Hebu nisaidieni katika hili wanajamii

May 16, 2008
74
7
Wanajamii hebu tulijadilini hili.

Toka amefariki Dkt Daudi Ballali kumekuwa na mijadala mbalimbali kwenye vyombo mbalimbali vya habari, wanasiasa na hapa JF ambapo kuna post nyingi sana. Lakini pia kabla ya hapo pia kulikuwa na mijadala ya mahali alipokuwa anauguziwa hadi kufikia wengine kuanza kusema ameshafariki hata kabla ya familia yake kusema. Lakini katika yote hayo serikali ilikaa kimya kwa muda mrefu kabla ya kuja na taarifa moja kuwa haijui alipo na haimuhitaji ila ikimhitaji itamtafuta na kumpata.

Baada ya kufuatilia mijadala ya muda mrefu na kupima uzito (maana hamna hata mmoja aliyeleta ushahidi) nilijiridhisha mwenyewe ya kuwa Ballali amefariki kifo cha kawaida yaani bila mkono wa mtu.

Ila sasa baada ya kusikia taarifa za viongozi wa serikali yetu ( Waziri Simba, Membe na Mkurugenzi wa mawasiliano ikulu bwana Salva) naanza kuamini tofauti huku maswali yakianza kugonga tena kichwani mwangu.

Huyu bwana amefutwa kazi kwa sababu ya upotevu wa mabilioni ya pesa za walalahoi kama ikigundulika ameiba atakabiliwa na kesi ya kujibu, sasa serikali haiogopi mtu ambaye Mh Rais amekosa imani naye akatudanganya amekufa kwa kuishirkisha familia yake katika hili?

Au basi kama si yeye kutudanganya kwa kushirikiana na familia yake basi serikali na yenyewe inahusika katika kupanga kifo chake maana haiwezekani mtu ambaye ulikua hujui alipo leo ukiambiwa amekufa na kuonyeshwa jeneza unakubali bila hata kuuliza na kuja kuwalazimisha wengine waamini.

Au sasa serikali inataka niamini maneno ya baadhi ya watu kuwa yenyewe inahusika katika kifo chake?

Bado nataka kuendelea kuamini kuwa serikali yangu ni makini na wala haijahusika katika kifo cha Ballali hebu kama kuna mtu anaweza kunisaidia nikaamini tofauti na ninavyoanza kuamini baada ya kumsikiliza Salva.
 
Naona sasa tunaongezeka...Safi sana tu...Vilio vya wananchi visikilizwe na mambo yawekwe wazi!
Kama JK ameshindwa kuwashughulikia mafisadi then ajiuzulu ama bunge liwarudishe kwa wananchi.
 
Toka mwanzo nilikua naamini tofauti na ulivyokuwa unaamini wewe na nilifikiri labda nikipata taarifa za ndani (serikalini) ningeweza kuja kuelimisha na wewe uamini tofauti na unavyoamini wewe. Lakini....................

Kama kuna mtu anaweza kuja namaelezo kwa nn serikali inatetea hivi kuwa amekufa eti sababu balozi ameona jeneza nitamsikiliza kwa makini ili nirudi katika msimamo wangu kuwa Ballali amefariki kweli
 
Toka mwanzo nilikua naamini tofauti na ulivyokuwa unaamini wewe na nilifikiri labda nikipata taarifa za ndani (serikalini) ningeweza kuja kuelimisha na wewe uamini tofauti na unavyoamini wewe. Lakini....................

Kama kuna mtu anaweza kuja namaelezo kwa nn serikali inatetea hivi kuwa amekufa eti sababu balozi ameona jeneza nitamsikiliza kwa makini ili nirudi katika msimamo wangu kuwa Ballali amefariki kweli

Naona "Taarifa za ndani(serikalini)" Zimeku let down.
Pole kwa hilo.
Pole pia kwa watanzania wengine tuliokuwa na imani kuwa JK ni kiongozi shupavu na hivyo apewe muda wa kumshughulikia Ballali kabla hajafa.
Sasa kauli zao kuwa Ballali alikuwa mgonjwa kwa muda mrefu..Inadhihirisha kuwa walikuwa wanajua atakufa na hivyo kutuomba sisi wananchi tuwape muda huo wa ili Ballali aweze kufa.
 
