Hekaya za Abunwasi....zinakutufunza nini wa-TZ?

Mpasuajipu

JF-Expert Member
Oct 22, 2010
836
49
Katika mwaka mmoja, Abunuwasi aliamua kuwa mfugaji mbuzi. Alinunua mbuzi na akanza kufuga na huku akiwa na tamaa ya kumuongezea kipato chake pindi tu mbuzi huyo atapoanza kuzaa watoto, naye atawafuga hadi wawe wengi na kuwa tajiri mji mzima kwa mbuzi wake hao.
Siku moja Abunuasi akipokuwa anampeleka malishoni mbuzi wake njiani alikikuta kiatu kimoja kizuri sana kati kati ya njia. Alisimama na akakingalia na kilimpendeza na alisema "kiatu hiki ni kizuri lakini mbona kipo kimoja tu" alitafuta kiatu chengine pembezoni mwa ile njia hakukiona. Akaona hakina maana kukichukua kwani hawezi kuvaa kiatu kimoja.
Abunuasi akachukuwa mbuzi wake na akakiwacha kile kiatu pale pale. Aliposonga mbele kidogo akakikuta kiatu chengine kama kile ambacho kilikuwa ni cha mguu mwengine wa kile cha mwanzo. Abunuasi alishangaa na akaona bora angelikichukua kile cha mwanzo na kwa sasa vingelikuwa tayari vishatimia pea moja. Ndipo alipoamua kumfunga mbuzi wake pembeni ya njia na akakiweka kiatu kile pale pale alipomfunga mbuzi ili arudi akakichukuwe kiatu kile cha mwanzo.
Aliporudi pale kilipokuwepo kiatu cha mwanzo hakukikuta tena kiatu kile, alijaribu kukitafuta lakini hakukiona. Basi akaona kuwa ametokea mtu amekiokota. Akarudi haraka alipomfunga mbuzi wake. Nako pia hakumkuta mbuzi wala kile kiatu kimoja. Ikawa amemkosa mbuzi na pia viatu hakuvikuta, Abunuasi ndoto zake zote za utajiri ziliruka na akabaki na umasikini wake kwa ubaya wa tamaa zake.

Hapo nilipiga mstari: Mafisadi inabidi tuwadhibiti sasa, la sivyo tukisema tutawarudia baadaye tutakosa kila kitu!
 
"Zinakutufunza" ndo kitu gani? Au ni moja Kati ya misamiati mipya iliyoundwa karibuni pamoja na mkukuta, mkurabita, umitashumta, nk?
 
Hivi abunuwasi alikuwa raia wa wapi?

ABUNUWASI alikua RAIA wa MESEPOTANIA...ambayo vijana waleo hawataijua kamwe kwani sasa inajulika kama IRAQ Kwa zamani kabla ya BC..dunia ilikua ina ma bara ma tatu 3..tu ndio yalikua yanajulikana nayo ni UYUNANI ..greec...UAJEMI...iran..na METHEPOTANIA ...IRAQ
 
huu uzi umejirudia!

Katika
mwaka mmoja, Abunuwasi aliamua kuwa mfugaji mbuzi. Alinunua mbuzi na
akanza kufuga na huku akiwa na tamaa ya kumuongezea kipato chake pindi
tu mbuzi huyo atapoanza kuzaa watoto, naye atawafuga hadi wawe wengi na
kuwa tajiri mji mzima kwa mbuzi wake hao.

Siku moja Abunuasi akipokuwa anampeleka malishoni mbuzi
wake njiani alikikuta kiatu kimoja kizuri sana kati kati ya njia.
Alisimama na akakingalia na kilimpendeza na alisema "kiatu hiki ni
kizuri lakini mbona kipo kimoja tu" alitafuta kiatu chengine pembezoni
mwa ile njia hakukiona. Akaona hakina maana kukichukua kwani hawezi
kuvaa kiatu kimoja.

Abunuasi akachukuwa mbuzi wake na akakiwacha kile kiatu
pale pale. Aliposonga mbele kidogo akakikuta kiatu chengine kama kile
ambacho kilikuwa ni cha mguu mwengine wa kile cha mwanzo. Abunuasi
alishangaa na akaona bora angelikichukua kile cha mwanzo na kwa sasa
vingelikuwa tayari vishatimia pea moja. Ndipo alipoamua kumfunga mbuzi
wake pembeni ya njia na akakiweka kiatu kile pale pale alipomfunga mbuzi
ili arudi akakichukuwe kiatu kile cha mwanzo.

Aliporudi pale kilipokuwepo kiatu cha mwanzo hakukikuta
tena kiatu kile, alijaribu kukitafuta lakini hakukiona. Basi akaona kuwa
ametokea mtu amekiokota. Akarudi haraka alipomfunga mbuzi wake. Nako
pia hakumkuta mbuzi wala kile kiatu kimoja. Ikawa amemkosa mbuzi
na pia viatu hakuvikuta,
Abunuasi ndoto zake zote za utajiri
ziliruka na akabaki na umasikini wake kwa ubaya wa tamaa zake.


Hapo nilipiga mstari: Mafisadi inabidi tuwadhibiti sasa, la sivyo
tukisema tutawarudia baadaye tutakosa kila kitu!
 
Back
Top Bottom