Hebu tukumbushie tuliozaliwa miaka ya sabini na....

Wana jf naomba tukumbushane kwa wale tuliokuwepo enzi hizo, na kwa faida ya wanetu wa sasa, kinachonifanya nisisahau kikubwa kuliko vyote
kuna kanga zilikuwa zinaitwa teleza za polister nilikuwa nimembebea mdogo wangu nikaenda kisimani wakati najitwisha ndoo nguo ikafunguka mtoto akatumbukia kisimani, kingine
vita vya amini,
kukamatwa kwa jua,
Unga wa yanga
Wenzangu mnakumbuka nini?

1.Unga wa yanga
2.Sabuni ya mawingu
3.Kitambaa cha madurufu a.k.a MAFAFA
Vitenge vyaMawingu a.k.a BATIK
Maduka ya NMC na RTC,Ukitaka SEMBE LA YANGA kg1 UNALAZIMISHWA KUNUNUA NA PAKET YA SIGARA hata kama SI MVUTAJI.
au Sukari kg 1 na BETRI 4,hata kama REDIO HUNA.
 
Safari na muziki. basi lenye spika nauli juu. halafu yakaja mabasi yenye pazia.
Basi likiwa na rangi nyingi linaitwa luxury.
Arusha hadi Dar siku mbili, au zaidi ikinyesha.
Una book Kamata au Relwe, wiki mbili kabla ya safari na rushwa juu.
Ni lazima basi liharibike njiani.
Madereva wa mabasi ni mibaba minene, sijui kwa nini.
mnaweza safiri masaa matatu barabarani bila kupishana na gari jingine.
nakumbuka watu wakisafiri na sufuria za kupikia njiani.
still, hizo zinaonekana kuwa siku njema ukifananisha na sasa
 
mi nakumbuka shuleni tulikuwaga na chawa sana! Hivi wale wadudu bado wapo kweli? Siku nyingi cjawaona.
 
nakumbuka nilikuwa mwanza kipindi hiko maeneo ya bugando then tukapata taarifa kuwa idi amin atapiga maeneo yale tulihahaje??
Vita mbaya sana asikwambie mtu
 
Unakumbuka enzi zile jangwani kulikua poli simba nje nje,nyumba zilikua zinaishia lumumba tu pale sisiemu!

Mazee wewe unaongea 30's au seventies? Unapajua Mwembetogwa wewe? Magomeni mbona kina Nyerere wamekaa zamani sana kabla ya seventies? kabla hata ya uhuru?

Mie nakumbuka wanajeshi wakipiga mchakamchaka kwenda kumpiga Amini.

Nakumbuka ziara za Makamu wa Rais Aboud Jumbe Mwinyi.

Nakumbuka mabasi ya KAMATA na karibu kila mkoa na wilaya nyingi zilikuwa na kampuni zake za mabasi.

Nakumbuka ukienda mjini Dar watu wachache sana (early eighties)

Nakumbuka Nyerere anatoa shahada za UDSM (early eighties)

Nakumbuka televisheni ya kwanza mtaani (early eighties)

Nakumbuka "machafuko ya hali ya hewa Zanzibar" na "Miezi kumi na nane ya kujifunga mkanda" (early eighties)

Nakumbuka Hemed Maneti singing "Ally Mwinyi, Ally Mwinyi, Ndiyo Ndiyo, Ndiyo" 1985.
 
mimi nakumbuka enzi za zamani mnazi mmoja palikuwa panaitwa Mguu wa simba mwene! nawakumbuka wauza uzuri! nakumbuka Judo pale ferry na watemi wa judo akina makwasu kwasu!nawakumbuka vijana watemi wa Dar: Pale Ilala quartes alikuwa Chale cheusi, kariakoo alikuwa Ingama, Ilala bungoni alikuwa kibunda list! kweli vijana wengi wa Dar walikuwa wanaishi maisha ya western europe kupita kiasi. halafu sinema moja ilikuwa inaitwa seven Dollas to kill. hii iliwachochea vijana wengi sana kupigana mitaani halafu watu mnashabikia kulaa, kulaaa, kulaaa kula eeeenh!!!!!!!!!!!!!!!!!! halafu mtu ukipigwa watu wanaita kubotwa! utasikia fukani kabotwa leo!
 
Club raha leo shooooooow! umenikumbusha mbali mkuu, radio tz enzi hizo ilikuwa na vipi vya kuelimisha kibao, nakumbuka kile kipindi cha radio tanzania shuleni, walimu walikuwa wanaingia na redio darasani, mnasikiliza wee baada ya hapo maswali ole wako ushindwe kujibu, inaamanisha ulikuwa unacheza hukuwa unasiliza na enzi zile fimbo zilikuwa njenje tu

Maduka ya ushirika kama kitabu hakijasainiwa na balozi no unga no sukari

Nakumbuka pia, ujambazi ulikuwa umeshika kasi sana wakati huo, ikifika saa moja hakuna mtu barabarani, unasikia tangazo zimeni taa wakubwa wapite, majambazi wanapita zao ole wako waone taa inawaka kwenye nyumba utaona risasi tu inapenya kama si dirishani basi kwenye mlango

zama za club la leo shooooooooooooooooooooooooo haikuwa enzi izo kweli
Ila nina hamu na buluga!
Wapi maduka ya ushirika mnaenda kwa jina la dingi kuchukua sukari kwa foleni unaweka jiwe gari likaribia tuu unaitwa
 
