezi kuchukua maamuzi bora.
Kiongozi ni lazima awe na msimamo wa kuchukia rushwa ili aweze kuchukua maamuzi ya kupigana na rushwa; kiongozi ni lazima awe na msimamo wa kukataa uonevu ili achukue maamuzi ya kutokumuonea mtu.
Misimamo bora hutanguliwa na fikra bora. Hata hivyo, mtu hawezi vile vile kuchukua misimamo bora kama fikra zake na mtiririko wa fikra zake siyo bora. Mtu ambaye hajajifunza kufikiria na kujenga hoja na kuzipima kwa kina atajikuta anachukua misimamo mibovu.
Kama mtu anaamini kuwa wazungu wako mbali na kuwa wazungu siyo mafisadi mtu huyo anapoenda kujadiliana na wazungu hawezi kufikiria kuwa wanamuingiza mkenge!
Hivyo, ili mtu aweze kufikia misimamo bora ni lazima awe na fikra bora ili hatimaye aweze kuchukua maamuzi bora. Nje ya hapo utaona kuwa mtu mwenye fikra za uduni atakuwa na misimamo ya uduni (kama kwenye mikataba) na matokeo yake atachukua maamuzi ya mtu duni.
Ni kwa sababu hiyo, kama taifa na kama wananchi unapokuja uchaguzi huu mkuu ni lazima tuwapime viongozi wetu siyo kwa kile wanachosema bali kila wanachosimamia na hiki kinaonekana kwenye historia zao.
Kiongozi anayeibuka sasa hivi na misaada kwenye jimbo lake na ahadi kibao za nini atafanya ni kiongozi wa kuogopwa. Viongozi bora hawaanzi wakati wa uchaguzi. Ni wananchi wenzetu ambao tumekuwa nao wakituonyesha njia na kutushawishi katika mambo kadhaa hata bila ya wao kuwa na maslahi ya uchaguzi au kuchaguliwa. Hawa ndio viongozi ambao hutambulikana kwa fikra zao, misimamo yao na maamuzi yao bora.
Hawa ndio viongozi ambao ndani ya hizi kumi na mbili tunawahitaji ili kuweza kuanza kuushinda ufisadi na kuanza kujenga misingi ya taifa jipya la kisasa. Vinginevyo, tuwe tayari kupokea bora viongozi."
Heko Mwkjj!!!