Mathias BM
Member
- Jun 28, 2012
- 21
- 3
Wana jf tushirikishane hili suala muhimu! wapenzi au wanandoa wengi wanapotaka kuanza mahusiano yao huulizana maswali kama haya...'unasoma wapi, unafanya kazi gani, we ni mnene au mwembamba n.k' Halafu wakishajua majibu hayo, hapo ndo husingizia dhana ya kupendana kwa dhati kisha kuanza mahusiano! jamani, wote tunafahamu kuwa maisha ya watu hubadilika na maumbile pia hubadilika, Je ina maana kwamba mabadiliko hayo huashiria mwisho wa safari yao ya uhusiano na kupotea kwa dhana ya kupendana? Hebu jaribu kumuuliza mwenzi wako kwa nia njema 'amekupendea nini? akikupa sababu jaribu kuhusisha sababu hiyo na maelezo hapo juu. Je, ana upendo wa dhati kutoka moyoni au anasingizia na kubadilisha dhana ya nakupenda. Fanya uchunguzi wa kina kisha toa maoni yako hapa..!