Hebu soma hapa!!

Eiyer

JF-Expert Member
Apr 17, 2011
28,258
20,709
Tangu tumezaliwa tumesikia neno UPENDO,mimi binafsi wazazi wala shule sikuwahi kuambiwa maana ya hili neno!Nilikuja kulitafuta mwenyewe!Nakumbuka kwenye mafundisho ya dini tulikua tunaambiwa tupendane,nyumbani hivyohivyo.Nilipokua nikajua kuna kumpenda mwanamke,hawa walionieleza kuhusu upendo hawakuwahi kunifafanulia,nikajiuliza kuna tofauti kati ya kumpenda mama yangu na jirani yangu pia vipi kuhusu mwanamke?Nilibaki mtupu!Lakini niliamua kutafuta maana na nimepata tafsiri hii;Upendo ni kumkubali mtu bila masharti.Yaani kama ni mwanao sio mpaka afaulu mtihani ndo apendwe,kama ni jirani rio mpaka awe na pesa ndo apendwe,upendo ni kutoa tu bila kujali unaempenda anakurudishia nini,yaani wewe ni kutoa tu,na ukiwa hivi hautaona shida kuishi na mke/mume mkorofi.ANGALIZO,kwenye ndoa ni hatari kuishi na mtu mwenye tabia za hatari kama kupiga,kufuja,kudhalilisha n.k,hapa unatakiwa usitishe haya mahusiano,kufanya hivi haimaanishi unamchukia.Unaweza ukatengana nae lakini mkawa pamoja kwenye mambo mengine.Sasa kama niko sahihi,kuna upendo siku hizi?Na kama siko sahihi,tafsiri yako ni muhimu hapa,tuambie......
 
Upendo upo sana siku hizi tena bwerere
wewe tu na roho yako.
OTIS
 
Tangu tumezaliwa tumesikia neno UPENDO,mimi binafsi wazazi wala shule sikuwahi kuambiwa maana ya hili neno!Nilikuja kulitafuta mwenyewe!Nakumbuka kwenye mafundisho ya dini tulikua tunaambiwa tupendane,nyumbani hivyohivyo.Nilipokua nikajua kuna kumpenda mwanamke,hawa walionieleza kuhusu upendo hawakuwahi kunifafanulia,nikajiuliza kuna tofauti kati ya kumpenda mama yangu na jirani yangu pia vipi kuhusu mwanamke?Nilibaki mtupu!Lakini niliamua kutafuta maana na nimepata tafsiri hii;Upendo ni kumkubali mtu bila masharti.Yaani kama ni mwanao sio mpaka afaulu mtihani ndo apendwe,kama ni jirani rio mpaka awe na pesa ndo apendwe,upendo ni kutoa tu bila kujali unaempenda anakurudishia nini,yaani wewe ni kutoa tu,na ukiwa hivi hautaona shida kuishi na mke/mume mkorofi.ANGALIZO,kwenye ndoa ni hatari kuishi na mtu mwenye tabia za hatari kama kupiga,kufuja,kudhalilisha n.k,hapa unatakiwa usitishe haya mahusiano,kufanya hivi haimaanishi unamchukia.Unaweza ukatengana nae lakini mkawa pamoja kwenye mambo mengine.Sasa kama niko sahihi,kuna upendo siku hizi?Na kama siko sahihi,tafsiri yako ni muhimu hapa,tuambie......
Ahsante mwalimu, kwa darasa hili maridhawa la Upendo............... Sina cha kuongeza, umemaliza mkuu
 
Ahsante mwalimu, kwa darasa hili maridhawa la Upendo............... Sina cha kuongeza, umemaliza mkuu

Thanx Mtambuzi!Inaonekana tafsiri zetu zinafanana,je upo huo upendo now days?
 
Upendo... Daima huja na huwa ni wa kweli na hauna mpaka.... Dini wala jamii haisemi kua mpende mtu ambae atakufurahisha tu. Hakuna kitu ambacho ni kugumu kufuata katika maisha kama kua na upendo consistent.... Upendo huwepo haijalishi huyo mtu ni mbaya, ana tabia za ovyo ama ana roho mbaya. Kuweza pass all that na ukampenda bado, ndio Upendo hasa wa kweli na ambao hasa kila mwanadamu anatakiwa kua nayo... However because we are human roho zetu zimeumbwa kwa nyama, upendo mara nyingi hujegwa na matendo ya umpendae..... Waweza mpenda mtu, awe mume, mzazi, mtoto ama mwanadamu yoyote yule, ila in the long run upendo ukashuka na kupungua juu ya huyo mwanadamu bila kutarajia.... wala bila kupenda.
 