Duh nguo zilikuwa sare kama mashati ya katale, Juliana, bendi ya masantula, sinema ya yomba yomba, wahaini walivyotaka kupindua nchi, aboud jumbe alivyofungwa kisiasa hehee kubwa kuliko wanaume walikuwa wanatongoza kwa barua maneno meeeeengi unakumbuka walikuwa wanaandikaje
 
mi nakumbuka shuleni tulikuwaga na chawa sana! Hivi wale wadudu bado wapo kweli? Siku nyingi cjawaona.
Umesahau maharage yenye wadudu weusi na ugali wa dona funza kibao ukikataa kula siku tatu kwenu
 
mimi nakumbuka enzi za zamani mnazi mmoja palikuwa panaitwa Mguu wa simba mwene! nawakumbuka wauza uzuri! nakumbuka Judo pale ferry na watemi wa judo akina makwasu kwasu!nawakumbuka vijana watemi wa Dar: Pale Ilala quartes alikuwa Chale cheusi, kariakoo alikuwa Ingama, Ilala bungoni alikuwa kibunda list! kweli vijana wengi wa Dar walikuwa wanaishi maisha ya western europe kupita kiasi. halafu sinema moja ilikuwa inaitwa seven Dollas to kill. hii iliwachochea vijana wengi sana kupigana mitaani halafu watu mnashabikia kulaa, kulaaa, kulaaa kula eeeenh!!!!!!!!!!!!!!!!!! halafu mtu ukipigwa watu wanaita kubotwa! utasikia fukani kabotwa leo!

Duh! Mkuu umenikumbusha huyu mbabe, alitutesa sana sisi tuliokuwa tunakaa maflatini! Kulikuwa na mwingine akiitwa Zongo, unamkumbuka?
 
Enzi ya libert sinema mwanza kulikuwa na mbabe anaitwa shaft pamoja na alshas disco.
enzi za breakdancer ilikuwa kiboko...nakumbuka enzi za usafiri mlima sekenge shelui tumekaa pale siku nne magari yamekwama
 
familia yangu tulikuwa na unga wa kutosha... Ila nikienda kwa jirani na kukuta unga wa manjano,nilikuwa naitamani,na nauona ndiyo mzuri kwa rangi yake..
Nilielimishwa kuwa sisi ndiyo tuna unga mzuri,wala sikuelewa,hadi walipoupika nyumbani..!

Nakumbuka majumba yote ya Cinema(hakuna hata moja sikuwahi kuingia)!

Foleni ya duka la kaya kwa mzee Chaurembo(mi wa K'koo)

hata UDA kulikuwa na la sh 4,na la nafuu ni la sh 3..nalo liliitwa la kaya! Tiketi zake zinakatwa kwa mashine,kupanda mlango wa nyuma kushuka mlango wa mbele..

Halafu ilikuwa ukitembelea nyumba,maghorofa waliyokuwa wanakaa Wahindi,utajua tu,kwani kulikuwa na harufu ya tofauti,na mbaya! Tofauti na sasa!

Nakumbuka kuacha begi langu ndani ya basi saa 6 mchana,likaletwa nyumbani jioni na Auntie yangu...! Akasema lilikuwa limetundikwa naye alipotazama,akaona vitu vyangu!

Kuokota wadudu aina ya senene katika barabara ya Msimbazi,usiku wa saa 3,magari yanakuwa hakuna,na mataa ya barabarani yote yanakuwa yamewashwa! Hata wazazi wanaruhusu watoto kuokota,usalama wa barabara usiku ulikuwa wa kutosha..
 
RUDI NCHI YANGU TANZANIA...NAKUPENDAYE SANA....NIKUPENDAYE KWA MOYO WANGU WOTE:

"UDA kulikuwa na la sh 4,na la nafuu ni la sh 3..nalo liliitwa la kaya! Tiketi zake zinakatwa kwa mashine,kupanda mlango wa nyuma kushuka mlango wa mbele.... Nakumbuka kuacha begi langu ndani ya basi saa 6 mchana,likaletwa nyumbani jioni na Auntie yangu...! Akasema lilikuwa limetundikwa naye alipotazama,akaona vitu vyangu!

Kuokota wadudu aina ya senene katika barabara ya Msimbazi,usiku wa saa 3,magari yanakuwa hakuna,na mataa ya barabarani yote yanakuwa yamewashwa! Hata wazazi wanaruhusu watoto kuokota,usalama wa barabara usiku ulikuwa wa kutosha....



familia yangu tulikuwa na unga wa kutosha... Ila nikienda kwa jirani na kukuta unga wa manjano,nilikuwa naitamani,na nauona ndiyo mzuri kwa rangi yake..
Nilielimishwa kuwa sisi ndiyo tuna unga mzuri,wala sikuelewa,hadi walipoupika nyumbani..!

Nakumbuka majumba yote ya Cinema(hakuna hata moja sikuwahi kuingia)!

Foleni ya duka la kaya kwa mzee Chaurembo(mi wa K'koo)

hata UDA kulikuwa na la sh 4,na la nafuu ni la sh 3..nalo liliitwa la kaya! Tiketi zake zinakatwa kwa mashine,kupanda mlango wa nyuma kushuka mlango wa mbele..

Halafu ilikuwa ukitembelea nyumba,maghorofa waliyokuwa wanakaa Wahindi,utajua tu,kwani kulikuwa na harufu ya tofauti,na mbaya! Tofauti na sasa!

Nakumbuka kuacha begi langu ndani ya basi saa 6 mchana,likaletwa nyumbani jioni na Auntie yangu...! Akasema lilikuwa limetundikwa naye alipotazama,akaona vitu vyangu!

Kuokota wadudu aina ya senene katika barabara ya Msimbazi,usiku wa saa 3,magari yanakuwa hakuna,na mataa ya barabarani yote yanakuwa yamewashwa! Hata wazazi wanaruhusu watoto kuokota,usalama wa barabara usiku ulikuwa wa kutosha..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom