Hekima Ufunuo
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 220
- 11
Mswada wa afya uliokuwa unajadiliwa nchini Marekani Kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja sasa umepitishwa na Baraza tayari kusainiwa na Raisi Obama.
Kwa wafuatiliaji wa siasa mjadala wake unatakiwa kutupa sisi somo kubwa sana katika medani ya Demokrasia, naamini M. M Mwanakijiji atatuandalia mada juu ya hili.
MIMI NIMEJIFUNZA NINI?
1. Mpambano ulikuwa kati ya Republican na Democrat, Hakuna Repblican hata mmoja aliyeunga mkono mswada huu.- Wapiganaji/ Wapamabanji waliendela na mpambano mpaka mwisho.
2 Wale Democrat ambao hawakuwa wameridhika, hawakujificha walionyesha wazi msimamo wao mpaka zilipofanyika juhudi za kuwashawishi nao kuridhika ndipo walipoungana na wenzao- HAKUNA MSIMAMO WA CHAMA, HAKUNA KIKAO CHA KAMATI YA CHAMA NA WALA HAKUNA CHAMA KILITAKA KUNINYANGANYA KADI. yote yalikuwa maslahi ya taifa na wananchi wake.
3. Wingi wa wajumbe wa Democrat ndani ya Baraza na pia idadi ya wajumbe wa Repblican ilikuwa ni changamoto nzuri sana kwa mswada wenyewe. siyo baraza lote kuwa la chama kimoja kama hapa kwetu. Hoja zimechambuliwa na ufafanuzi kufanyika kwa makini mpaka kila mmoja ameridhika.
4. Maandamano niliyoyaona kwenye miji mbalimbali hakuna polisi hata mmoja aliyewapiga mabomu, Ustarabu ni wa kiwango cha juu kwa wote polisi na hata waandamanji.- kwetu inawezekana?
Mwisho
Nimejifunza mengi sana, hata hizi kanuni za uchaguzi zinatotungwa sasa Dk slaa asingelalamika kama mjadala wa sheria ungekuwa wa wazi kama huu wa Afya- Marekani.
Kwa wafuatiliaji wa siasa mjadala wake unatakiwa kutupa sisi somo kubwa sana katika medani ya Demokrasia, naamini M. M Mwanakijiji atatuandalia mada juu ya hili.
MIMI NIMEJIFUNZA NINI?
1. Mpambano ulikuwa kati ya Republican na Democrat, Hakuna Repblican hata mmoja aliyeunga mkono mswada huu.- Wapiganaji/ Wapamabanji waliendela na mpambano mpaka mwisho.
2 Wale Democrat ambao hawakuwa wameridhika, hawakujificha walionyesha wazi msimamo wao mpaka zilipofanyika juhudi za kuwashawishi nao kuridhika ndipo walipoungana na wenzao- HAKUNA MSIMAMO WA CHAMA, HAKUNA KIKAO CHA KAMATI YA CHAMA NA WALA HAKUNA CHAMA KILITAKA KUNINYANGANYA KADI. yote yalikuwa maslahi ya taifa na wananchi wake.
3. Wingi wa wajumbe wa Democrat ndani ya Baraza na pia idadi ya wajumbe wa Repblican ilikuwa ni changamoto nzuri sana kwa mswada wenyewe. siyo baraza lote kuwa la chama kimoja kama hapa kwetu. Hoja zimechambuliwa na ufafanuzi kufanyika kwa makini mpaka kila mmoja ameridhika.
4. Maandamano niliyoyaona kwenye miji mbalimbali hakuna polisi hata mmoja aliyewapiga mabomu, Ustarabu ni wa kiwango cha juu kwa wote polisi na hata waandamanji.- kwetu inawezekana?
Mwisho
Nimejifunza mengi sana, hata hizi kanuni za uchaguzi zinatotungwa sasa Dk slaa asingelalamika kama mjadala wa sheria ungekuwa wa wazi kama huu wa Afya- Marekani.