Msaada ni tume huru ambapo mwenye chochote ataapishwa na kusema anachojua.
Kama ilikuwa siri alikolazwa wakati anaumwa hadi amekufa pia kuna utata mara kafia Boston mara nyumbani kwake Washington,tusitegemee miujiza bila ya tume.Utata wa namna hii huondolewa na tume maalum huru ambayo itachunguza kama ilivyokuwa kesi ya Zombe.
 
katika yote haya tutaumiza vichwa kunyambua yasiyonyambulika, Naamini Time will tell. Kuna vitu watajaribu kuficha havitafichika, hapo itapelekea hata vilivyoweze kufichwa awali navyo vifichuke.
Time.....time..... keep watching.
 
Mmmmmm!!!!!!!!, ina maana hakuna hata mtanzania mmoja aliyeshuhudia mazishi yake jamani? vipi hata waziri wa mambo ya nje hakuweza kuudhuria? Jamani vipi hata kapicha? aaaaaaaaaaaaa!!!, jamani serikali tuambieni jamani watoto wetu watatuuliza siku za usoni kuhusu kifo cha gavana wetu tutawajibu nini jamani?
 
hivi watanzania mlioko states hakuna hata mwenye picha ya mazishi? humu jf hakuna ndugu wa balali angalau atuthibitishie tumwache ndugu yao apumzike kwa amani?

kama balali hakufa, jambo hili ni nzito mno, na kwa kuwa MUNGU YUKO, MAAJABU YATATOKEA NA AKIIBUKA DOLA LA MAFISADI LITAKUWA NDO MLINAFUNGA PAZIA, YAANI MOVE IMEISHA

kama balali amekufa kwa mkono wa binadamu yaani kuficha ukweli ili watu waendelee kutesa na pesa za maskini watanzania, basi damu yake itawalilia mafisadi kokote waliko, watalaaniwa kwa dham,bi ya kaini na abel
 
Mr. Politician

Hapo ndipo kuna kizaazaaa nguo kuchanika, tangu nimezaliwa inakuwa mara ya kwanza kusikia kihoja kama hiki, nyumbani kwa marehu kuwekewa ulinzi!!!! Daaaa, kwenye msiba ni mahali panapohitaji mkusanyiko wa watu ili kuweza kuhani msiba huo, sasa kwa Dr. Balali mambo si hivyo,

unajua iko siku mawe yatasema, hapo mabubu watakapokuwa wakiimba wimbo wa kizigua. Jamani huu uoga wetu ni nani kautia mioyoni mwetu? kohoji kwetu mwiko, na hata hao waandishi ni 2% tu ndiyo wenye mori, mungu tusaidie.
 
Mr. Politician

Hapo ndipo kuna kizaazaaa nguo kuchanika, tangu nimezaliwa inakuwa mara ya kwanza kusikia kihoja kama hiki, nyumbani kwa marehu kuwekewa ulinzi!!!! Daaaa, kwenye msiba ni mahali panapohitaji mkusanyiko wa watu ili kuweza kuhani msiba huo, sasa kwa Dr. Balali mambo si hivyo,

unajua iko mawe yatasema, hapo mabubu watakapokuwa wakiimba wimbo wa kizigua. Jamani huu uoga wetu ni nani kautia mioyoni mwetu? kohoji kwetu mwiko, na hata hao waandishi ni 2% tu ndiyo wenye mori, mungu tusaidie.
 
hivi watanzania mlioko states hakuna hata mwenye picha ya mazishi? humu jf hakuna ndugu wa balali angalau atuthibitishie tumwache ndugu yao apumzike kwa amani?

kama balali hakufa, jambo hili ni nzito mno, na kwa kuwa MUNGU YUKO, MAAJABU YATATOKEA NA AKIIBUKA DOLA LA MAFISADI LITAKUWA NDO MLINAFUNGA PAZIA, YAANI MOVE IMEISHA

kama balali amekufa kwa mkono wa binadamu yaani kuficha ukweli ili watu waendelee kutesa na pesa za maskini watanzania, basi damu yake itawalilia mafisadi kokote waliko, watalaaniwa kwa dham,bi ya kaini na abel

Hivi ukionyeshwa picha ya Ballali akiwa amelala ndani ya jeneza na pamba puani itatosha kukufanya uamini amekufa?

Tuombe Mungu maajabu yatokee ila hata shetani huwa ana nguvu za kuwasaidia wanaomtumikia, labda kwa wengine ambao sio mawakala wa shetani tumwombe Mungu miujiza itokee.
 
