Hekaheka za wakimbizi na usalama wa raia waishio mipakani!

RC.

JF-Expert Member
May 24, 2012
444
41
Ama kweli wema usizidi uwezo;msemo huu nilipokuwa nikiusikia nilifikiri wanaoutumia msemo huu either walikuwa hawawatakii mema wenzao,lkn nimeona ni ukweli mtupu,watu hawa(wakimbizi)kwa muda sasa wamekuwa wakiripotiwa kuua wenyeji wao bila huruma,wamekuwa wakiweka sumu kwenye mizoga ya wanyamapori na kuua wanyama walao nyama kama simba,chui,fisi,tai na wengineo na kupelekea nchi yetu kupoteza rasilimali hii adimu inayotuletea fedha za kigeni,wamekuwa wakiharibu mazingira kwa kukata miti hovyo, huku wakigoma kurudi makwao kwa visingizio vya kuwa kwao kuna vita,sasa najiuliza maswali mengi ambayo sijapata majibu sahihi,1;ni kwanini watu hawa wanatuua huku wako kwetu na vyombo vya usalama vimekaa kimya?,2;hivi ni lazima kuendelea kuwa na wakimbizi wasio na shukrani katika nchi yetu? kwa kutaja machache.ukienda kigoma na ukanda mzima wa maziwa makuu utawakuta wageni hawa wanafanya shughuli mbalimbali kama uvuvi,na biashara,watu hawa wamekuwa wakiwapiga na hata kuwauwa watanzania wenyeji wa maeneo hayo na kufanya matukio ya kijambazi kwa kukata watu mikono yao maarufu kama ''kaoshi''hakuna lolote linalofanyika kuwafikisha kwenye mamlaka husika,je tuwafanyeje watu hawa? imefika wakati watanzania wamekuwa kama wamkimbizi ndani ya nchi yao.sasa ndugu watanzania wenzangu tuwafanyeje watu hawa wasio na shukrani?...naomba kuwasilisha.
 
Angalia kwanza sheria za Umoja wa mataifa zinasemaje kuhusiana na wakimbizi, inakueje wewe uje ulalamike tu kwamba wakimbizi wanaoua wanyama, wanakata miti na pia ni majambazi? Hivi unaamini kuwa wakimbizi hawa wakiondoka vitendo hivi vitakuwa vimekomeshwa Tanzania. Wakimbizi wapo mkoa wa Kigoma na mkoa wa Rukwa ndo kuna makambi ya wakimbizi. Sasa nakuuliza sehemu zingine za Tanzania ambako kuna vitendo vya naman hii nako vimesababishwa na wakimbizi?

Kila siku matukio ya ujambazi yanaripotiwa mkoa wa Kigoma, sasa naomba kuuliza wanaokamatwa na kufungwa ni wakimbizi au hata raia wa mikoa jirani? Mi nadhani kama mkimbizi amegoma kurudi nyumbani kwake kwa kuhofia usalama wake, nchi husika inatakiwa kimtafutia hifadhi kwenye nchi nyingine ya pili in case kama watakuwa wamechoshwa na uwepo wake.Lakini kumrudisha mkimbizi nyumbani kwake wakati yeye hapendi ni kinyume na mkataba wa wakimbizi wa umoja wa mataifa
 
Back
Top Bottom