Hahahaaa,Mtambuzi kumbe OTIS anazungumzia ule wa kwenye tamthilia za Kifilipino na Latin Amerikaeee!"I Love u more than myself"wizi mtupu!
 
Dada Asha,u hali gani?,.....Upendo halisi haushuki wala hauishi,unaoisha ni ule upendo wa "kutegemea something in return"it means kwamba kama hujanifanyia hiki au kile sitakupenda,huu ni upendo wa masharti,na pia sio upendo!Tena hali hii kwenye uhusiano ndo kubwa,kiukweli hii ni mihemko ambayo hukujia baada ya mtu kukutendea jambo fulani au mtu kuwa na mtazamo/muonekano fulani[makalio,miguu ya bia,sauti,mrefu,mtanashati n.k]mihemko inayotokana na hali hizi huisha pale unapokinai kilichokuvuta au kinapotoweka!Upendo hauna masharti haya,haujali kama unarudisha matusi,au chuchu saa sita zimelala baada ya kunyonywa na mtoto.Mwenye upendo anaangalia ubinadamu tu.
 
Dada Asha,u hali gani?,.....Upendo halisi haushuki wala hauishi,unaoisha ni ule upendo wa "kutegemea something in return"it means kwamba kama hujanifanyia hiki au kile sitakupenda,huu ni upendo wa masharti,na pia sio upendo!Tena hali hii kwenye uhusiano ndo kubwa,kiukweli hii ni mihemko ambayo hukujia baada ya mtu kukutendea jambo fulani au mtu kuwa na mtazamo/muonekano fulani[makalio,miguu ya bia,sauti,mrefu,mtanashati n.k]mihemko inayotokana na hali hizi huisha pale unapokinai kilichokuvuta au kinapotoweka!Upendo hauna masharti haya,haujali kama unarudisha matusi,au chuchu saa sita zimelala baada ya kunyonywa na mtoto.Mwenye upendo anaangalia ubinadamu tu.

mmh this z so true, uko njema leo eiyer naona toka uko juu unamwaga mapoint 2 duh.
congratzz.
 
Upendo ni kujipenda wewe tu hakuna kingine-mimi sijawahi kuona mtu anampenda mtu mwingine zaidi yake.
 
mkuu habari ya masiku? Vp sikukuu?

Nzuri mkuu,sikuku ilikua njema ila tulipika pilau akaja kibaka akapita na sufuria lote ikabidi tupike UGALI!Si unajua nyumba zetu za uswazi jiko ni nje ya chumba chako...Lol!
 
Upendo ni kumkubali mtu bila masharti.
ANGALIZO, kwenye ndoa ni hatari kuishi na mtu mwenye tabia za hatari kama kupiga,kufuja,kudhalilisha n.k,hapa unatakiwa usitishe haya mahusiano,kufanya hivi haimaanishi unamchukia.

.....Upendo halisi haushuki wala hauishi,unaoisha ni ule upendo wa "kutegemea something in return"it means kwamba kama hujanifanyia hiki au kile sitakupenda.
Kama tutaangalia kwenye dondoo hizi mbili, kuna mambo yanachanganya - kumpenda mtu bila masharti na upendo wa kutegemmea something in return". Nahisi tusijidanganye, mwenye tabia chafu hapendeki (kama zilizotajwa hapo juu kwenye ndoa, au kwa rafiki mwongo, virungu, mbea, mchonganishi n.k, au mtoto mwizi, mwivu, mlevi n.k.) Anayependa katika mahusiano yoyote, iwe baina ya wapenzi, rafiki au familia, hutegemea kurejeshewa upendo, ikiwa atachokuwa anavuna ni maudhi na maumivu upendo hupungua na pengine huisha kabisa.
Sumu ya upendo/mapenzi ni maudhi.
 
Back
Top Bottom