Mr. Politician

Hapo ndipo kuna kizaazaaa nguo kuchanika, tangu nimezaliwa inakuwa mara ya kwanza kusikia kihoja kama hiki, nyumbani kwa marehu kuwekewa ulinzi!!!! Daaaa, kwenye msiba ni mahali panapohitaji mkusanyiko wa watu ili kuweza kuhani msiba huo, sasa kwa Dr. Balali mambo si hivyo,

Hivi hasa hasa Hao walinzi walikuwa wanalinda nini? Serikali ilikuwa inajihami na nini juu ya hilo? Hatuwezi kujua lakini!
 
Hivi hasa hasa Hao walinzi walikuwa wanalinda nini? Serikali ilikuwa inajihami na nini juu ya hilo? Hatuwezi kujua lakini!

Nani anajua ndugu yangu? wao ndiyo wanaojua kile kinachojiri sisi ni watazamaji wa ngoma hii, ila pale tunapolazimishwa kuicheza huku tukiwa hatujui tuanzie wapi
 
Wanajamii hebu tulijadilini hili.

Toka amefariki Dkt Daudi Ballali kumekuwa na mijadala mbalimbali kwenye vyombo mbalimbali vya habari, wanasiasa na hapa JF ambapo kuna post nyingi sana. Lakini pia kabla ya hapo pia kulikuwa na mijadala ya mahali alipokuwa anauguziwa hadi kufikia wengine kuanza kusema ameshafariki hata kabla ya familia yake kusema. Lakini katika yote hayo serikali ilikaa kimya kwa muda mrefu kabla ya kuja na taarifa moja kuwa haijui alipo na haimuhitaji ila ikimhitaji itamtafuta na kumpata.

Baada ya kufuatilia mijadala ya muda mrefu na kupima uzito (maana hamna hata mmoja aliyeleta ushahidi) nilijiridhisha mwenyewe ya kuwa Ballali amefariki kifo cha kawaida yaani bila mkono wa mtu.

Ila sasa baada ya kusikia taarifa za viongozi wa serikali yetu ( Waziri Simba, Membe na Mkurugenzi wa mawasiliano ikulu bwana Salva) naanza kuamini tofauti huku maswali yakianza kugonga tena kichwani mwangu.

Huyu bwana amefutwa kazi kwa sababu ya upotevu wa mabilioni ya pesa za walalahoi kama ikigundulika ameiba atakabiliwa na kesi ya kujibu, sasa serikali haiogopi mtu ambaye Mh Rais amekosa imani naye akatudanganya amekufa kwa kuishirkisha familia yake katika hili?

Au basi kama si yeye kutudanganya kwa kushirikiana na familia yake basi serikali na yenyewe inahusika katika kupanga kifo chake maana haiwezekani mtu ambaye ulikua hujui alipo leo ukiambiwa amekufa na kuonyeshwa jeneza unakubali bila hata kuuliza na kuja kuwalazimisha wengine waamini.

Au sasa serikali inataka niamini maneno ya baadhi ya watu kuwa yenyewe inahusika katika kifo chake?

Bado nataka kuendelea kuamini kuwa serikali yangu ni makini na wala haijahusika katika kifo cha Ballali hebu kama kuna mtu anaweza kunisaidia nikaamini tofauti na ninavyoanza kuamini baada ya kumsikiliza Salva.

kwa kuanzia tu,

walioshiriki kwenye wizi wa BoT ni wengi na sio Ballali peke yake. Ukichukulia hilo kwenye mawazo utagundua kuwa wanaotaka kumfanya Ballali kama yeye pekee ndiye mtuhumiwa kwenye hii case wana alot to gain na kifo cha Ballali kuliko hata huyo Ballali mwenyewe.
 
Kwani Mzee Ballali kazikwa kwenye "unamarked grave"? Kama siyo, basi wasioamini watafute namna ya kufukua kaburi ili wapate sampuli ya angalau nywele mbili-tatu halafu wakapime DNA. Vinginevyo kama wamemchoma moto, basi sanasana ni meno pekee yake yangefaa kwa DNA test. Kama vyote haviwezekani (yaani kupata ushahidi wowote ule huria na wa kisayansi wa kifo cha Ballali) basi watu wana kila haki kutilia mashaka kifo cha Ballali.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom