LD
JF-Expert Member
- Aug 19, 2010
- 3,014
- 574
Mwenzenu nilivunjwa moyo miaka miwili iliyopita, Tangu moyo ulivyovunjika nimekuwa nikimuomba Mungu aniponye na nina Imani ameniponya kabisa, manake najiona sina kinyongo, wala uchungu na huyo heart breaker, na ninachomshukuru Mungu zaidi nina furaha na Amani, na maisha yanaendelea vizuri.
Pamoja na hivo ninamshukuru Mungu kwa sababu amenisamehe dhambi niliyokuwa nimeitenda, kwa sababu nilijidai ninampenda sana huyo mtu kuliko hata Mungu, nikampa vyote, nafsi, roho na mwili. Wakati mwingine hata muda wa kwenda kuabudu ulipungua kwa kumpa huyo heart breaker muda mwingi zaidi.
Baada ya tukio hilo,niliamua kujipa likizo ya kumpenda mwanaume, yani nikaziba madirisha yote ya kumkaribisha mwanaume moyoni mwangu.
Siwachukii lakini nimejipa likizo kwa muda wa miaka mitano hivi, na sasa huu ni mwaka wa pili, ina maana bado miaka mitatu.
Je uamuzi wangu wa kujipa likizo ni sahihi?
Najiona ninaweza kuendelea na likizo hadi miaka mitatu iliyobakia iishe, je ni kweli au
naidanganya nafsi yangu.
Angalizo Marufuku kunitania Broken Heart!! Umesikia GY, Asprin, TF, Askofu na Teamo T, bila kumsahau Bigirita. Mjukuu mtiifu umesikia!! na wewe St. RR.
Pamoja na hivo ninamshukuru Mungu kwa sababu amenisamehe dhambi niliyokuwa nimeitenda, kwa sababu nilijidai ninampenda sana huyo mtu kuliko hata Mungu, nikampa vyote, nafsi, roho na mwili. Wakati mwingine hata muda wa kwenda kuabudu ulipungua kwa kumpa huyo heart breaker muda mwingi zaidi.
Baada ya tukio hilo,niliamua kujipa likizo ya kumpenda mwanaume, yani nikaziba madirisha yote ya kumkaribisha mwanaume moyoni mwangu.
Siwachukii lakini nimejipa likizo kwa muda wa miaka mitano hivi, na sasa huu ni mwaka wa pili, ina maana bado miaka mitatu.
Je uamuzi wangu wa kujipa likizo ni sahihi?
Najiona ninaweza kuendelea na likizo hadi miaka mitatu iliyobakia iishe, je ni kweli au
naidanganya nafsi yangu.
Angalizo Marufuku kunitania Broken Heart!! Umesikia GY, Asprin, TF, Askofu na Teamo T, bila kumsahau Bigirita. Mjukuu mtiifu umesikia!! na wewe St. RR.